Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Savelina Slivanus Mwijage

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE Aliuliza:- Nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ni za muda mrefu na zimekuwa chakavu sana na nyingine zimeanza kubomoka. (a) Je, ni lini Serikali itafanya operesheni kubaini uharibifu ulioko kwenye nyumba hizo? (b) Je, ni lini Serikali itatenga bajeti kwa ajili ya kukarabati au kujenga upya nyumba hizo?

Supplementary Question 1

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa nyumba nyingi zimefanyiwa ukarabati kama alivyosema Naibu Waziri, Bukoba Mjini kuna majumba ya NHC yaliyochakaa yanaonesha Mji kuchafuka kwa ajili ya nyumba hizo za NHC.
Je, ni lini Serikali itafanyia ukarabati au kujenga
majengo mapya ya NHC?
Swali la pili, kuna majengo ambayo yamechakaa yako kwenye mtaa wa Miembeni watu wameishi muda mrefu hayana miundombinu hayana sehemu za kuingilia watu wenyewe waliopanga mle ndio wanajiwekea miundombinu na Serikali inakusanya ushuru na inakusanya kodi za majengo.
Je, ni lini Serikali itajenga nyumba mpya au
kuwaruhusu wale waliomo ndani kuzinunua?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mwijage amezungumzia suala la ukarabati wa nyumba za Bukoba zilizo chakavu. Kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi nimesema suala la ukarabati ni suala endelevu na pale ambapo nyumba zinaonekana zimechakaa haziwezi tena kufanyiwa ukarabati, shirika linabomoa nyumba zile na kujenga majengo mengine mapya.
Kwa hiyo, niseme kwamba kama nyumba za Bukoba anavyosema kwamba zimechakaa, zinahitaji ukarabati nadhani bado tutaangalia kwa sababu Meneja yupo pale anaziona na anajua na ndiyo maana nimesema ukarabati huu unaendelea nchi nzima, kwa hiyo na Bukoba pia ni moja ya eneo ambalo litaangaliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili eneo la Miembeni nyumba zilizoko ni chakavu na hazina miundombinu. Kama nilivyosema jibu la msingi kama ni chakavu na haziwezi kufanyiwa ukarabati nadhani jukumu lililopo ni kubomoa na kujenga nyumba nyingine mpya na watu wakakaa katika mazingira yaliyo mazuri. Hatakubali kuendelea kuwa na nyumba ambazo ni chakavu na hazina
uwezekano wa kufanyiwa repear. Kwa hiyo, ni jukumu la Shirika la Nyumba tutawatuma waende waangalie hizo ambazo hazina miundombinu na haziwezi kukarabatika tena tuone utaratibu wa kuweza kuzijenga upya katika hali hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, umilikishaji kwa wananchi ni kwamba sasa hivi kuna ule utaratibu wa mpangaji mnunuzi, kwa hiyo, kuna maeneo ambayo kuna hizo nyumba ambazo zinajengwa bado mpangaji anaweza kuwa mnunuzi kwa hiyo mtu atamilikishwa nyumba pale atakapokuwa amelipia nyumba yake na amefikia mwisho wa gharama ya nyumba husika.

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE Aliuliza:- Nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ni za muda mrefu na zimekuwa chakavu sana na nyingine zimeanza kubomoka. (a) Je, ni lini Serikali itafanya operesheni kubaini uharibifu ulioko kwenye nyumba hizo? (b) Je, ni lini Serikali itatenga bajeti kwa ajili ya kukarabati au kujenga upya nyumba hizo?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu wa Serikali wa kuhamisha nyumba zilizokuwa chini ya Halmashauri kwenda Serikali Kuu umeacha watumishi katika Halmashauri ya Karagwe bila makazi, takribani kaya za Watumishi 60 hivi sasa hazina makazi kwa sababu Serikali Kuu imechukua nyumba ambazo zilikuwa chini ya Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe.
Je, Wizara haioni kwamba inabidi iwasaidie watumishi hawa kwa kuiomba NHC ishirikiane na
Halmashauri, Halmashauri tunaweza tukawapa eneo la kujenga nyumba nafuu kwa ajili ya watumishi hawa? Nashukuru

