Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kemirembe Rose Julius Lwota

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ni miongoni mwa Halmashauri mpya zilizoanzishwa mwaka 2015 na watumishi 98 walihamishiwa kutoka Halmashauri za Sengerema, Misungwi, Ilemela, Jiji la Mwanza, Kwimba na Magu lakini watumishi hawa hadi sasa hawajalipwa fedha za uhamisho:- Je, ni lini Serikali itawalipa stahiki zao watumishi hawa?

Supplementary Question 1

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ila nina swali dogo moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuliona hili na siku ya Mei Mosi ametoa tamko watumishi wote watakaohamishwa vituo vyao walipwe fedha zao kabla ya uhamisho. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna baadhi ya watumishi wengi tu ambao wamehamishwa kwenye vituo vyao vya kazi, wameenda kwingine na hawajalipwa fedha zao za uhamisho mpaka leo. Kuna baadhi ya taasisi hata waliohamishiwa hapa Dodoma Makao Makuu hawajalipwa fedha zao mpaka leo.
Sasa ni lini Serikali italipa fedha za watumishi hawa waliohamishwa na hawajalipwa fedha zao za uhamisho? Nashukuru.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa concern ya Mheshimiwa Mbunge na siku zote maswali yake yamekuwa yakigusa wananchi wake na hasa watumishi, nakupongeza sana Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ofisi yetu ilifanya zoezi la uhakiki wa madeni kwa sababu tuna Halmashauri mpya nyingi sana zimeanzishwa. Kwa mfano, siku nilivyofika pale Busega au kwa mtani wangu Tabora Vijijini kwenye Halmashauri mpya ya Isikizya, nimekutana na watumishi wakilalamikia suala hili la madeni. Ndiyo maana ofisi yetu tukafanya uhakiki wa madeni na tumeyawasilisha Hazina.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tunazunguka maeneo mbalimbali tumekuta baadhi ya Halmashauri tayari madeni haya yameshaanza kulipwa. Kwa hiyo, kwa sababu uhakiki ulishafanyika na taarifa iko Hazina tufanye subira na wengine wameshaanza kulipwa na madeni yao yote yatalipwa kwa sababu Serikali haitaki kuona haki za watu zinadhulumiwa.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Naibu Waziri Mheshimiwa Selemani Jafo kwa majibu mazuri, lakini pia Mheshimiwa Kemilembe kwa swali zuri ambalo kusema ukweli linawagusa watumishi wengi na hasa wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tabia za Wakurugenzi wa Halmashauri kuwahamisha na hasa walimu kwa kuwakopa gharama ambazo wangepaswa kuwalipa kwa ajili ya usumbufu na gharama za uhamisho.
Nilisema hapa Bungeni hadi tarehe 30/04/2017 wanapaswa kuwa wamewalipa walimu waliowahamisha. Hili nililisema si kwa madeni ya nyuma sana ya uhamisho maana yale yote tulishayapeleka Wizara ya Fedha kwa ajili ya kulipwa, lakini kuna uhamisho uliofanyika kati ya mwezi Januari hadi Machi wa kupanga ikama za walimu. Deadline imefika na kuanzia sasa Wizara yangu itachukua hatua kwa wale wote ambao hawajawalipa walimu waliowahamisha. Haiwezekani Serikali tunapambana kupunguza madeni lakini wako watu wengine ni viwanda vya kuzalisha madeni yasiyokuwa na sababu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kusema ukweli suala hili tumelitilia msisitizo mkubwa lakini pia Serikali ipo katika mchakato wa kuandaa fedha kwa ajili ya kupanga hizi ikama kwa nchi nzima kwa Halmashauri zote. Zoezi hili litaenda sambamba na malipo ya moja kwa moja kwa watumishi watakaohamishwa kwa sababu ni haki yao ya msingi ya kiutumishi.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ni miongoni mwa Halmashauri mpya zilizoanzishwa mwaka 2015 na watumishi 98 walihamishiwa kutoka Halmashauri za Sengerema, Misungwi, Ilemela, Jiji la Mwanza, Kwimba na Magu lakini watumishi hawa hadi sasa hawajalipwa fedha za uhamisho:- Je, ni lini Serikali itawalipa stahiki zao watumishi hawa?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo yaliyoko huko Buchosa yanafanana kabisa na matatizo yaliyoko Itigi katika Halmashauri mpya ya Itigi. Wakati Halmashauri hii inaanzishwa ilipata watumishi kutoka Halmashauri mama ya Manyoni ambayo hata nayo ilikuwa na watumishi wachache na hivi tunavyozungumza Halmashauri ya Itigi pia imekutana na janga hili la vyeti fake, kuna baadhi ya watumishi ambao wameondoka, je, Serikali iko tayari sasa itakapotoa ajira kutuletea watumishi wa kutosheleza katika Halmashauri mpya ya Itigi?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na naomba kujibu swali la Mheshimiwa Massare kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunatambua upo upungufu na kama ambavyo tumekuwa tukieleza humu ndani, mwaka kesho tunatarajia kuajiri zaidi ya watumishi wapya 52,436. Jana tu pia tayari Mheshimiwa Rais alishaagiza, tumetoa kibali cha watumishi wapya 15,000 kwa ajili ya kwenda kuziba pengo la watumishi ambao wamekutwa na vyeti vya kughushi, lakini vilevile kuweza kuziba ikama na tutaendelea kufanya hivyo kila mara itakapobidi.

