Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Wananchi wa wa Kibiti wanaishukuru Serikali kwa kupata Mji Mdogo Kibiti na kufanya uchaguzi wa Mwenyekiti na viongozi. (a) Je, kuna tatizo gani hadi leo Mamlaka ya Mji haijaanza kazi na kumpata Meya? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka Mkurugenzi wa Mji Mdogo?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kutokana
na vitendo vya uhalifu vinavyoendelea ambavyo vinasababisha Kibiti kushindwa kukusanya makusanyo yake ya ndani, je, Wizara itaiangaliaje kwa jicho la huruma ili kuhakikisha wanapata Mwenyekiti wao wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kibiti?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, kutokana
na ukweli kwamba Kibiti ni Halmashauri mpya Mkurugenzi na DC hawana vifaa vya kutendea kazi kama magari. Je, Serikali inaliangaliaje hilo kwa jicho la huruma?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nitoe pole kwa Mheshimiwa Mbunge na wananchi wote wa Kibiti na Rufiji kwa tatizo kubwa linaloendelea pale kwa sababu mpaka hivi sasa tumepoteza Wenyeviti wengi sana na hali hiyo inaogopesha.
Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko na wananchi wa Kibiti na Rufiji na tutaangalia nini cha kufanya kwa sababu sasa hivi ukiitisha uchaguzi pale hata Wenyekiti wenyewe kujitokeza kugombea nafasi yenyewe wanaogopa.
Kwa hiyo, Serikali inafanya kazi ya kurudisha hali ya utulivu na amani ili hali ya usalama iweze kukaa vizuri. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge amini kwamba Serikali yako itashirikiana na wewe kama inavyofanya hivi sasa ndiyo maana timu ya Mkoa wa Pwani iko kule site kuhakikisha mambo yanakaa sawa. Kwa hiyo, hili jambo tumelichukua kwa moyo wa dhati kabisa na tutashirikiana kupata ufumbuzi wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili la changamoto
ya magari, ni kweli na Mheshimiwa Ungando nikushukuru sana, tulipotembelea vile visiwa 40 vya delta kule tulifanya kazi kubwa sana, tokea asubuhi mpaka tulivyomaliza saa mbili usiku, nimebaini changamoto hizo. Ndiyo maana kipindi kile nilivyorudi haraka tukafanya utaratibu kuwaletea gari moja pale la Road Fund. Hata hivyo, Serikali imeona hili tatizo kwa DC na Mkurugenzi tutajitahidi nini tufanye kwa pamjoa kuisaidia Halmashauri hii mpya ambayo ina changamoto kubwa sana katika suala zima la vitendea kazi.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Wananchi wa wa Kibiti wanaishukuru Serikali kwa kupata Mji Mdogo Kibiti na kufanya uchaguzi wa Mwenyekiti na viongozi. (a) Je, kuna tatizo gani hadi leo Mamlaka ya Mji haijaanza kazi na kumpata Meya? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka Mkurugenzi wa Mji Mdogo?

Supplementary Question 2

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mamlaka ya Mji
wa Lushoto sasa hivi ina zaidi ya miaka nane. Je, Serikali haioni sasa imefikia wakati wa kuipandisha hadhi kuwa Halmashauri ya Mji wa Lushoto ukizingatia Mheshimiwa Jafo alitembelea kule na kuona Mji wetu wa Lushoto jinsi unavyopendeza na ulivyokuwa mkubwa? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani concern hii Mheshimiwa Mbunge aliileta ofisini kwetu na ndiyo maana Waziri wangu aliniagiza niweze kufika Lushoto kule na nimeweza kufika. Kimsingi wana mambo mengi, kuanzisha hii Mamlaka ya Mji wa Lushoto, suala zima la Halmashauri ya Mlalo, kuna mambo mengi sana yamejitokeza kule. Kwa hiyo, kama Serikali Waziri wangu alituma timu kule ikaenda kufanya assessment na taarifa zile ziko Ofisi ya TAMISEMI katika uchambuzi pale itakapoonekana kwamba vigezo vyote vimekidhi basi hakutakuwa na tatizo. Mheshimiwa Shekilindi naomba vuta subira tu wakati maamuzi yanaenda kufanyika kwa kuangalia kama imekidhi vigezo mbalimbali basi mtapata jibu halisi. Na mimi nimefika pale nimeona ile hali halisi basi tuache michakato iweze kuendelea baadaye tufanye maamuzi sahihi.

