Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUSAN A. J. LYIMO (K.n.y. MHE. NAJMA MURTAZA GIGA) aliuliza:- Matumizi ya SHISHA yamegundulika kuwa ni miongoni mwa aina ya uvutaji wa sigara ambao wauzaji wengine huchanganya na aina mbalimbali za dawa za kulevya na vileo vikali na kusababisha vijana wadogo kuathiriwa kwa kiasi kikubwa. Je, kwa nini Serikali hadi sasa inaendelea kuruhusu matumizi ya SHISHA kwenye baadhi ya migahawa na hoteli kubwa ambayo inatumiwa na watu wa rika zote?

Supplementary Question 1

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu ya Serikali, lakini ni wazi kwamba siku za nyuma kulikuwa na mgogoro kati ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na Bwana Siro kuhusiana na suala hili. Naomba kujua wakati ambapo Polisi walisema hakuna, lakini Mkuu wa Mkoa alikuwa anasema zipo. Je, huu mgogoro umeishia wapi?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba hakukuwa na mgogoro wowote kati ya Kamanda wa Kanda Maalum na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa ni viongozi wanaofanya kazi kwa pamoja na mara zote maelekezo ya Kamati ya Ulinzi na Usalama imekuwa ikielekezwa kwenye utekelezaji na shughuli hiyo imeendelea kufanyika na kama nilivyosema Mheshimiwa Waziri Mkuu alishaelekeza na Mikoa yote imeitikia na sisi kama Wizara tunawaelekeza wote wanaokuwa field kuhakikisha kwamba maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu yanafanyiwa kazi bila kupunguza hata nukta.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. SUSAN A. J. LYIMO (K.n.y. MHE. NAJMA MURTAZA GIGA) aliuliza:- Matumizi ya SHISHA yamegundulika kuwa ni miongoni mwa aina ya uvutaji wa sigara ambao wauzaji wengine huchanganya na aina mbalimbali za dawa za kulevya na vileo vikali na kusababisha vijana wadogo kuathiriwa kwa kiasi kikubwa. Je, kwa nini Serikali hadi sasa inaendelea kuruhusu matumizi ya SHISHA kwenye baadhi ya migahawa na hoteli kubwa ambayo inatumiwa na watu wa rika zote?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante nami nataka kujua hapo kwamba kwa kuwa wakati shisha linapigwa marufuku, huku nyuma kuna watu walikuwa wamepewa leseni ya kufanya hiyo biashara kwa sababu ilikuwa inaonekana ni biashara halali. Je, Serikali inatoa tamko gani kuhusu hilo? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, masuala yote yanayohusu afya za Watanzania ni kipaumbele cha Serikali na kwa kuwa ni kipaumbele cha Serikali, jambo la kwanza tunalofanya ni kuokoa maisha ya Watanzania. Wakati tunafanya hivyo, ndiyo maana tunasema tunaliwekea utaratibu mzuri wa Kisheria na hivi tunavyoongea, ukienda kwenye ukurasa wa 15 wa kitabu cha hotuba ya Waziri wa Afya, ameongelea utaratibu ambao utachukuliwa na tayari alishatungia kanuni. Kwa hiyo, inasubiria mashauriano ya mwisho ndani ya Serikali ambayo yanazingatia concern aliyoitoa Mheshimiwa Shangazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Shangazi, n kwa kutambua kwamba hilo jambo lilikuwepo lakini ni lazima tuzingatie afya za Watanzania na tuzingatie utaratibu ambao utaweka utaratibu wa kisheria wa kudumu ili kuweza kuhakikisha kwamba afya za Watanzania zinalindwa. (Makofi)

