Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yussuf Haji Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS (K.n.y MHE. MBAROUK SALIM ALI) aliuliza:- Moja ya jitihada za Serikali za kufufua Kiwanda cha General Tyre kilichopo Arusha ni pamoja na kuendeleza kilimo cha mpira katika mashamba yaliyoko Tanga na Morogoro ili kupata malighafi. Je, mashamba hayo yana ukubwa gani na umri gani?

Supplementary Question 1

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu marefu ya Mheshimiwa Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshiwa Naibu Spika, katika majibu yake Mheshimiwa Waziri amekiri kwamba mashamba haya yamekuwa ya muda mrefu na uzalishaji wake umekuwa mdogo sana. Pia mashamba haya yanatumia hekari nyingi sana, kwa hiyo, yamechukua sehemu kubwa ya ardhi ya Tanzania. Pamoja na kukiri kwamba hakuna uhusiano baina ya Kiwanda ya General Tyre na mashamba haya. Namuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, je, Serikali iko tayari kuleta matumizi mbadala ya mashamba haya kwa sababu hayalisaidii Taifa?(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Kiwanda cha General Tyre si kiwanda kipya ni kiwanda cha zamani sana na kilikuwa kinazalisha. Hata hivyo, marekebisho yake naambiwa yafanyiwa utafiti, ukiuliza utafiti, ukiuliza utafiti, hakimaliziki kiwanda kufanyiwa utafiti ili kuzalisha. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri haoni kwamba hatujawa tayari kuingia katika Tanzania ya viwanda kwa mwendo huu?(Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kuhusu mipira au zao la mpira kuchukua ardhi kubwa na hiyo ardhi kutoweza kutumika kwa tija zaidi, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sasa mashamba ya mpira tuliyonayo hayajachukua ardhi kubwa sana. Tunachofikiria sasa kama Wizara na Serikali ni kujaribu kutafuta ardhi nyingine ili tuongeze uzalishaji wa mpira. Kwa sasa tunafikiri mpira soko lake limeimarika tena hata jirani nchini Kenya kuna soko, lakini vilevile China kuna soko kubwa. Kwa hiyo, sasa tunajaribu kuangalia namna ya kuwekeza tena kwenye mpira ili liwe tena ni zao ambao wakulima wetu wanaweza kunufaika nalo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa sasa hatufikirii ile ardhi iende kwenye matumizi mengine lakini tunachofanya ni kuendelea kuimarisha mashamba yaliyopo lakini vilevile kujaribu kuongeza ardhi nyingine ili kilimo cha mpira kiweze kupanuka. Vilevile kujaribu kuimarisha teknolojia ambayo tunatumia kwa sasa ili iweze kuendana na mahitaji ya sasa ya soko la mpira duniani.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ni kuhusiana na General Tyre. Kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, Serikali inaendelea kufanya tathmini kuhusu namna bora ya kurejesha tena Kiwanda cha General Tyre kiingie katika uzalishaji. Kimsingi tulichosema ni kwamba taarifa ya awali inaonyesha kwamba tunahitaji kuboresha teknolojia iliyopo, lakini vilevile mfumo wa uendeshaji uwe ni kwa utaratibu wa kushirikiana na sekta binafsi kwa maana ya PPP ili Serikali iweze kubakia na hisa chache tu na hasa zile zinazolingana na mali au uwekezaji ambao Serikali tayari umeshaufanya, lakini huku Serikali ikijaribu kuvutia wawekezaji ili iendeshwe kwa ubia na sekta binafsi. Kwa hiyo, siyo kwamba Kiwanda cha General Tyre kimetupwa lakini ni kwamba sasa jitihada zinaendelea ili kukifufua ili kiweze kufanya kazi tena.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS (K.n.y MHE. MBAROUK SALIM ALI) aliuliza:- Moja ya jitihada za Serikali za kufufua Kiwanda cha General Tyre kilichopo Arusha ni pamoja na kuendeleza kilimo cha mpira katika mashamba yaliyoko Tanga na Morogoro ili kupata malighafi. Je, mashamba hayo yana ukubwa gani na umri gani?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Katika nchi yetu ajali za barabarani zimekuwa nyingi sana na moja kati ya sababu za ajili hizi ni matairi ya mitumba yanayoagizwa kutoka nje. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, labda niseme Tanzania ni nchi pekee ambayo inaagiza matairi ya mitumba ikijua kabisa kwamba matairi haya yanakuwa yamemaliza muda wake na inaweza ikawa kisababishi kikubwa cha ajali. Sasa wakati tukisubiri kiwanda hiki kufufuliwa, hadithi ambayo imekuwa ni ya miaka mingi, je, Serikali ina mpango gani wa kupiga marufuku uingizaji wa matairi yaliyotumika katika nchi ambayo yanasababisha ajali?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba ajali za barabarani zimeendelea kuongezeka nchini na inawezekana kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge kwamba matairi yasiyo na ubora ni moja kati ya visababishi. Kimsingi suala la ajali za barabarani ni suala ambalo Serikali linalichukulia kwa uzito sana, ni kero kubwa inaondoa maisha ya wananchi wetu. Kwa hiyo, Serikali inaangalia ni namna gani ya kudhibiti ajali hizo ikiwa ni kuangalia visababishi kama hilo la matairi, kwa sababu kuna visababishi vingine mfano uendeshaji usiozingatia utaratibu, uendeshaji kupita speed inayotakiwa, lakini vilevile madereva kulewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi Serikali inaangalia suala la ajali katika ujumla wake na visababishi vile itahakikisha inavifanyia kazi ili tuendelee kupunguza ajali barabarani. Kwa hiyo, kama hilo la matairi ni moja ya visababishi kwa vyovyote vile Serikali inalifanyia kazi.

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS (K.n.y MHE. MBAROUK SALIM ALI) aliuliza:- Moja ya jitihada za Serikali za kufufua Kiwanda cha General Tyre kilichopo Arusha ni pamoja na kuendeleza kilimo cha mpira katika mashamba yaliyoko Tanga na Morogoro ili kupata malighafi. Je, mashamba hayo yana ukubwa gani na umri gani?

Supplementary Question 3

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, shamba la Kihuhwi ambalo
lipo Wilayani Muheza ni kweli lilikuwa linalima mpira na linaendelea kulima mpira na lilikuwa lina- supply kwenye kiwanda cha General Tyre - Arusha. Sasa hivi shamba hilo ni moja ya mashamba ambalo limeshafutiwa hati na Mheshimiwa Rais. Mheshimiwa Naibu Waziri, haoni sasa kutokana na matatizo ya Kiwanda cha General Tyre - Arusha, mikakati ifanyike kiwanda hicho kiwe na mashine za kisasa na kihamishiwe Wilayani Muheza ambapo nafasi tunaweza kutoa na kiwe karibu na malighafi?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anapendekeza kwamba tuhamishe Kiwanda cha General Tyre tupeleke Muheza. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari kuna timu inafanya kazi ya kuangalia namna bora ya kufufua Kiwanda cha General Tyre.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nimhakikishie tu kwamba nitawapelekea pendekezo la kuangalia kama inawezekana kupeleka Muheza, lakini zaidi zaidi ni vizuri vilevile kuangalia uwezekano wa kuanzisha kiwanda kipya Muheza.