Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA NASSIR ALI (K.n.y MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA) aliuliza:- Zanzibar kumekuwa na matukio ya uhalifu yanayojitokeza mara kwa mara. Je, Serikali ina mpango gani wa kuzuia vitendo vya uhalifu visijitokeze Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na nina swali moja la nyongeza. Kwa vile hali ya kiusalama sasa Zanzibar ni shwari na naomba niendelee kuipongeza Serikali kwa hilo, je, Serikali ina mpango gani wa kuzidi kuimarisha hali hiyo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunashukuru Mheshimiwa Khadija Nassir kwa kuona jitihada na mafanikio makubwa ya hali ya kuimarisha usalama sio tu kwa Zanzibar lakini Tanzania nzima na tunaomba Waheshimiwa Wabunge na wananchi kwa ujumla waendelee kutoa ushirikiano wao kwa vyombo vya ulinzi na usalama ili hali hiyo iweze kudumu. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wetu kama ambavyo nimejibu kwenye swali la msingi tutaendelea kuhakikisha kwamba hali hii inadumu kwa kuhakikisha kwamba tunaimarisha vitendea kazi na uwezo kwa maana ya uwezo wa kiutendaji wa vyombo hivi vya ulinzi tukitarajia kabisa ushirikiano kati ya wananchi na vyombo hivyo utaongezeka ili kuweza kupata taarifa za kiintelejensia kabla ya kuanza kufanya kazi za kuweza kuwakamata wahalifu ambao wamekuwa wakisumbua Taifa letu kwa kiwango fulani katika nchi yetu.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. KHADIJA NASSIR ALI (K.n.y MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA) aliuliza:- Zanzibar kumekuwa na matukio ya uhalifu yanayojitokeza mara kwa mara. Je, Serikali ina mpango gani wa kuzuia vitendo vya uhalifu visijitokeze Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa vitendo hivi vya uhalifu vipo nchi nzima na kule Jimboni Mlalo mwezi wa nane/tisa vikundi vya ugaidi vimeua watu wawili na kuchoma mabweni ya Chuo Kikuu cha SEKOMU. Je, ni lini Serikali itaimarisha ulinzi katika maeneo ya Jimbo la Lushoto ikiwa ni pamoja na kujenga seliya kuwekea silaha katika Kituo cha Mlalo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuna kazi kubwa imefanyika ya kuweza kupambana na ujambazi katika maeneo mbalimbali ikiwemo Mkoa wa Tanga. Kimsingi nchi yetu haina ugaidi, tunasema tunavimelea vya ugaidi. Kwa hiyo, kilichofanyika Tanga na ninyi ni mashahidi katika maeneo ya Amboni na kwingineko ni kazi kubwa sana ambayo imefanyika kwa mafanikio makubwa na hakika kwamba mafanikio yale ndiyo ambayo yamesababisha mpaka sasa hivi Mkoa wa Tanga kwa ujumla wake ikiwemo Lushoto kuendelea kuwa katika hali ya usalama. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa suala la uhalifu ni suala ambalo linaendelea kuwepo, tutaendelea kuhakikisha kwamba tunaimarisha kazi hiyo ifanyike zaidi na zaidi ili kutokomeza kabisa uhalifu katika maeneo ambayo yamesalia katika nchi yetu.

Name

Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA NASSIR ALI (K.n.y MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA) aliuliza:- Zanzibar kumekuwa na matukio ya uhalifu yanayojitokeza mara kwa mara. Je, Serikali ina mpango gani wa kuzuia vitendo vya uhalifu visijitokeze Zanzibar?

Supplementary Question 3

MHE. SALMA M. MWASA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Kumekuwa na utaratibu wa vituo vya polisi vidogo (police post) hasa kwa Mkoa wa Dar es Salaam kufungwa saa kumi na mbili hii inasababisha matukio mengi ya uhalifu hasa yanatokea usiku. Je, Serikali haioni inahatarisha usalama wa wananchi hasa Mkoa wa Dar es Salaam wenye wakazi zaidi ya milioni tano?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa PGO kuna vituo vya polisi vya aina tatu; kuna Class A, Class B na Class C. Kwa hiyo, vituo vya Class C kwa kawaida havifunguliwi zaidi ya saa 12. Sasa sina hakika Mheshimiwa Mbunge kituo ambacho anakizungumzia ni kituo kiko katika class gani labda pengine baada ya hapo tuone kama kitakuwa kipo katika nje ya class ambayo inapaswa kifungwe zaidi ya hapo na kinafungwa basi tutachukua hatua tuone nini kinafanyika tufanye uchunguzi tujue tatizo ni nini. Lakini nadhani kulijibu moja kwa moja swali lako kwasababu hajaainisha kituo chenyewe ni kituo gani kwa wakati huu itakuwa ni vigumu.