Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Tagamenda Substation ni kituo kikubwa kati ya vituo vinavyosafirisha umeme wa Gridi ya Taifa kwani kinapokea umeme kutoka Mtera, Kidatu na Kihansi, lakini vijiji vya Tagamenda, Ikuvilo na Wangama vinavyozunguka kituo hicho havina huduma ya umeme ingawa ndivyo vinalinda kituo hicho. (a) Je, ni kwa nini Serikali inashindwa kutoa huduma ya umeme katika vijiji vinavyozunguka kituo hicho? (b) Je, ni sababu gani zinazofanya vijiji hivyo kukosa kupatiwa huduma hata ya umeme wa REA?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali la kwanza, katika majibu ya Mheshimiwa Waziri amesema kuwa REA III imeanza Machi, 2017. Kwa kuwa wananchi katika vijiji hivyo vya Wangama, Ikuvilo, Tagamenda, Lupembelwasenga pamoja na Lyamgungwe ni wakulima na wanajihusisha na kilimo cha umwagiliaji na kuna wawekezaji ambao wameonesha nia ya kujenga viwanda na tunasema tunahitaji Tanzania ya viwanda lakini umeme haupo. Naomba commitment ya Serikali ni lini watapata umeme kwa sababu imekuwa ni muda mrefu kutopatiwa umeme katika maeneo hayo ili wanufaike na viwanda? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika kipengele
cha kwanza majibu ya Waziri ni tofauti kabisa na hali halisi ya eneo hilo la Malulumo kwa sababu mimi natokea eneo hilo na wanasema utekelezaji umefanyika kwa 90%. Je, Waziri yuko tayari kuongozana na mimi akaone huo utekelezaji wa 90% uliopo maeneo yale? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze na swali la pili, niko tayari kufuatana na Mheshimiwa Grace kwenda kwenye eneo lake ili kuangalia utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya Tatu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Grace tukimaliza Bunge tu mguu mmoja mimi na wewe Iringa tukamalize kazi hiyo, lakini kwa ruhusa yako Mwenyekiti. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini sasa vijiji vilivyobaki vitapatiwa umeme. Awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Grace na Wabunge wote wa Mkoa wa Iringa kwa jinsi ambavyo wanafuatilia utekelezaji wa miradi ya umeme. Niwahakikishie kwamba tarehe 21 Machi, 2017 tulizindua rasmi utekelezaji wa Mradi wa Umeme Awamu ya Tatu katika Mkoa wa Iringa na eneo la Iliwa kwa Mheshimiwa Mwamoto ndipo tulipofanyia uzinduzi kwa niaba ya mkoa.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niwahakikishie kabisa Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Iringa pamoja na Mufindi, Kilolo, Njombe, tumeshawakabidhi wakandarasi wawili, NACROI na NAMIS na wameshaanza utekelezaji wa kazi hiyo. Kwa hiyo, kuanzia Machi tumeshaanza kutekeleza mradi huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji ambavyo amevitaja Mheshimiwa Grace vya Wangama, Lupembelwasenga, Tagamenda na Mseke pamoja na vijiji vingine ambavyo amevitaja na kwa Mheshimiwa Mwamoto vitapatiwa umeme katika awamu hii ya mradi. Nimeenda kwa Mheshimiwa Mwamoto na Waheshimiwa Wabunge wengine, nimeenda Nang’uruwe, Kihesa Mgagao na huko tumeshawapelekea umeme. Kwa hiyo, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba utekelezaji wa mradi huu umeanza na utakamilika mwaka 2020/2021.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Tagamenda Substation ni kituo kikubwa kati ya vituo vinavyosafirisha umeme wa Gridi ya Taifa kwani kinapokea umeme kutoka Mtera, Kidatu na Kihansi, lakini vijiji vya Tagamenda, Ikuvilo na Wangama vinavyozunguka kituo hicho havina huduma ya umeme ingawa ndivyo vinalinda kituo hicho. (a) Je, ni kwa nini Serikali inashindwa kutoa huduma ya umeme katika vijiji vinavyozunguka kituo hicho? (b) Je, ni sababu gani zinazofanya vijiji hivyo kukosa kupatiwa huduma hata ya umeme wa REA?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mji wa Maswa umekosa maji kwa mara nyingine tena kwa muda zaidi ya wiki moja baada ya operesheni kata umeme. Kata umeme imeathiri hadi mamlaka ambazo ziko daraja la tatu ambapo kama Mamlaka ya Maji ya Mji wa Maswa iko daraja la tatu kwa hiyo bili zake zinalipwa na Wizara, hawajilipii bili wao wenyewe. Kwa hiyo Wizara haijalipa TANESCO …
TANESCO wanakata. Swali langu, napenda kupata commitment ya Serikali ni lini Maswa watarudishiwa umeme katika Mamlaka ya Maji ili wananchi wa Maswa waweze kupata maji katika Mji wa Maswa? Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo hilo nakiri kweli lipo lakini Serikali tumekaa kikao Wizara ya Maji na Hazina pamoja na TAMISEMI tumekubaliana. Vilevile tarehe 8 Mei Makatibu Wakuu wa Wizara ya Nishati na Wizara ya Maji watakaa kukamilisha suala hili ili kuhakikisha tatizo la malipo lililokuwepo tukishakaa na Hazina tutalimaliza ili maeneo yote umeme uweze kurejeshwa.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Tagamenda Substation ni kituo kikubwa kati ya vituo vinavyosafirisha umeme wa Gridi ya Taifa kwani kinapokea umeme kutoka Mtera, Kidatu na Kihansi, lakini vijiji vya Tagamenda, Ikuvilo na Wangama vinavyozunguka kituo hicho havina huduma ya umeme ingawa ndivyo vinalinda kituo hicho. (a) Je, ni kwa nini Serikali inashindwa kutoa huduma ya umeme katika vijiji vinavyozunguka kituo hicho? (b) Je, ni sababu gani zinazofanya vijiji hivyo kukosa kupatiwa huduma hata ya umeme wa REA?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nilitaka nimueleze Mheshimiwa Waziri kwamba Mkoa wa Mtwara ndiko inakozalishwa gesi inayozalisha umeme wa Dar es Salaam ambako haukatiki kila mara, kiasi tumeanza kuamini gesi yetu haitunufaishi ni bora tungerudishiwa yale majenereta yaliyokuwa yanazalisha umeme Mtwara wakati huo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la umeme la Mtwara linasababishwa na kuharibika kwa transfoma ya jenereta moja yake ambayo nafahamu mpaka sasa kuna mvutano mkubwa kati ya TANESCO pamoja na MANTRAC Tanzania Limited kwa ajili ya ku-supply ile transfoma kwa sababu ya madeni sugu ambayo TANESCO hawajalipa.
Mheshimiwa Waziri, naomba utueleze kinagaubaga ni lini matatizo ya TANESCO na MANTRAC yatakwisha ili kuwarejeshea wananchi wa Mtwara umeme wa uhakika? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mweyekiti, ni kweli kabisa liko tatizo la kuharibika kwa mashine moja Mtwara kiasi cha kushindwa kupeleka megawatt 18 kwa ujumla wake. Kwa sasa hivi ni kweli kabisa Mtwara wanapata megawatt chini ya 18, wanapata 16 na 15.6
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wa Mtwara na Lindi lakini hatua zilizochukuliwa ni kwamba hivi sasa ukarabati umeshaanza. Mgogoro uliokuwepo kati ya TANESCO na MANTRAC umekwisha na jenereta inatengenezwa, ni hatua ya kwanza. Hatua ya pili, Mtwara tunawaongezea mashine nyingine sita ambapo kila mashine itakuwa na megawatt mbili. Kwa hiyo, mtakuwa na megawatt nyingine za ziada 12 na jumla kuwa na megawatt 30. Kwa hiyo, sasa umeme wa Mtwara pamoja na Lindi maeneo ya jirani utakuwa ni wa uhakiki zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala hili linashughulikiwa na baada ya Bunge hili Mheshimiwa Mbunge tutakwenda wote kukagua mashine hii ikiwa imeshakamilika na umeme unapatikana.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Tagamenda Substation ni kituo kikubwa kati ya vituo vinavyosafirisha umeme wa Gridi ya Taifa kwani kinapokea umeme kutoka Mtera, Kidatu na Kihansi, lakini vijiji vya Tagamenda, Ikuvilo na Wangama vinavyozunguka kituo hicho havina huduma ya umeme ingawa ndivyo vinalinda kituo hicho. (a) Je, ni kwa nini Serikali inashindwa kutoa huduma ya umeme katika vijiji vinavyozunguka kituo hicho? (b) Je, ni sababu gani zinazofanya vijiji hivyo kukosa kupatiwa huduma hata ya umeme wa REA?