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ni miongoni mwa Halmashauri mpya zilizoanzishwa mwaka 2015 na watumishi 98 walihamishiwa kutoka Halmashauri za Sengerema, Misungwi, Ilemela, Jiji la Mwanza, Kwimba na Magu lakini watumishi hawa hadi sasa hawajalipwa fedha za uhamisho:- Je, ni lini Serikali itawalipa stahiki zao watumishi hawa?

Supplementary Question 3

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ambayo yametolewa kuhusiana na suala la kuhamisha watumishi katika Halmashauri zetu lakini suala hili limekuwa sugu sana. Ukiacha hao walimu ambao wamewazungumzia lakini wapo pia wauguzi, watendaji wa kata na vijiji. Mimi kama Mbunge au Diwani naweza kwenda kwa Mkurugenzi nikamuambia Mtendaji huyu simtaki mpeleke katika kijiji au kata nyingine bila kujali stahiki zake. Ni nini sasa kauli ya Serikali kuhusu watumishi hawa? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, alichosema Mheshimiwa Sikudhani ni kweli na hili sisi viongozi tunatakiwa tujitathmini kwamba wakati mwingine una interest zako binafsi unasababisha mtu fulani ahame kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine bila kujua kwamba unalimbikiza madeni katika maeneo hayo. Bahati mbaya sana wakati mwingine Mkurugenzi akikataa ndiyo unaanza bifu (kutokuelewana) naye kuanzia hapo kwamba Mkurugenzi huyu hatufai.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kwamba utaratibu wa kuhamisha kama alivyozungumza Waziri mwenye dhamana Mheshimiwa Boniface Simbachawene ni lazima uendane na bajeti iliyokuwepo. Vilevile si vyema kwa viongozi wowote kuwaweka katika mazingira magumu watumishi hawa na kuwa-frustrate kwa kuwahamisha bila sababu yoyote. Tunasema jambo hilo likome na lisiendelee katika Halmashauri zetu kwa sababu halileti afya kwa watumishi wetu ndani ya nchi yetu.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ni miongoni mwa Halmashauri mpya zilizoanzishwa mwaka 2015 na watumishi 98 walihamishiwa kutoka Halmashauri za Sengerema, Misungwi, Ilemela, Jiji la Mwanza, Kwimba na Magu lakini watumishi hawa hadi sasa hawajalipwa fedha za uhamisho:- Je, ni lini Serikali itawalipa stahiki zao watumishi hawa?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuweza kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri
ya Mawaziri na Naibu Waziri, kwa Wilaya ambazo ni mpya na Mheshimiwa Naibu Waziri amezungumzia suala la Busega kwamba alikuta pale matatizo ya watumishi, je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia Wilaya hizi mpya ambazo zimeanzishwa zenye uhaba wa ikama ya watumishi? Vilevile pili baadhi ya watumishi walio wengi hawajalipwa mafao yao. Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu pale awali ni kwamba tutajitahidi Halmashauri hizi mpya ambazo zimeanzishwa na bahati nzuri Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi) amezungumza wazi kwamba tuna hizi ajira mpya ambazo zinakuja lengo kubwa ni kuziba mapengo yote yaliyokuwepo katika maeneo yetu. Ofisi yetu imeshaanza kufanya tathmini ya kujua ni watumishi wangapi wanahitajika katika Halmashauri gani ili kuziba haya mapengo yaliyopo. Kwa hiyo, mtani wangu Mheshimiwa Dkt. Chegeni ondoa hofu zoezi hili litaweza kujibu matatizo ya watumishi katika Jimbo na Halmashauri yako ya Busega.