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba nyumba zilizokuwa awali za Wizara ya TAMISEMI baadae zikaenda NHC sasa zimerudishwa Serikali Kuu. Hivi sasa wataalam wangu na Wataalam wa Wizara ya Ujenzi wanapima maeneo hayo ili yamilikishwe kwa Serikali Kuu. Lengo la Serikali ni kujenga nyumba mpya ili ziweze kuboresha mandhari ya Miji, kwa sababu nyumba hizi tangu zimemilikiwa na Serikali za Mitaa na NHC ingawa maeneo yale ni mijini lakini nyumba zimekuwa chakavu na hivyo
zinaleta mandhari mbaya katika miji. Hivyo, lengo la Serikali ni kuzijenga upya.
Pili, kuchukua zile nyumba kuziweka Serikali Kuu hakumaanishi kwamba wale wanaokaa katika nyumba zile sasa wafukuzwe. Mheshimiwa Rais ameagiza kwamba zoezi hili linakoendelea kupima mpaka itakapofikia zamu ya kujenga nyumba mpya katika maeneo hayo, waliomo wanaopanga sasa wabaki katika nyumba hizo wasibughudhiwe na wasifukuzwe. Whether ni watumishi wa leo au watumishi wa zamani wenye mikataba ya kukaa kwenye nyumba hizo wabaki wale wale.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, wale wa Karagwe hao hawapaswi kutoka, wakae humo humo whether ni watumishi au wananchi wa kawaida. Nyumba hizi ingawa si lazima wakae watumishi tu lakini kuna sehemu nyingine watumishi wa Serikali wanakaa na wananchi wa kawaida. Kwa hiyo, waliomo kwenye nyumba hizo wasifukuzwe. Huko Karagwe kama wananisikia wanafikiri kwamba hao wafanyakazi wanatakiwa kufukuzwa hapana. Tunahaulisha tu utaratibu wa umiliki wa Serikali lakini hatuwaondoi wapangaji.

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE Aliuliza:- Nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ni za muda mrefu na zimekuwa chakavu sana na nyingine zimeanza kubomoka. (a) Je, ni lini Serikali itafanya operesheni kubaini uharibifu ulioko kwenye nyumba hizo? (b) Je, ni lini Serikali itatenga bajeti kwa ajili ya kukarabati au kujenga upya nyumba hizo?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona na mimi niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa lengo la kuboresha nyumba hizi za National Housing ni kuwaondolea bugudha wapangaji wanaoishi katika nyumba hizo; sasa pale kwenye nyumba zilizoko Keko Juu, Kata ya Keko njia panda ya kwenda Uwanja wa Taifa wapangaji katika nyumba nne kati ya nyumba Nane zilizokuwa pale waliwahi kupewa notice ya kutaka kuhama bila sababu za msingi na wapangaji wakaamua kwenda mahakamani. Mpaka tunapozungumza sasa kesi hiyo ipo mahakamani. Mahakama imesema kwamba wakati kesi bado inaendelea pande zile mbili kati ya National Housing na wapangaji sizibughudhiane, lakini mara kwa mara...
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja kwenye swali. Kinachoendela sasa kila baada ya muda mfupi National Housing wanawatuma madalali kupeleka notice kwa wapangaji wale. Kwa kuwa, kesi ipo Mahakamani na kuwapelekea notice ni kuwabughudhi wapangaji wale na kuingilia Mahakama, Mheshimiwa Waziri anaweza kutoa kauli hapa leo ya kuwaambia National Housing waache kuwabughudhi wapangaji wale mpaka kesi itakapoisha?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba Wizara kama Wizara haiwezi kutoa kauli hapa kwa maamuzi ambayo yako nje ya muhimili wa Bunge. Maamuzi ya Mahakama yatabaki kama yalivyo na kwa maana hiyo yale yaliyoagizwa na Mahakama ndiyo yatakayoendelea kuheshimiwa mpaka hapo uamuzi sahihi utakapokuwa umetoka.

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE Aliuliza:- Nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ni za muda mrefu na zimekuwa chakavu sana na nyingine zimeanza kubomoka. (a) Je, ni lini Serikali itafanya operesheni kubaini uharibifu ulioko kwenye nyumba hizo? (b) Je, ni lini Serikali itatenga bajeti kwa ajili ya kukarabati au kujenga upya nyumba hizo?

Supplementary Question 4

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa imeshatenga eneo ambalo Shirika la Nyumba la Taifa wanatakiwa kujenga nyumba, sasa ni miaka miwili.
Je, Shirika la Nyumba bado lina mpango wa kujenga nyumba kwenye Mji wa Maswa au mpango huu umesitishwa?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, National Housing bado inayo dhamira ya dhati ya kujenga nyumba katika maeneo yetu kwa nchi mzima na hasa pale Halmashauri zenyewe zinapokuwa ziko tayari zimetenga maeneo kwa ajili ya kazi hiyo. Kwa eneo na Maswa bahati nzuri nilifika na nafahamu eneo lilipo bado dhamira ya Shirika iko pale pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo kubwa ambalo
linatakiwa kufanyika kwa sababu mara nyingi pia tumekuwa tukilalamika kuwa bei ya nyumba kuwa kubwa, sasa Halmashauri ambazo zina maeneo kama Maswa wanatakiwa kuwa wamefanya maandalizi ya miundombinu katika maeneo yao, ikiwepo suala la barabara, suala la maji na suala la umeme ili watakapo kuja kujenga zile nyumba basi ziwe na gharama nafuu kama ambavyo inatarajiwa kuwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo napenda
kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba dhamira ya shirika bado ipo pale pale kujenga nyumba kwa kihakikisha Watanzania wanakuwa na makazi bora.