Supplementary Question 4

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize swali moja la nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa vijiji vya Makutupa, Mlembule, Tambi, Bolisazima na Mgoma tayari nyaya na nguzo zimeshawekwa bado transfoma. Sasa namuuliza Naibu Waziri, vijiji hivi vitapata lini transfoma ili waweze kuanza kupata huduma ya umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali moja la Mheshimiwa Lubeleje, Mbunge Mkongwe katika Bunge hili, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kulikuwa na transfoma mbili mbovu katika Jimbo lake na jana tulikuwa tunawasiliana na Meneja na amenihakikishia kwamba mwisho wa wiki hii transfoma mbili zitapatikana. Nimpongeze sana Mheshimiwa Lubeleje kwa niaba ya wananchi wake na nimwambie kwamba transfoma hizi mbili zitapatikana Ijumaa (kesho kutwa) mwezi huu. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Tagamenda Substation ni kituo kikubwa kati ya vituo vinavyosafirisha umeme wa Gridi ya Taifa kwani kinapokea umeme kutoka Mtera, Kidatu na Kihansi, lakini vijiji vya Tagamenda, Ikuvilo na Wangama vinavyozunguka kituo hicho havina huduma ya umeme ingawa ndivyo vinalinda kituo hicho. (a) Je, ni kwa nini Serikali inashindwa kutoa huduma ya umeme katika vijiji vinavyozunguka kituo hicho? (b) Je, ni sababu gani zinazofanya vijiji hivyo kukosa kupatiwa huduma hata ya umeme wa REA?

Supplementary Question 5

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri anisaidie, kwanza napongeza kasi ya usambazaji wa umeme lakini kuna tatizo la nguzo kwenda chache.
Naomba aniambie katika kata ya Bumanga kwenye kiwanda cha akina mama cha kusindika mbogamboga, msitiki, kanisa na shule walikosa nguzo hivyo hamna umeme, ni lini mtapeleka nguzo hizo ili waweze kupata umeme? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile Mheshimiwa Mlata ameniambia kwamba kuna tatizo la nguzo, nitawasiliana na wataalam leo hii ikiwezekana mwisho wa wiki hii au wiki ijayo ziweze kupatikana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kusema kwamba kwa sasa nguzo, mashine na transfoma zinapatikana hapa nchini hatuagizi kutoka nje. Kwa hiyo, uhakika wa upatikanaji wa nguzo pamoja na vifaa vingine utakuwa ni rahisi zaidi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mlata tutafuatana lakini mwisho wa wiki hii au wiki ijayo nguzo zitapatikana.