Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N HASUNGA aliuliza:- Kwa kuwa watumishi na viongozi wengi wamekuwa wanaingia kwenye madaraka mbalimbali ya nchi bila kupewa mafunzo ya kuwaandaa kama ilivyo katika nchi nyingi duniani na kama ilivyo kwenye vyombo vya majeshi yetu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa viongozi wote wanapewa mafunzo ya awali kabla ya uteuzi wa madaraka yoyote katika utumishi wa umma?

Supplementary Question 1

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2007/2008 Serikali kupitia Ofisi ya Rais - Utumishi ilikipa Chuo cha Utumishi wa Umma kikishirikiana na chuo kimoja cha Macintosh cha Canada kuandaa framework ya kuwandaa viongozi ambayo ilijulikana kama Leadership Competence Framework. Na katika framework hiyo ilikuja na sifa 24 yaani leadership competencies 24. Sasa, je, ni lini Serikali itakuwa tayari sasa kuziingiza hizo competencies katika mafunzo ambayo tayari yameandaliwa na Serikali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa katika utaratibu wa majeshi yetu kuna utaratibu kwamba mtu hawezi kupata cheo chochote mpaka kwanza apate mafunzo fulani. Sasa kwa kuwa Serikali imesema inaandaa utaratibu wa kozi ambazo zitakuwa ni lazima kwa watumishi wa umma waandamizi. Je, ni lini sasa tamko la Serikali hizo kozi zitaanza ili watumishi hawa wawe wanafundishwa na wanaandaliwa ili wawe mahiri kabla hawajapata uteuzi wa madaraka ya aina yoyote?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Hasunga, alikuwa ni mtumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma kwa hiyo, anaifahamu sekta hii vizuri sana na anakifahamu chuo vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na swali lake la kwanza kwamba ni lini sasa Serikali itakuwa tayari kuingiza zile sifa 24 za uongozi katika mafunzo yake; nisema tu kwamba sasa tunaandaa utaratibu katika hayo mafunzo ya lazima, utakapokamilika na zile sifa zote 24 katika leadership competence zitaweza kuingizwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili, ni lini sasa katika mafunzo ya in-service, kabla watu hawajapandishwa cheo yataweza kuwekewa utaratibu, nipende tu kusema kwamba pamoja na haya tumeandaa pia, utaratibu wa kuwa na assessment centre ambao tutaweza kuweka kuwa na pool ya watu mbalimbali ambao wana-managerial positions ambazo wakati wowote wanaweza wakateuliwa. Watakuwa tested, lakini pamoja na hayo pia, kutakuwa na yale mafunzo ya lazima ambayo niliyaeleza awali yatakapokamilika basi wataweza kupatiwa na tutakuwa hatuwezi kupandisha cheo mtu kabla hajapata mafunzo hayo.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. JAPHET N HASUNGA aliuliza:- Kwa kuwa watumishi na viongozi wengi wamekuwa wanaingia kwenye madaraka mbalimbali ya nchi bila kupewa mafunzo ya kuwaandaa kama ilivyo katika nchi nyingi duniani na kama ilivyo kwenye vyombo vya majeshi yetu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa viongozi wote wanapewa mafunzo ya awali kabla ya uteuzi wa madaraka yoyote katika utumishi wa umma?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana. Tatizo la viongozi kukosa semina elekezi juu ya masuala ya uongozi yamekuwa yakionekana kuanzia ngazi za juu, kwa mfano mdogo tu hapa katika swali lililopita unakuta Mawaziri wamejibu, Naibu Waziri naye anajibu kwa hiyo, protocol inakuwa inaonekana pale haijafuatwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, suala langu ninalotaka kujua ni kwamba taratibu kama hizi, viongozi ambao wanakosa semina za mafunzo elekezi na contradiction inaonekana ndani ya Bunge lako Tukufu…
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilitaka nijue makosa kama haya yataendelea mpaka lini kwa viongozi ambao hawana semina kama Mawaziri? Ahsante.

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na semina elekezi au mafunzo elekezi kabla watu hawajaingia katika madaraka nimeshaeleza awali.
Lakini pili, kwa mwaka huu wa fedha peke yake Taasisi ya Uongozi imetoa mafunzo kwa viongozi 544, lakini pia tumekuwa tukitoa mafunzo kwa Mawaziri, tumekuwa tukitoa mafunzo kwa Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri pamoja na nafasi nyinginezo na tutaendelea kufanya hivyo kila wakati itakapobidi.

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. JAPHET N HASUNGA aliuliza:- Kwa kuwa watumishi na viongozi wengi wamekuwa wanaingia kwenye madaraka mbalimbali ya nchi bila kupewa mafunzo ya kuwaandaa kama ilivyo katika nchi nyingi duniani na kama ilivyo kwenye vyombo vya majeshi yetu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa viongozi wote wanapewa mafunzo ya awali kabla ya uteuzi wa madaraka yoyote katika utumishi wa umma?

Supplementary Question 3

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya viongozi katika ngazi za Wilaya, hasa ma-DC na ma-DAS, wengi wao wamekuwa wababe na wamekuwa wakitumia madaraka yao kuwanyanyasa wananchi kwa kisingizio eti wao ni Marais wa Wilaya. Wakati nafahamu katika uchaguzi uliopita tumemchagua Rais mmoja tu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. (Makofi)
Je, Serikali haioni hili linaweza kuwa ni tatizo kubwa sana? Na inawezekana kama tutaendelea bila kufanya utafiti wa kutosha na kuwachunguza watu hawa wanaweza kuharibu hata imani ya wananchi kwa Chama cha Mapinduzi?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kama nilivyosema muda mfupi uliopita kwamba hawa ni binadamu na ni Watanzania wenzetu. Na kutokana na kazi na nature ya kazi wanazozifanya inawezekana mahali fulani kukatokea mikwaruzano, lakini tatizo la mtu mmoja haliwezi kuwa la watu wote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwahakikishie kwamba Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wanafanya kazi nzuri sana. Wanatusaidia maana wao ndio wasimamizi kwa niaba ya Serikali katika maeneo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa jana lilitokea swali ambalo lilikuwa linataka kufahamu kofia au nafasi ya Mkuu wa Mkoa. Mkuu wa Mkoa ana kofia mbili, ana kofia ambazo zinashuka kwa Rais zile mbele, Head of Executive and Head of State. The President is Head of State and at the same time Head of Executive. Wakuu wa Mikoa wanashukiwa na zile kofia mbili na ndio maana wanalindwa na bunduki kati ya saba mpaka kumi na moja na askari saba hadi kumi na moja. Na ni haki yao wao kulindwa kwa sababu wanafanya maamuzi mazito, wanaweza wakaingilia jambo ambalo haliendi sawa kwa sababu ndio wawakilishi wa Serikali katika maeneo yao. Na kwa hiyo lazima vyombo vya ulinzi na usalama viwalinde kwa sababu ya nature ya kazi zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nichukue nafasi hii kuwaomba sana Waheshimiwa Wabunge ni suala la mawasiliano, sio na ninyi tena kutunishiana ubabe kule. Kinachowezekana kutokea kule sasa ikiwa hivyo itaonekana nani ni nani. Lakini kama tukiletewa, inapotokea upungufu tunaweza tukashughulikia administratively tu na jambo likaenda vizuri, kama nilivyosema hawa nao ni binadamu. Kwa hiyo, pale ambapo tunapata fursa tumekuwa tukitoa maelekezo kwao na tumekuwa tukitoa hata kwa maelekezo ya maandishi na wala semina sio jambo la msingi sana. Lakini kubwa hapa ni maelekezo na mtu kujua wajibu wake.