Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hafidh Ali Tahir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dimani

Primary Question

MHE. HAFIDH ALI TAHIR aliulliza:- Bunge la Jamhuri ya Muungano hupitisha Bajeti ya Serikali kwa kila Wizara kwa mwaka ikiwemo Wizara ya Mambo ya Ndani:- (a) Je, inakuwaje Wilaya yenye vituo saba vya polisi ina gari moja tu na inapatiwa lita tano hadi saba tu za mafuta kwa siku? (b) Je, Serikali iko tayari kuziongezea mafuta na magari Wilaya za Magharibi A na B zenye vituo vya polisi vya Fumba, Mbweni, Mazizini, Mwanakwerekwe, Kijitoupele, Fuoni, Airport na Mfenesini ambazo ni gari moja tu kila Wilaya ili kukongeza ufanisi na kuendana na kasi ya hapa kazi tu hasa ukizingatia kuwa Zanzibar inajiandaa na marudio ya Uchaguzi Mkuu?

Supplementary Question 1

MHE. HAFIDH ALI TAHIR: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jawabu zake, lakini swali langu lilikuwa na msisitizo ukizingatia kuwa Zanzibar inajiandaa na marudio ya Uchaguzi Mkuu, ndiyo sababu swali langu kubwa lilikwenda huko. Kurudiwa kwa Uchaguzi Zanzibar siyo jambo geni, mwaka 1961 Uchaguzi ulifutwa na ukarudiwa mwaka1963. (Makofi)
Sasa kwa tokeo hili Mheshimiwa Waziri swali langu la kwanza, huoni kwamba kuna haja ya kuweka umaksudi wa kupatia usafiri Wilaya nilizozitaja wakati huu tukielekea katika uchaguzi ili yale mazombi yanayozungumzwa yapunguke kufanya kazi?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili, namwomba Waziri aniambie kwamba kwenye Bajeti ijayo ameahidi kwamba atatupatia magari Wilaya alizozitaja, Mheshimiwa Naibu Waziri naomba ukubali hii ni ahadi na nikungoje kwenye bajeti? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie kwamba nilizungumza vilevile kuhusiana na hili suala la magari ambalo kwa bahati mbaya kuna baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wamelipotosha kwa makusudi ama hawajalielewa. Lakini naomba nichukue fursa hii kwa kueleza tu kwa ufupi ni kwamba Jeshi la Polisi na ninyi Wabunge ni mashahidi mara nyingi mmekuwa mkihoji, vituo vyangu havina magari, Jimbo langu kwenye kituo fulani hakuna magari, na ndiyo kwa kuzingatia hilo Serikali kupitia Jeshi la Polisi, likaandaa mkakati kabambe wa kupunguza hiyo hali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kulimaliza kwa wakati mmoja, siyo rahisi kwa sababu katika nchi tuna zaidi ya vituo 4,500, kwa hiyo, kupata gari 4,500 kwa mpigo ili kila kituo kiweze kupata gari ni jambo ambalo ni gumu. Kwa hiyo kulikuwa kuna mpango wa kwanza wa kuweza kupata gari 777 kupitia mkopo wa Exim Bank ya India, ambapo kati ya hizo tuliweza kupata gari 104, lakini pia Serikali iliweza kutoa gari takribani 203 kwa hiyo kufanya jumla ya idadi ya gari ambazo zilipatikana kuwa ni 387. Kati ya gari hizo, gari 37 zilipelekwa Zanzibar na nimhakikishie Mheshimiwa Hafidh Ali Tahir kwamba gari hizi bado hazijagawiwa katika Wilaya, nina hakika kwamba wakati mgao utakapokuwa umefanyika, basi Wilaya hizo ambazo zimezungumzwa vituo vya Wilaya yake ya Magharibi A na Magharibi B vitapata gari.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali lake la pili, alizungumzia kuhusiana na hali ya usalama kwa ujumla. Mimi nataka nimhakikishie tu kwamba pamoja niichukue fursa hii, kuwaeleza Wananchi wa Zanzibar kwamba Jeshi la Polisi ama Serikali itahakikisha inalinda usalama wa raia kama ambavyo majukumu yake ya msingi yanavyotaka. Kwa hiyo, wasiwe na wasiwasi wajitokeze kwa wingi kushiriki uchaguzi utakaporudiwa na hakuna wasiwasi wowote kila mtu ambaye atakuwa na haki ya kupiga kura, apige kura kwa usalama na amani. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. HAFIDH ALI TAHIR aliulliza:- Bunge la Jamhuri ya Muungano hupitisha Bajeti ya Serikali kwa kila Wizara kwa mwaka ikiwemo Wizara ya Mambo ya Ndani:- (a) Je, inakuwaje Wilaya yenye vituo saba vya polisi ina gari moja tu na inapatiwa lita tano hadi saba tu za mafuta kwa siku? (b) Je, Serikali iko tayari kuziongezea mafuta na magari Wilaya za Magharibi A na B zenye vituo vya polisi vya Fumba, Mbweni, Mazizini, Mwanakwerekwe, Kijitoupele, Fuoni, Airport na Mfenesini ambazo ni gari moja tu kila Wilaya ili kukongeza ufanisi na kuendana na kasi ya hapa kazi tu hasa ukizingatia kuwa Zanzibar inajiandaa na marudio ya Uchaguzi Mkuu?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, ninaomba niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa shida ya ulinzi iliyopo Dimani inafanana sana na Jimbo la Ukonga, nina Kata 13, sina kituo kikubwa cha Polisi, na ni eneo la pembezoni ikiwepo Msitu wa Kazimzumbwi, lakini hata kituo cha Sitakishari ambacho kinahudumia Jimbo la Segerea na Ukonga hakuna gari, sasa nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, atatujengea Kituo cha Polisi Ukonga au apeleke gari Segerea Sitakishari ili ihudumie wakati mipango mingine inaendelea?
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwasilishe, ahsanteni.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani ule umuhimu wa magari ambayo nimekuwa nikiuzungumza umeongezeka uzito wake, sasa niweke tu wazi kwamba katika yale magari ambayo tumeyapata, magari mengi ni kwa ajili ya doria, operation na matumizi ya kawaida ya polisi. Hayo magari yanayoitwa ya washawasha sidhani hata 24 sujui kama yanafika.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Waitara nadhani utakubaliana na mimi na Wabunge wengine kwamba, Jeshi la polisi linahitaji magari zaidi, ikiwemo katika Kituo chako ulichozungumza, mimi naomba hili nilichukue tuone tutalifanyia kazi vipi.

Name

Suleiman Masoud Nchambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. HAFIDH ALI TAHIR aliulliza:- Bunge la Jamhuri ya Muungano hupitisha Bajeti ya Serikali kwa kila Wizara kwa mwaka ikiwemo Wizara ya Mambo ya Ndani:- (a) Je, inakuwaje Wilaya yenye vituo saba vya polisi ina gari moja tu na inapatiwa lita tano hadi saba tu za mafuta kwa siku? (b) Je, Serikali iko tayari kuziongezea mafuta na magari Wilaya za Magharibi A na B zenye vituo vya polisi vya Fumba, Mbweni, Mazizini, Mwanakwerekwe, Kijitoupele, Fuoni, Airport na Mfenesini ambazo ni gari moja tu kila Wilaya ili kukongeza ufanisi na kuendana na kasi ya hapa kazi tu hasa ukizingatia kuwa Zanzibar inajiandaa na marudio ya Uchaguzi Mkuu?

Supplementary Question 3

MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, wabheja sana. Kwa kuwa Jimbo la Kishapu halikupata mgao wa magari mapya ya polisi katika awamu hii na Jimbo hili lenye watu sharp na askari wanaofanya kazi zao kwa u-sharp, lina magari mawili mabovu yenye umri wa zaidi ya miaka mitano.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, nilipata ahadi kuwa mwezi wa pili tutapata magari mapya ya polisi, uko tayari kunihakikishia Jimbo sharp litapata magari mapya ili Wananchi waweze kupata huduma hasa za kiusalama wanapohitaji kuliko hivi sasa polisi wangu wa Kishapu wanavyohangaika? Wabheja

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Nchambi kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano ya hapa kazi tu huwa haina desturi za kutoa ahadi ambazo hazitekelezeki. Kwa hiyo, kama ni ahadi ambayo imetolewa, basi nitaifuatilia hiyo ahadi yenyewe halafu tuone hatua zilizofikiwa zimefikiwaje na kama imekwama imekwama vipi, halafu tutaonana mimi na yeye tuone ni jinsi gani ya kufanya.