Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Katika kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2010 Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga kwa changarawe barabara ya Kibiti – Nyamisati. (a) Je, ni sababu zipi zilizochelewesha kukamilika kwa ahadi hiyo? (b) Je, ni lini sasa ahadi hiyo itatekelezwa?

Supplementary Question 1

Pwani. MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nianze kusema mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Waziri huyu ni mchapakazi, kweli tarehe 5 Januari, ni Waziri wa kwanza aliyefika maeneo ya Delta na nilifanya naye kazi na nikaonesha kweli kauli ya hapa kazi inatekelezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niulize maswali yangu mawili; moja, je, kutokana na barabara hii kwamba kwa sasa ina maeneo mawili ya daraja hayapitiki, je, Serikali haioni kwamba ina kila sababu ya kukarabati madaraja hayo? Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; Barabara ya kutoka Muhoro kwenda Mbwela ina matatizo makubwa hasa kwenye Daraja la Mbuchi, je, Serikali itatusaidiaje katika hilo la Mbuchi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kupokea shukrani zake ndugu yangu Mheshimiwa Ungando, naomba nikiri, kweli nilikuwepo kule na tulitembelea visiwa 40 vya Deltakatika Jimbo lile la Kibiti. Barabara ya kutoka hapa Bunju mpaka Nyamisati kule ndani kwa kweli ina changamoto kubwa sana naomba tulipokee jambo hili kwa sababu katika programu yetu ya uondoaji wa vikwazo tutajitahidi ofisi yetu tufanye kila liwezekanalo kwa sababu tukiwasaidia wananchi wa eneo lile tutakuwa hata tumewasaidia wananchi wa Mafia kwa sababu wanaposafiri kutoka Nyamisati kwenda Mafia lazima watumie barabara ile. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika suala zima la Daraja la Mbuchi, na kwa sababu tulipita kule na vilevile tunajua kuwa tuna harakati ofisi yetu kutengeneza Daraja la Mbwela, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo kuhakikisha mambo haya yote ofisi yetu inayashughulikia na Mheshimiwa Ungando amini Serikali yako tutakupa ushirikiano kwa sababu jimbo lako ni miongoni mwa majimbo yenye changamoto kubwa.

Name

Saumu Heri Sakala

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Katika kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2010 Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga kwa changarawe barabara ya Kibiti – Nyamisati. (a) Je, ni sababu zipi zilizochelewesha kukamilika kwa ahadi hiyo? (b) Je, ni lini sasa ahadi hiyo itatekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii. Barabara ya Tanga - Pangani - Bagamoyo ni barabara ambayo imekuwa ikitolewa ahadi kila chaguzi kuu zinapofika na Uchaguzi Mkuu uliopita pia ahadi hiyo ilitolewa ya kwamba itaanza kutengenezwa na tayari tunaambiwa upembuzi yakinifu umekwishafanyika, sasa je, ni lini utengenezaji wa barabara hiyo utaanza ikiwa tayari upembuzi yakinifu umekwishafanyika? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara hii nimepita mara kadhaa na juzijuzi nilivyokuwa natembelea Mkoa wa Tanga, ni miongoni mwa barabara niliyoipita kutoka Bagamoyo mpaka pale Pangani na kikubwa zaidi katika kufika pale nilikuta reference ya Waziri wa Miundombinu aliyekuwa akipita pale na kutoa ahadi hiyo ya ujenzi wa barabara hiyo lakini ikiwa sambamba na ujenzi wa daraja lile la pale Pangani. Mheshimiwa Mawenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu ni commitment ya Serikali na kipindi cha sasa kwa sababu ujenzi wa barabara ya lami lazima kwanza upembuzi yakinifu ufanyike na jambo hilo limekamilika, ninaamini suala la barabara hii kwa sababu ni barabara ya kimkakati, kwamba hata kwenda Mombasa ni barabara ya shortcut naamini Serikali hii itafanya kila liwezekanalo ujenzi wa barabara hii uweze kukamilika.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Katika kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2010 Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga kwa changarawe barabara ya Kibiti – Nyamisati. (a) Je, ni sababu zipi zilizochelewesha kukamilika kwa ahadi hiyo? (b) Je, ni lini sasa ahadi hiyo itatekelezwa?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la dogo nyongeza. Barabara ya kutoka Mkuranga Mjini mpaka Kisiju Pwani ni miongoni mwa barabara ambayo zimekuwa zikiahidiwa pia kuwekwa lami na Awamu ya Nne na hata Awamu hii ya Tano. Barabara hii inapita katika Makao Makuu ya Wilaya yetu ya Mkuranga lakini pia inapita katika Hospitali yetu Kuu ya Wilaya ya Mkuranga. Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini sasa Serikali itatusaidia kuhakikisha barabara hii inawekwa lami kutoka Mkuranga Mjini kupita Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Hospitali ya Wilaya mpaka Kisiju Pwani?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niweke kumbukumbu sawa, kwanza Mheshimiwa Ulega juzi kwa uchapakazi wake mzuri juzi alikuja ofisini kwetu kwa ajili ya kuhakikisha suala zima la miundombinu ya barabara katika jimbo lake na hii ni miongoni mwa barabara ambayo tulikuwa tukiijadili na Katibu Mkuu wangu pale jinsi gani tutafanya, kwa sababu yale ni Makao Makuu ya Halmashauri na kila Makao Makuu ya Halmashauri lazima angalau barabara ya lami iweze kufikika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali tutaangalia jinsi gani tutafanya lakini nikijua wazi barabara ile ambayo inaenda mpaka Kisiju Pwani ni jambo la mkakati mkubwa sana na kuna barabara nyingine kutoka Kimanzichana inapita katikati kule mpaka inakuja maeneo ya Msanga katika Jimbo la Kisarawe, hizi zote ni barabara za kimkakati kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Mkoa wa Pwani unafunguka, lengo kubwa ni kwamba katika uchumi unaofunguka wa viwanda sasa wananchi waweze kushiriki vizuri katika mchakato wa viwanda. Kwa hiyo, Mheshimiwa Ulega naomba nikuahidi tutakupa ushirikiano wa kutosha kujenga miundombinu yetu ya barabara za lami katika maeneo yetu.