Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Utegi hadi Kirongwe?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Majibu ya Serikali kwa kweli yanasikitisha. Barabara hii ni ya ahadi tangu Awamu ya Tatu ya Hayati Mheshimiwa Rais Mkapa. Sasa maswali yangu yangu mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, tuna barabara ya kiusalama ambayo iko Jimbo la Tarime Vijijini inayoanzia Jimbo la Rorya, inapita Susuni - Mwema - Sirari - Mbogi - Gwitio mpaka Nyanungu. Barabara hii imekuwa ikiahidiwa itajengwa kiwango cha lami mpaka leo. Ni lini sasa barabara hii itaenda kujengwa kwa kiwango cha lami ili kuweza kuimarisha usalama pale mpakani? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuna barabara ya kuanzia Utegi inapita Kowaki kwenda Kinesi. Ni barabara pia ambayo imeahidiwa toka Awamu ya Nne lakini mpaka leo haijajengwa. Barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi ukizingatia kule tuna ziwa, tunavua samaki na mazao mengine: Ni lini barabara hii itae

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ester Nicholas Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ya ulinzi ambayo inaanzia Kirongwe kupita Mriba hadi Kegongo ni barabara ya Ulinzi kati ya Tanzania na mpaka wa Kenya. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sasa Serikali inahakikisha kwamba barabara hii inapitika muda wote wa mwaka. Kwa hiyo, imetengewa fedha kuhakikisha kwamba inatengenezwa kwa kiwango cha changarawe ili iweze kupitika kuimarisha ulinzi.

Mheshimiwa Spika, barabara aliyotaja ya Kowaki kwenda Kinesi tunajua inaunganisha Kowaki na Hadari, na ni kweli ni barabara ya uchumi sana kwa Mkoa wa Mara na hasa kwa Jimbo la Rorya. Tunachofanya sasa hivi pia ni kuhakikisha kwamba tunatenga fedha; na ukiangalia kwenye bajeti ya mwaka huu, tumetenga fedha za kutosha kuhakikisha kwamba tunaitengeneza iweze kupitika wakati huo Serikali inatafuta fedha ili ianze kufanya kufanya usanifu wa kina.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Utegi hadi Kirongwe?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa barabara ya Kahama - Bulige Mwakitolio mpaka Solwa ni barabara ya kimkakati na iko kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi; je, ni lini ujenzi wa kiwango cha lami utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Christina Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ya Kahama kwenda Solwa imeshafanyiwa usanifu wa kina na sasa Serikali inatafuta fedha ili kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Utegi hadi Kirongwe?

Supplementary Question 3

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara ya Morogoro - Dodoma ni barabara ambayo inatumiwa na wananchi wengi na hususan viongozi wa kiserikali na wanadiplomasia wa kigeni wanapokuwa wanatembelea Makao Makuu.

Mheshimiwa Spika, barabara hii imekuwa chakavu maeneo mengi na hususani kutoka Dumila – Gairo: Swali langu, Serikali inampango gani wa kujenga barabara hii ili kuondoa vifo vya ajali vinavyotokea na kunusuru Maisha ya wananchi?

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Agnesta Lambert, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba barabara hii imechakaa na traffic imeongezeka sana. Tayari tumeshafanya usanifu wa kina ikiwa ni pamoja na kuipanua hii barabara. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti tunayoiendea sasa hivi, maeneo mengi ambayo ni korofi yatakarabatiwa ikiwa ni pamoja na mpango wa kuifumua barabara nzima ili kuipanua na kupunguza hizo ajali na mashimo ambayo yapo.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Utegi hadi Kirongwe?

Supplementary Question 4

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Barabara inayotoka Bulyanhulu kwenda Kahama ni barabara ya kimkakati na inachangia pato kubwa katika nchi hii. Sasa swali langu lilikuwa: Ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa barabara hii ambayo kimsingi ni barabara ya muda mrefu na ni muhimu sana katika Jimbo la Msalala? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kassim Iddi, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyotaja kutoka Bulyanhulu kwenda Kahama ipo kwenye mpango wa bajeti tuliyoipanga na pia ni barabara ambayo wenzetu wa Mgodi wa Tembo Barrick wamekubali kuisaidia Serikali kuijenga hiyo barabara. Kwa hiyo, tayari Serikali inaendelea na mazungumzo na wenzetu, lakini pia Serikali imepanga bajeti kuanza kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Utegi hadi Kirongwe?

Supplementary Question 5

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Naomba kumwuliza Naibu Waziri wa Ujenzi: Ni lini Serikali itatafuta fedha ya kukamilisha ujenzi wa barabara ya Amkeni – Kitangali hadi Mtama kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maimuna Mtanda, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoanisha Serikali inaitambua. Tutakamilisha kwanza kufanya usanifu wa kina halafu baada ya hapo, Serikali itatafuta fedha ili kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Utegi hadi Kirongwe?

Supplementary Question 6

MHE. MWITA B. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba niulize swali la nyongeza. Barabara ya Nyamswa – Bunda – Bulamba na barabara ya Sanzate – Mgeta – Nata, wanachi wamebomolewa nyumba zao. Ni lini wananchi hao watapewa fidia ya nyumba zao?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwita Getere Mbunge wa Mbunda Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara mbili alizozitaja ya Nyamuswa – Bunda kwenye Bulamba na Nyamuswa kwenda upande wa Nata ni barabara ambazo zinajengwa kwa kiwango cha lami. Tayari tulishafanya tathimini na sasa hivi Wizara ya Fedha inafanya uhakiki wa mwisho ili kuandaa malipo kwa wananchi ambao wamepisha ujenzi wa hizo barabara mbili.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Utegi hadi Kirongwe?

Supplementary Question 7

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Ni lini barabara ya kutoka Lyazumbi hadi Kabwe itajengwa kwa kiwango cha lami? Kwa sababu kule kuna bandari kwa uchumi wa Mkoa wa Rukwa.

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Rukwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Lyazumbi – Kabwe ni barabara ambayo ilikuwa finyu. Cha kwanza ambacho Serikali imefanya baada ya kujenga bandari ilikuwa ni kuipanua ile barabara ili iweze kupitisha magari makubwa na pia kujenga madaraja ambayo sasa yanaweza yakahimili magari yenye uzito mkubwa na hatua ya sasa ni kukamilisha usanifu ili kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami.