Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Pamoja na juhudi za Serikali kupeleka huduma za umeme vijijiji vya Wilaya ya Kiteto hasa Kata za Lengatei, Kijungu, Magungu, Songambele, Ndedo na Makame, hawajafikiwa kabisa na utaratibu huu wa REA. Je, Serikali itapeleka lini umeme katika vijiji vilivyotajwa?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu ya kutia matumaini, naomba kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kiteto kwa sehemu kubwa inakaliwa na jamii ya wafugaji ambao shule haijawa kipaumbele sana, hasa kwa watoto wa kike. Kwa sehemu kubwa ukombozi mkubwa ni kuwa na shule za bweni ambako wasichana wanaweza wakabaki shuleni badala ya kurudi nyumbani kukwepa kuolewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachosikitisha ni kwamba kuna baadhi ya sekondari za kata tena za muda mrefu zenye mabweni, kama sekondari ya Ndedo na Lesoit ambazo ni za bweni na zina wasichana wengi wa Kimasai, lakini inasikitisha kwamba hizo shule za kata hadi leo hazina umeme. Na sio hizo shule tu hata Kituo cha Afya cha Osteti ambacho kinasaidia sana huduma za afya kwa akina mama hakuna umeme.
Je, ni lini Naibu Waziri sasa atachukua jukumu la makusudi kutembelea Wilaya ya Kiteto, hasa maeneo haya niliyoyataja, ili kujionea mwenyewe jinsi ambavyo sekondari hizo hazina walimu na hata maabara tulizojenga hazitumiki kwa ajili ya kukosa umeme?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, naomba ku-declare interest kwamba nimetoa mikopo kwa takribani miaka 20 sasa katika Mkoa wangu wa Manyara. Uzoefu unaonyesha kwamba ufanisi mkubwa kwa kurejesha mikopo kwa wanawake na vijana ni katika vijiji vile vyenye umeme wa uhakika. Je, nini kauli ya Serikali kabla ya kutoa hizo shilingi milioni 50 katika maeneo haya ya wafugaji na mikoa ya pembezoni kuhakikisha kwamba vijiji hivyo vitakuwa na umeme kabla ya kusambaza hizo fedha?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa Mradi wa REA Awamu ya Pili ulipokamilika maeneo mengi sana ya taasisi hayakupatiwa umeme. Nitoe rai tu kwamba, REA Awamu ya Tatu inayoanza sasa itaweka kipaumbele sana kupeleka umeme kwenye taasisi za umma ikiwemo shule, sekondari, pamoja na taasisi nyingine. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Umbulla kwamba, shule ya sekondari ambayo ameitaja Lesoit pamoja na shule ya Ndedo pamoja na Kituo cha Afya cha Osteti vitaanza kabisa kupelekewa umeme kwenye mradi wa REA Awamu ya Tatu unaoanza hivi karibuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, nimpongeze tu Mheshimiwa Mbunge, amekuwa akifuatilia sana masuala haya, lakini nimhakikishie mbali na vituo vya afya kwa sababu viko vingi. Viko vituo vya afya katika eneo lake la Njiapanda ambako pia kuna kituo cha afya kitawekewa umeme, lakini kuna eneo la Songambele halijawekewa umeme pamoja na vituo vingi sana ikiwemo na vijiji vya katikati na vyenyewe vitapatiwa umeme katika REA Awamu ya Tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitapenda kutembelea, kwa ridhaa yako, mara baada ya Bunge tufuatane na Mheshimiwa Mbunge moja kwa moja ikwezekana tuanze kukaa hata kabla ya kuanza kutembelea maeneo yake.
Kuhusiana na vijiji ambavyo vitapewa mikopo au ruzuku ya shilingi milioni 50 kupata umeme. Tutaanza kuvipatia umeme, tutakaa na wenzetu wa TAMISEMI ili kusudi shilingi milioni 50 zisiende bure, ili waanze kutumia umeme mara watakapoanza kupata pesa hizo.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Pamoja na juhudi za Serikali kupeleka huduma za umeme vijijiji vya Wilaya ya Kiteto hasa Kata za Lengatei, Kijungu, Magungu, Songambele, Ndedo na Makame, hawajafikiwa kabisa na utaratibu huu wa REA. Je, Serikali itapeleka lini umeme katika vijiji vilivyotajwa?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi, ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Mradi wa REA Awamu ya Pili umeshapita baadhi ya maeneo tena ya barabarani katika Jimbo la Lushoto. Je, Serikali inaniahidi lini itapeleka umeme wa REA Awamu ya Tatu hasa katika Kata za Kilole, Kwekanga, Makanya, Ngwelo pamoja na maeneo mengine yaliyobaki?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kusema tu Mradi wa REA Awamu ya Tatu unapeleka umeme katika vijiji vyote, katika vitongoji vyote na katika taasisi zote za umma, lakini hata miji ambayo pia, iko isolated. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kijiji chake cha Kilole kitapelekewa umeme hata kijiji cha Makanya kitapelekewa umeme kwa sababu, ni mpango wa Serikali kupeleka umeme katika vijiji vyote kupitia REA Awamu ya Tatu.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Pamoja na juhudi za Serikali kupeleka huduma za umeme vijijiji vya Wilaya ya Kiteto hasa Kata za Lengatei, Kijungu, Magungu, Songambele, Ndedo na Makame, hawajafikiwa kabisa na utaratibu huu wa REA. Je, Serikali itapeleka lini umeme katika vijiji vilivyotajwa?

Supplementary Question 3

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kabla ya kuanza kwa Mradi wa REA III, kuna baadhi ya maeneo Miradi ya REA I na REA II bado haijakamilika ikiwemo katika baadhi ya maeneo ya Jimbo la Momba. Sasa tunataka assurance ya kukamilisha miradi kwanza ya REA I na REA II kabla ya hiyo REA III, lini itakamilika miradi hii, REA I na REA II? Ahsante Sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Silinde kwanza nakupongeza, Miradi ya Awamu ya Pili ya REA imeshakamilika na mahali ambapo Mradi wa REA ikitokea kwamba haukukamilika ni vijiji ambavyo sasa vitaanza kutekelezwa katika Miradi ya REA Awamu ya Tatu.
Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Silinde kama kuna kijiji specific ambacho hakijakamilika kupitia mradi wa pili, naomba tukae na tuanze kutekeleza hata kabla ya kuingia Mradi wa REA Awamu ya Tatu. Na vijiji vyote ambavyo havikukamilika kupitia miradi ya REA Awamu ya Pili, ambavyo havijakamilika, vitaanza kukamilika kwanza ndio tunaingia kwenye REA Awamu ya Tatu. Kwa hiyo, vijiji vyote Mheshimiwa Silinde katika Jimbo lako la Momba vitapatiwa umeme wa uhakika kupitia Mradi wa REA Awamu ya Tatu.