Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Barabara ya Mbeya – Chunya - Makongorosi imejengwa kwa kiwango cha lami kwa asilimia 80. Je, ni lini Serikali itaweka mizani katika barabara hiyo ya lami ili kuilinda iweze kudumu muda mrefu?

Supplementary Question 1

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Napenda kumshukuru sana Naibu Waziri amejibu vizuri sana na amejibu kitaalamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imesema Chunya ina mazao mengi ambayo yakibebwa ndiyo yanaharibu barabara, sasa napenda nimwambie Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba wanaosomba tumbaku, magari yanayobeba tumbaku au mbao au mkaa yanabeba lumbesa, yanakuwa mara mbili, yakifika Mbeya yanagawa kwa sababu kuna mizani kule ndiyo yawe magari mawili na Serikali hapa imesema kwamba itadhibiti hiyo kwa kuweka mobile weighbridges.
Je, ni lini itaweka kwa sababu Chunya sasa hivi sijaiona mobile weighbridge hata moja? Hilo ni swali la kwanza
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili nashukuru Serikali imesema kwamba ujenzi wa barabara hiyo kuanzia Chunya kwenda Makongorosi karibu utaanza, napenda nimwambie Naibu Waziri kwamba Mheshimiwa Rais akiwa Makongorosi aliwaahidi wananchi wa Makongorosi kwamba atawapa kilomita nne za lami pale Makongorosi na kwamba barabara hiyo ya Chunya Makongorosi itaanza kujengwa Makongorosi kuja Chunya.
Je, hiyo barabara itanza lini kujengwa? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama tulivyosema kwenye jibu la msingi la swali la msingi kwamba weighbridge itaanza hivi karibuni. Naomba kuchukua nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Mwambalaswa kama yeye alivyo-concerned na uharibifu wa barabara hiyo na sisi ambao ndiyo wenye dhamana hiyo tuko concerned kwa kiwango kikubwa, ninamhakikishia hiyo weighbridge inatafutwa hivi karibuni itaanza kufanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili naomba kumjulisha Mheshimiwa Mwambalaswa kwamba mara fedha zitakapopatikana barabara hii itaanza kujengwa na suala la ianzie wapi whether ianzie Makongorosi au ianzie Chunya nadhani ni muhimu tuwaachie wataalamu na ahadi ya kilomita Nne nayo katika eneo la Makongorosi itaangaliwa kwa umakini wake. (Makofi)