Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hafidh Ali Tahir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dimani

Primary Question

MHE. HAFIDH ALI TAHIR (K.n.y. MHE. ALI SALIM KHAMIS) aliuliza:- Kisiwa cha Shungimbili kilichopo Wilaya ya Mafia kinamilikiwa na mwekezaji ambaye amekibadilisha jina na kukiita Thanda, mmiliki wake ni Kampuni ya Utalii ya Zululand ya Afrika Kusini. Aidha, kuna madai kuwa kisiwa hicho kimeuzwa kwa mwekezaji huyo; kwenye kisiwa hicho kuna hoteli yenye hadhi ya dunia na ndicho kisiwa ghali duniani kuishi kwani kwa siku ni USD 10,000 na ili upate chumba ni lazima ufanye booking kwa muda usiopungua siku saba:- (a) Kama kisiwa hicho kimeuzwa: Je, kimeuzwa shilingi ngapi na hoteli hiyo inalipa kodi kiasi gani kwa Serikali? (b) Je, Wizara ya Maliasili na Utalii inashirikiana vipi na Wizara ya Utalii Zanzibar hasa ukizingatia Wizara ya Mambo ya Nje ni ya Muungano katika Mikataba ya Kimataifa?

Supplementary Question 1

MHE. HAFIDH ALI TAHIR: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake sahihi, lakini nina maswali madogo ya nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri, anataka kuliambia Bunge hili kwamba suala la Kampuni ya Zululand kwamba ni ya Afrika Kusini ni kauli ya upotoshwaji kwamba inamiliki Kisiwa hiki?
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri atuambie, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kati ya utalii Zanzibar na ile ya Muungano, wanashirikianaje katika suala zima la utalii katika ulimwengu? Ahsante.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, ni kweli kama nilivyofafanua kwenye jibu langu la msingi kwamba Kisiwa cha Shungimbili na kazi inayofanyika hivi sasa pale, kwa ujenzi wa ile hoteli ya Kitalii, ile lodge; inaendelea kufanyika chini ya MPRU ambayo iko chini ya Wizara ya Kilimo na Uvuvi, kazi hiyo itakapokamilika, itakapoingia sasa kwenye masuala ya uwekezaji yenyewe; ya uendeshaji wa biashara yenyewe ya hoteli; pale sasa ndiyo Wizara ya Maliasili na Utalii inapoingia, watakapokuja sasa kuomba Leseni ya Biashara ya Utalii ambapo sasa watalazimika kuomba leseni hiyo chini ya chombo chetu cha Tanzania Tourism Licencing Board. Pale tutaweza sasa kutoa hiyo leseni, ikiwa watakidhi vigezo vyote ambavyo vipo kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ushirikiano kati ya Bara na Visiwani, ni kama nilivyojibu kwenye swali la msingi na niliorodhesha masuala kadhaa ambayo tunayafanya kwa kushirikiana baina ya pande zetu zote mbili za utalii. Kwa faida ya Mheshimiwa Mbunge mwuliza swali pamoja na Wabunge wengine, nimesema ushirikiano kati ya pande mbili za Muungano, unajumuisha maeneo ya utangazaji wa vivutio vya Tanzania Kimataifa kama nchi moja, utayarishaji taarifa na ujenzi wa mfumo imara wa ukusanyaji wa takwimu ambapo takwimu hizo sasa ndiyo zinatumika Kimataifa kwa ajili ya kuifahamu vizuri zaidi nchi yetu na masuala yanayohusiana na utalii, kwa sababu ni takwimu zinazohusiana na utalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nimetaja hayo mawili miongoni mwa manne ambayo nimekwishayataja, lakini mtu anaweza kurejea kwenye jibu langu la msingi kwamba hayo ndiyo maeneo ambayo tunafanya ushirikiano au mashirikiano baina ya pande hizi mbili za Muungano.

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAFIDH ALI TAHIR (K.n.y. MHE. ALI SALIM KHAMIS) aliuliza:- Kisiwa cha Shungimbili kilichopo Wilaya ya Mafia kinamilikiwa na mwekezaji ambaye amekibadilisha jina na kukiita Thanda, mmiliki wake ni Kampuni ya Utalii ya Zululand ya Afrika Kusini. Aidha, kuna madai kuwa kisiwa hicho kimeuzwa kwa mwekezaji huyo; kwenye kisiwa hicho kuna hoteli yenye hadhi ya dunia na ndicho kisiwa ghali duniani kuishi kwani kwa siku ni USD 10,000 na ili upate chumba ni lazima ufanye booking kwa muda usiopungua siku saba:- (a) Kama kisiwa hicho kimeuzwa: Je, kimeuzwa shilingi ngapi na hoteli hiyo inalipa kodi kiasi gani kwa Serikali? (b) Je, Wizara ya Maliasili na Utalii inashirikiana vipi na Wizara ya Utalii Zanzibar hasa ukizingatia Wizara ya Mambo ya Nje ni ya Muungano katika Mikataba ya Kimataifa?