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. SUSAN A. J. LYIMO (K.n.y. MHE. NAJMA MURTAZA GIGA) aliuliza:- Matumizi ya SHISHA yamegundulika kuwa ni miongoni mwa aina ya uvutaji wa sigara ambao wauzaji wengine huchanganya na aina mbalimbali za dawa za kulevya na vileo vikali na kusababisha vijana wadogo kuathiriwa kwa kiasi kikubwa. Je, kwa nini Serikali hadi sasa inaendelea kuruhusu matumizi ya SHISHA kwenye baadhi ya migahawa na hoteli kubwa ambayo inatumiwa na watu wa rika zote?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Vijana wengi wanaotumia shisha, bangi, madawa ya kulevya na pombe kali kali hizi, wanatumia kutokana na kukata tamaa katika maisha; nami siamini sana katika kutunga sheria, kuwakamata na kuwaadhibu. Mfano mzuri, juzi Waziri Mkuu Serikali ilipiga marufuku utumiaji wa viroba, lakini sasa kwa taarifa ya Mheshimiwa Waziri kilevi kingine kimeanzishwa. Sasa vijana wanaanza kuvuta gundi kitu ambacho ni kibaya zaidi. (Makofi)
Sasa Je, sisi kama Taifa, Serikali kuna utaratibu gani wa kuwasaidia vijana hawa ambao wengi wamekata tamaa ili waweze kupata matumaini katika maisha na waache mambo hya bila lazima ya kutunga sheria au kuwakamata?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti nimshukuru sana Mheshimiwa Selasini kwa swali lake la nyongeza. Kubwa ambalo tunalifanya sasa hivi ili kuwaepusha vijana wa Kitanzania na matumizi ya tumbaku na vileo ni kuendelea kutoa elimu kwa jamii kupitia Luninga na redio, lakini pia tumechapisha vijarida mbalimbali ili kuonesha madhara ya tumbaku pamoja na matumizi ya pombe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, wale ambao walikuwa tayari wanatumia kwa mfano, madawa ya kulevya, tumeanza mpango wa kuongeza vituo vya kutoa dawa (Methodone). Kwa hiyo, siyo tu Dar es Salaam lakini tutaanzisha Mbeya, Arusha, Tanga, Kilimanjaro pamoja na Dodoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kubwa ni kwamba leo ni siku ya familia, kwa hiyo, tunatoa wito kwa wazazi, walezi kutimiza wajibu wao wa msingi wa malezi bora kwa watoto wao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa sababu nimepata pia fursa ya kusema leo ni Siku ya Familia Duniani. Kwa hiyo, familia bora ndiyo msingi wa maendeleo ya nchi yoyote. (Makofi)

Name

Mariamu Ditopile Mzuzuri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUSAN A. J. LYIMO (K.n.y. MHE. NAJMA MURTAZA GIGA) aliuliza:- Matumizi ya SHISHA yamegundulika kuwa ni miongoni mwa aina ya uvutaji wa sigara ambao wauzaji wengine huchanganya na aina mbalimbali za dawa za kulevya na vileo vikali na kusababisha vijana wadogo kuathiriwa kwa kiasi kikubwa. Je, kwa nini Serikali hadi sasa inaendelea kuruhusu matumizi ya SHISHA kwenye baadhi ya migahawa na hoteli kubwa ambayo inatumiwa na watu wa rika zote?

Supplementary Question 4

MHE. MARIAM D. MZUZURI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona na kunipa nafasi. Swali langu, je, kwa tafiti ambazo zimefanywa nchi nyingi sana, ikiwemo kwa nafasi kubwa nchi za Kiarabu, sigara ina madhara makubwa, mara dufu kuliko hii Shisha na kila siku tunasema ajira, ajira. Biashara ya Shisha ilikuwa inaajiri vijana wengi sana na kweli wamepata matatizo tangu hili zuio.
Swali langu kwa Serikali; je, mlifanya utafiti wa kutosha wa kuona kwamba hii Shisha ina madhara makubwa kuliko sigara? Nashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mariam kwa kutaka kujua kuhusu utafiti wa jambo hili. Nimhakikishie tu kwamba jambo hili lilifanyiwa utafiti na Wizara ya Afya na hivi vitu ambavyo vina vilevi, ubaya wake ni kwamba vijana wetu hawavitumii peke yake, wanachanganya na vitu vingine, kwa hiyo, wanaongeza makali zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ajira, nimhakikishie Mheshimiwa Mariam kwamba vijana bado wana fursa nyingi sana na nitolee mfano wa kwake yeye mwenyewe, ni mmoja wa vijana wanaofanya vizuri sana kwenye kilimo na yeye ni shahidi na amefanikiwa sana; ni mmoja wa Waheshimiwa Wabunge vijana waliofanikiwa sana kwenye kilimo. Kwa maana hiyo, vijana wengine wanaweza wakaiga mfano ule, wakalima mazao ya biashara. Mheshimiwa Mariam analima ufuta, wao nawakaribisha walime alizeti ama mazao mengine yanayostawi katika mikoa yao ili waweze kufanya biashara iliyo halali isidhuru maisha ya watu wengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ajira ya kudumu, ndiyo maana Mheshimiwa Rais ana mpango wa muda mrefu wa kukuza uchumi kwa kuhakikisha kwamba fedha zote zinatumika vizuri ili kuweza kutengeneza uchumi wa viwanda, uchumi unaojitegemea, uchumi unaotengeneza ajira nyingi ambazo zitakuwa zinaingiza kipato halali kwa vijana na afya za Watanzania.