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ni miongoni mwa Halmashauri mpya zilizoanzishwa mwaka 2015 na watumishi 98 walihamishiwa kutoka Halmashauri za Sengerema, Misungwi, Ilemela, Jiji la Mwanza, Kwimba na Magu lakini watumishi hawa hadi sasa hawajalipwa fedha za uhamisho:- Je, ni lini Serikali itawalipa stahiki zao watumishi hawa?

Supplementary Question 5

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo tu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Kibaigwa unakua
kwa kasi sana na kwa sasa mji ule ni Mji Mdogo. Hata hivyo, kwa kuwa hatuna watumishi wa kutosha na mji ule haujafanywa kuwa mamlaka, naiomba Serikali sasa ituambie ni lini Mji wa Kibaigwa utapewa mamlaka ili waweze kupanga shughuli za mji wao na kupewa watumishi wa kutosha kuendeleza Mji ule Mdogo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, toka asubuhi nimesema leo kuna utaratibu wa kuhamisha goli katika uwanja. Naomba nikuambie Mheshimiwa Felister Bura kwamba hoja yako imesikika na lengo letu ni kupanga miji hii yetu yote vizuri, kuna Kibaigwa, Kibakwe na maeneo mengine katika Mkoa wako wa Dodoma najua inakua kwa kasi sana. Hata hivyo, wakati tunajielekeza katika mipango ya Mamlaka ya Miji Midogo tutajielekeza jinsi gani tupate watumishi kuweza kuziba nafasi hizo ili wananchi wetu wapate huduma vizuri. Nakushukuru sana.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesimama tena kwa sababu jambo hili limekuwa likiwagusa Waheshimiwa Wabunge wengi na katika maeneo mengi na hasa pale inapoanzishwa Mamlaka za Miji Midogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kiutaratibu mwenye dhamana ya kuendeleza miji hii kuweza kuanza kufanya shughuli zake inapokuwa imeanzishwa Miji hii Midogo ni Halmashauri Mama. Kwa hiyo, inapokuwa Serikali tumekubali kwamba mji huo uanze mipango yote na utaratibu wa uanzishwaji unaanzia kwenye Halmashauri Mama kuijengea uwezo Halmashauri hiyo ya Mji Mdogo ili iweze kufanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwasihi Waheshimiwa Wabunge kwamba mipango yote itapaswa iingie kwenye mipango ya Halmashauri Mama na ndipo sasa kwa yale maeneo ya upungufu wa watumishi Serikali inaweza kuwaleta. Hata hivyo, kama hakuna bajeti au mpango kutoka kwenye Halmashauri Mama sio rahisi kwa Halmashauri hizo za Miji Midogo kuweza kuanza.

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ni miongoni mwa Halmashauri mpya zilizoanzishwa mwaka 2015 na watumishi 98 walihamishiwa kutoka Halmashauri za Sengerema, Misungwi, Ilemela, Jiji la Mwanza, Kwimba na Magu lakini watumishi hawa hadi sasa hawajalipwa fedha za uhamisho:- Je, ni lini Serikali itawalipa stahiki zao watumishi hawa?

Supplementary Question 6

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwenye Jimbo langu la Serengeti katika process za kuongeza vijiji, vitongoji na kata, kuna baadhi ya maeneo ambayo utaratibu haukufuatwa, baada uchaguzi kuna Serikali za Vijiji walijiuzuru. Kwa hiyo, kimsingi kuna migogoro ya mipaka kati ya vijiji na vijiji na mpaka ninavyoongea hakuna uongozi kwenye vijiji hivyo. Nini tamko la Wizara kuhusu maeneo ambayo yana migogoro ya mipaka kati ya vijiji na vijiji?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba iko migogoro mbalimbali lakini migogoro inatofautiana, iko mipaka ya kijiji kwa kijiji, kata kwa kata, iko ya aina nyingi na kwenye orodha tumeorodhesha zaidi ya 250 kwa nchi nzima.
Nimuombe tu Mheshimiwa Mbunge kwa sababu mazingira ya migogoro hii inatofautiana kutoka mgogoro mmoja hadi mwingine hatuwezi kuwa na tamko la pamoja kwa hiyo atuletee ili tuweze kuona hiyo scenario ikoje ili tuweze kutatua mgogoro husika ikiwa ni pamoja na mamlaka za uongozi wa maeneo husika.