Supplementary Question 2

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante. Ningependa tu kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba kwa kuwa hoteli hizi ambazo ni maalum sana, ambazo zinaitwa ‘za Kimataifa’, zinazojengwa kwenye maeneo maalum, zimekuwa zikichukua ajira za wafanyakazi wengi kutoka nje, zile ambazo ni muhimu sana na kuwaacha wazawa wakifanya kazi zile ndogo ndogo kwenye hayo mahoteli makubwa. Je, Serikali inajipanga vipi kuhakikisha kwamba nafasi zile kubwa zinachukuliwa na wazawa kuliko wafanyakazi kutoka nje?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli kwa ufupi kabisa! Ukweli ni kwamba mfanyabiashara anapotafuta mtu wa kumwajiri ili aweze kutoa huduma katika eneo lake la biashara, lazima atakuwa anatafuta mtu ambaye atamwezesha kupata tija katika biashara yake. Kwa hiyo, hilo linakuwa ni suala la ushindani.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeliona jambo hili kwamba kwa upande wa nchi yetu, tunao upungufu kwa kiwango fulani juu ya kuweza kushindana katika masoko haya ambayo yanahusisha ushindani wa Kimataifa. Kwa hiyo, hatua ya kwanza ambayo tutaifanya ni ile ambayo tunaboresha zaidi Vyuo vyetu ili tuboreshe zaidi wananchi wetu, waingie, wajifunze; lakini siyo kujifunza tu darasani, wakitoka pia waweze kufanya kama walivyojifunza.
Mheshimiwa Naibu Spika, mambo mengine, kwa mfano ya hospitality ni zaidi hata ya kujifunza darasani, lakini pale ni lazima mtu uweze ku-gain competencies ambazo zitaweza kukuwezesha kupambana kwenye soko la ajira; lakini haitafikia wakati tukaweza kumlazimisha mfanyabiashara kumwajiri mtu; isipokuwa tutajenga mazingira ya kuwawezesha Watanzania wawe washindani wazuri zaidi.

Name

Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Primary Question

MHE. HAFIDH ALI TAHIR (K.n.y. MHE. ALI SALIM KHAMIS) aliuliza:- Kisiwa cha Shungimbili kilichopo Wilaya ya Mafia kinamilikiwa na mwekezaji ambaye amekibadilisha jina na kukiita Thanda, mmiliki wake ni Kampuni ya Utalii ya Zululand ya Afrika Kusini. Aidha, kuna madai kuwa kisiwa hicho kimeuzwa kwa mwekezaji huyo; kwenye kisiwa hicho kuna hoteli yenye hadhi ya dunia na ndicho kisiwa ghali duniani kuishi kwani kwa siku ni USD 10,000 na ili upate chumba ni lazima ufanye booking kwa muda usiopungua siku saba:- (a) Kama kisiwa hicho kimeuzwa: Je, kimeuzwa shilingi ngapi na hoteli hiyo inalipa kodi kiasi gani kwa Serikali? (b) Je, Wizara ya Maliasili na Utalii inashirikiana vipi na Wizara ya Utalii Zanzibar hasa ukizingatia Wizara ya Mambo ya Nje ni ya Muungano katika Mikataba ya Kimataifa?

Supplementary Question 3

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Nataka kumwuliza Mheshimiwa Waziri; kwa vile utalii ni moja kati ya tegemeo kubwa la uchumi wa nchi yetu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea uwezo Mabalozi hasa walioko nchi mbalimbali za Latin America na America kuwa na uwezo wa kuweza kufanya ushawishi na kuweza kuunganisha Mashirika ya Kitalii yaliyoko katika nchi hasa za Ujerumani na Ufaransa kuweza kuja katika nchi zetu hizi na kuwa na mfano wa nchi ambazo wameweza kufanikiwa sana tukilinganisha nchi za Mauritius na nchi nyinginezo za Mashariki ya mbali ambazo zimefanikiwa sana katika suala hili la utalii?

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nakushukuru sana kwa kuniona, lakini napenda nianze kwa kweli kwa kumpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Sera ya Serikali ya economic diplomacy, hii ni moja ya nguzo ya kujenga mapato ya Serikali kwa kuzitumia Balozi zetu kutusaidia katika kutangaza utalii katika maeneo yao na tayari tumeanza kuandaa vitini ambavyo tutawapelekea Mabalozi ili hata mgeni akiingia kwenye Ubalozi wetu, ajue tayari ni vitu gani viko Tanzania. Kwa hiyo, tunawaomba Waheshimiwa Wabunge, tusaidiane katika jambo hili ili kuweza kufanikisha sera hii.