Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE.DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Je, ni lini Kata ya Mamba, Majimoto, Chamalema na Mwamapuli zitapatiwa maji safi na salama?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pia nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nasikitika kwamba, pesa hizi ni za bajeti ambayo tunakwenda kumalizia, naomba nijue ni lini pesa hizi zitatoka ziende zikafanye kazi hiyo kwa wananchi?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali langu la pili, kwa uzoefu unavyojionesha pesa hizi zinaweza zikatoka mwisho wa bajeti yaani Juni 30. Je, pesa hizi zinapotoka zinakwenda wapi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, pesa hizi ni za bajeti ya mwaka huu 2015/2016, lakini kama nilivyojibu awali, miradi mingi sana ya maji katika kipindi hiki toka tunapotoka katika mwaka wa uchaguzi mpaka hivi sasa, ni miradi mingi sana siyo katika Jimbo la Kavuu peke yake, isipokuwa miradi mingi sana imekuwa ikisuasua kutokana na upelekaji wa fedha. Hata hivyo Serikali imefanya juhudi kubwa sana mara baada ya kukusanya mapato makubwa Serikalini kuhakikisha kwamba maeneo mbalimbali ambayo miradi ilikuwa imesimama sasa ianze kufanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri kwamba Wizara ya Maji kwa kupitia Wizara ya Fedha, maeneo mbalimbali ambayo miradi mingine ilikwama sasa hivi imeshaanza kufanya kazi. Imani yangu kubwa iliyoko ni kwamba Ndugu yangu Mbunge ambaye najua siku zote ulikuwa ukipambana Jimboni kwako katika maeneo haya, kwa kipindi hiki tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo, Serikali iweze kupeleka maeneo yote ambayo miradi ilisimama ilimradi, miradi ikamilike katika mwaka huu wa fedha,
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, hata katika ripoti za Mkaguzi wa Serikali kuna miradi mingine inakwama kwa sababu fedha zinafika mwishoni. Kwa hiyo, niwaombe hasa ma-engineer wetu kule site kwamba, wajipange vizuri kiasi kwamba pesa hii itakapofika wahakikishe usimamizi unakwenda kwa haraka ilimradi wananchi wa Jimbo la Kavuu waweze kupata huduma za maji katika maeneo yao.

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE.DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Je, ni lini Kata ya Mamba, Majimoto, Chamalema na Mwamapuli zitapatiwa maji safi na salama?

Supplementary Question 2

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa hapa Bungeni tumekuwa tukipitisha fedha nyingi sana kwa ajili ya kwenda kutatua matatizo ya maji kule vijijini ikiwemo Mkoa wa Singida, lakini yamekuwa ni mazoea kwamba ma-engineer wanakwenda kuchimba maji maeneo ambapo hakuna maji ya kutosha na hivyo fedha nyingi kupotea.
Je, Serikali ni lini itakuja kutuletea idadi ya fedha ambazo zimepotezwa kwa sababu ya ma-engineer kwenda kuchimba maji kwenye maeneo ambayo hakuna maji matokeo yake wananchi wanaendelea kuteseka na adha za maji? Ni lini Serikali itatuletea figures hizo? Asante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la maji chini ya ardhi ni gumu sana na tuchukulie mfano Mkoa wa Tabora. Mkoa wa Tabora ulifanyiwa study na Wajapani na waka-confirm kwamba chini kuna maji, lakini wamekwenda kuchimba maji yamekosekana kutokana na mfumo wenyewe wa miamba chini ya ardhi. Kwa sasa Wizara ya Maji imetengeneza utaratibu mpya kwamba, study ya maji pamoja na uchimbaji utafanywa na mtu mmoja. Kitu tulichokiona ni kwamba, study inafanywa na Mhandisi Mshauri, anayekuja kuchimba ni mwingine na unakuta tunapoteza pesa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kitu tulichokifanya sasa hivi kwamba, pale tutakapotoa fedha kwa ajili ya kuchimba visima tunatafuta Mkandarasi mmoja na huyo huyo ndiyo anafanya study. Ili akifanya study akichimba kama maji hayakupatikana basi pesa hatutamlipa na kuhakikisha kwamba huo upotevu wa pesa unakuwa haupatikani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye hoja ya pili, tutafanya tafiti na tutatoa taarifa kwenye Bunge hili kuona ni fedha kiasi gani ambazo zimepotea baada ya huo utaratibu wa kuchimba visima na maji hayapatikani.