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Wananchi wa wa Kibiti wanaishukuru Serikali kwa kupata Mji Mdogo Kibiti na kufanya uchaguzi wa Mwenyekiti na viongozi. (a) Je, kuna tatizo gani hadi leo Mamlaka ya Mji haijaanza kazi na kumpata Meya? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka Mkurugenzi wa Mji Mdogo?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Sitakuwa mbali sana na wanaohitaji miji ipandishwe hadhi. Kwa kuwa kata ya Majimoto sasa imekuwa kubwa kiasi ambacho inatakiwa kupandishwa hadhi na tumekwishaleta maombi katika Wizara inayohusika. Je, ni lini sasa maombi hayo yatashughulikiwa ili kata ya Majimoto iwe Mji Mdogo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kupandisha hadhi na naomba nijibu na Wabunge wengine kwa sababu nimeona wengi wamesimama humu ndani na concern yao wote inafanana na ndiyo maana tuliunda kikosi kazi kwenda kupitia maeneo mbalimbali ikiwemo kwako Majimoto Mheshimiwa Mbunge. Jambo lile sasa liko ofisini kwetu linafanyiwa uchambuzi wa kina, naomba nikutoe hofu kwamba uchambuzi ule wa kina ukishafanyika basi maamuzi sahihi yatafanyika kwa mujibu wa sheria ambapo Waziri mwenye dhamana amepewa mamlaka hayo. Naomba vuta subira tu wakati kazi hii inawekwa vizuri lakini siyo Majimoto peke yake nikifahamu Dongobesh kule na maeneo mengine wote concern yao ni hiyo hiyo, kwa hiyo kama Serikali inafanyia kazi kwa upana wake suala hili.

Name

Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Wananchi wa wa Kibiti wanaishukuru Serikali kwa kupata Mji Mdogo Kibiti na kufanya uchaguzi wa Mwenyekiti na viongozi. (a) Je, kuna tatizo gani hadi leo Mamlaka ya Mji haijaanza kazi na kumpata Meya? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka Mkurugenzi wa Mji Mdogo?

Supplementary Question 4

MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Mimi naomba nifahamu, Jimbo la Kilombero lina Halmashauri mbili, Halmashauri ya Mji wa Ifakara wenye kata tisa na Halmashauri ya Kilombero yenye kata kumi. Kama ambavyo Jimbo la Bariadi ambalo lina Halmashauri mbili, Bariadi Vijijini kuna kata ishirini na moja na Bariadi Mjini kuna kata kumi. Hata hivyo, Mbunge wa Kilombero amezuiliwa na alizuiliwa kushiriki vikao vya Halmashauri ya Kilombero. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipotaka kushiriki nimefungwa miezi sita. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mwenzangu anashiriki mwanzo mwisho sehemu zote mbili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nifahamu, ni
kwa nini mimi wa Kilombero siyo tu kwamba nimezuiliwa kushiriki vikao hata kufanya maamuzi kwenye hizi kata zangu kumi sishiriki, lakini mwenzangu wa CCM anashiriki? Sasa naomba Waziri aniambie ni kwa nini ubaguzi huu unafanyika dhidi yangu halafu mwenzangu wa CCM anaachiwa afanye kazi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nifahamu inawezekana vipi Mbunge wa Kilombero nazuiliwa kushiriki vikao…

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Mheshimiwa Lijualikali ni Mbunge ambaye ana Halmashauri mbili. Kama zilizovyo haki za Wabunge wengine katika majimbo yao na katika Halmashauri zao wanapaswa kuwa wajumbe wa vikao mbalimbali ikiwepo Kamati ya Mipango na Fedha lakini pia na Baraza la Madiwani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, inakuwa vigumu sana kulisema jambo hili kwa sababu mhusika angepaswa tu ku-balance interest za maeneo yote na akaweza kufanya Ubunge wake. Kinachotokea ni pale ambapo mhusika pia ni Diwani na Diwani wa upande mmoja wa Jimbo. Kwa hiyo, scenario yake haiwezi ika-fall in all four angles kama ilivyo scenario ya Bariadi. Kwa sababu hiyo Mheshimiwa Mbunge anayo maelekezo yangu ambapo mimi na yeye tulizungumza sana jambo hili tukiwa pamoja na Mheshimiwa Kiwanga ambayo hayo hayatekelezi. Hivyo, kwa sababu ameleta jambo hili hapa Mheshimiwa Lijualikali ofisi yangu ipo, njoo tuzungumze tuone huo ugumu unaoupata na kwa nini haitokei hivyo, tutalimaliza jambo hili, nakukaribisha sana ofisini.

