Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, Chuo cha Utalii Dar es Salaam na Vyuo vingine vya utalii vimetoa wafanyakazi wangapi ngazi ya Menejimenti katika Hoteli za Serengeti na Ngorongoro?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo majibu aliyoyatoa Mheshimiwa Waziri, baada ya kumpata Mkuu wa Chuo Dar es Salaam ambaye ameanza kutangaza habari za chuo hicho, Chuo chetu cha Utalii - Dar es Salaam kinajiandaa kuwa kituo cha umahiri. Je, Serikali imefikia hatua gani katika mipango yake ili kuona kabisa kwamba watoto wanaotoka pale wanakuwa mahiri kweli kweli?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kumekuwa na malalamiko mengi sana kuhusu wahudumu wetu, yaani wanaita Wazungu Customer Care, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba vijana wetu wote wanaomaliza Vyuo vya Utalii vya Binafsi na vya Serikali wanapata mafunzo kazini ili watoe huduma bora katika mahoteli yetu? Ahsante.

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Ntara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo chetu cha Utalii kilichopo Dar es Salaam na matawi yake kule Arusha na Mwanza, kimefanya maboresho katika mitaala ya mafunzo ili kuongeza umahiri wa wahitimu wetu katika sekta ya utalii. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya kuimarisha mitaala hii, tunayo imani kubwa sasa kwamba mafunzo yatakayotolewa na umahiri wa wahitimu wetu utakuwa wa hali ya juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kwenye eneo la customer care, ni kweli imekuwepo changamoto ya wahudumu wetu kulalamikiwa mara kwa mara. Nataka nimhakikishie kwamba jambo hili linafanyiwa kazi kwa umakini mkubwa na kama anafuatilia kwa ukaribu huduma sasa hivi za watu wetu zimeanza kuimarika kwa kiasi kikubwa.