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Wananchi wa wa Kibiti wanaishukuru Serikali kwa kupata Mji Mdogo Kibiti na kufanya uchaguzi wa Mwenyekiti na viongozi. (a) Je, kuna tatizo gani hadi leo Mamlaka ya Mji haijaanza kazi na kumpata Meya? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka Mkurugenzi wa Mji Mdogo?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba niulize swali kwamba mwaka 2013 Mji Mdogo wa Igunga ulianzishwa na tumekuwa na tatizo hili ambalo wanalisema wote kwamba umeanzishwa lakini haufanyi kazi. Namshukuru Waziri ameeleza kwenye swali namba 142 kwamba ni Halmashauri inatakiwa isimamie, lakini sisi tumejaribu kuishauri Halmashauri isimamie jambo hilo na nimeweza kufika ofisini kwake mara moja na akaahidi kwamba angeweza kuandika Waraka wa kumwambia Mkurugenzi au kuiambia Halmashauri ifanye jambo hilo na halijafanyika.
Namuomba Mheshimiwa Waziri hebu utusaidie kwa sababu DED sasa hivi hataki kabisa kuisikiliza hiyo Mamlaka ya Mji Mdogo wa Igunga na hawana bajeti, hawana gari, wana mtendaji tu. Tunaomba Mheshimiwa Waziri utusaidie kama ikiwezekana njoo Igunga ili mamlaka hii iweze kuanza. Ahsante sana.

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikia swali la Mheshimiwa Mbunge na tutawasiliana tuone namna bora ya kulifanya jambo hili kwa sababu ni kweli tumekwishazungumza na ni kweli nilikwishatoa maagizo lakini halitekelezeki. Kama nilivyosema, mamlaka hizi zinapoanzishwa zinalelewa na Halmashauri Mama. Kwa hiyo, kama hakuna mipango madhubuti inayopanga mchakato wa namna ya kutafuta rasilimali fedha na rasilimali watu basi tatizo linakuwa kubwa zaidi. Kwa hiyo, tutajaribu kuliona namna lilivyo na halina tofauti sana na scenario za Miji mingine Midogo iliyoanzishwa ili tuone namna bora ya kuweza kulifanya.

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Wananchi wa wa Kibiti wanaishukuru Serikali kwa kupata Mji Mdogo Kibiti na kufanya uchaguzi wa Mwenyekiti na viongozi. (a) Je, kuna tatizo gani hadi leo Mamlaka ya Mji haijaanza kazi na kumpata Meya? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka Mkurugenzi wa Mji Mdogo?

Supplementary Question 6

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kumekuwa na mkanganyiko mkubwa sana katika Halmashauri mbalimbali nchini baada ya kauli ya Mheshimiwa Rais katika sherehe za Mei Mosi juzi kule Kilimanjaro alivyosema kwamba Halmashauri yoyote au Baraza lolote la Madiwani litakalojitokeza na kutaka kumuondoa Mkurugenzi kazini au kumfukuza, Baraza hilo litavunjwa mara moja na yeye ndiye mwenye mamlaka ya kumteua Mkurugenzi kwa hiyo atahakikisha anaifuta Halmashauri hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa mujibu wa Sheria
za Serikali za Mitaa, Waheshimiwa Madiwani ndiyo wasimamizi wa shughuli na miradi ya maendeleo na mapato na matumizi ya fedha za Halmashauri.
Je, Mkurugenzi akiwa ametumia fedha vibaya na akatumia madaraka yake vibaya, ni utaratibu gani ambao Waheshimiwa Madiwani watautumia kama siyo kumuondoa Mkurugenzi wakati Rais tayari ameshawaonya na amewaambia kwamba ataivunja Halmashauri hiyo? Ahsante.

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza si kweli kwamba kauli ya Mheshimiwa Rais imeleta mkanganyiko. Kauli ya Mheshimiwa Rais imemaanisha pale ambapo mkakati unafanywa na Waheshimiwa Madiwani kumuondoa Mkurugenzi kwa maslahi binafsi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa uzoefu wa mwaka wangu mmoja na miezi kadhaa yote mawili yanatokea, wakati mwingine kunakuwa na mkakati wa upande wa watumishi kumuondoa Mwenyekiti na wakati mwingine kuna mkakati kwa upande wa Madiwani kumuondoa Mkurugenzi kwa sababu tu maslahi yamegongana. Kwa hiyo, Mheshimiwa Rais anapolizungumzia hili hazungumzii kwa scenario unayoisema ya kwamba kumetokea ubadhirifu na wala Mheshimiwa Rais halindi wabadhirifu, anazungumzia pale ambapo kuna utaratibu unapangwa wa Madiwani kumuondoa Mkurugenzi anayesimamia watu wasifanye wizi, ndicho anachokizungumzia.
Kwa hiyo, huo mfano mwingine baki nao lakini wa
Rais ni huu aliokuwa anausema kwamba pale kunapokuwa kuna mkakati wa kumuondoa Mkurugenzi ambaye anasimamia fedha za Halmashauri hapo yuko tayari kuivunja Halmashauri na mimi mwenyewe nasema wala haitafika hata kwake mimi mwenyewe nitavunja hiyo Halmashauri.