Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO aliuliza:- Stesheni nyingi za reli hazina huduma nzuri kama maji, vyoo na sehemu za kukaa wakati wa mvua na hivyo abiria wengi hasa akina mama na watoto kupata shida. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuboresha huduma hizo ili kuwaondolea adha hiyo kubwa akina mama na watoto?

Supplementary Question 1

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nchi nyingi duniani stesheni za reli ni vituo vya biashara tofauti kabisa na nchini kwetu Tanzania. Serikali inaweza kueleza ni kwa nini stesheni kubwa kama Morogoro, Dodoma, Tabora na Mwanza huduma huwa zimedumaa na hakuna huduma za biashara? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, TRL ipo tayali kushirikiana na sekta binafsi kuendesha stesheni za reli kwa kuziboresha ikiwemo kuweka hoteli, huduma za maduka na kadhalika? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Halima Abdallah Bulembo kuuliza kitu ambacho Serikali nayo imekuwa ikijiuliza ni kwa nini wafanyabiashara hawachangamkii fursa za kufanya biashara katika maeneo ya stesheni za reli. Kwa sababu ametupa nguvu zaidi leo, suala hili tutaendelea kulisukuma, TRL waangalie uwezekano wa kuwahamasisha wafanyabiashara washirikiane nao kama wataona hili linafaa katika mazingira ambayo wanafanyia biashara hiyo ya reli.

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO aliuliza:- Stesheni nyingi za reli hazina huduma nzuri kama maji, vyoo na sehemu za kukaa wakati wa mvua na hivyo abiria wengi hasa akina mama na watoto kupata shida. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuboresha huduma hizo ili kuwaondolea adha hiyo kubwa akina mama na watoto?

Supplementary Question 2

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa sisi wadau wa reli tuna imani kubwa na Wizara lakini tuna imani kubwa na Mkurugunzi wa TRL, Bwana Masanja lakini tumekuwa na kero kubwa ya kutokukata tiketi bila kuwa na kitambulisho huku tukijua mazingira ya stesheni za vijiji zilivyo, tukijua watu wetu wanaoishi vijijini walivyo. Mtu akiwa mgonjwa mahuhuti hana kitambulisho anataka kwenda stesheni yenye zahanati anakataliwa kupewa tiketi. Je, Wizara pamoja na Shirika inakubaliana na mimi kufuta hilo sharti la vitambulisho ili mtu aweze kupata tiketi? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimia Naibu Spika, ni kweli kuna adha katika suala la uhitaji wa tiketi na tumeliona hilo, lakini kuna ukweli vilevile wapo watu wengi wamekuwa wakitumia fursa hiyo ya kutotumia kitambulisho kurusha tiketi, wanakusanya tiketi nyingi wanakuja kuwauzia watu wengine. Kwa upande wa pili vilevile suala la kiusalama, watu wengi sana ambao siyo Watanzania wamekuwa wakitumia safari zetu za reli na hivyo kuonekana kwamba TRL inashiriki katika kusafirisha wasafiri haramu. Kwa hiyo, tutaangalia katika hasara na faida ya suala hilo, kwa sasa naomba atuvumilie tutaendelea kufuata huo utaratibu hadi hapo tutakapoona kwamba changamoto hizi mbili kubwa zitafutiwe namna nyingine ya kuzishughulikia.

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO aliuliza:- Stesheni nyingi za reli hazina huduma nzuri kama maji, vyoo na sehemu za kukaa wakati wa mvua na hivyo abiria wengi hasa akina mama na watoto kupata shida. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuboresha huduma hizo ili kuwaondolea adha hiyo kubwa akina mama na watoto?

Supplementary Question 3

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa fursa hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, matatizo ya vituo vya reli yanafanana sana na matatizo ya vituo vya boti vinavyomilikiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari - TPA. Kituo cha boti cha Nyamisati hakina vyoo, maji na migahawa. Je, ni lini Naibu Waziri ataielekeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari - TPA wakajenge vyoo, maji, umeme pamoja na masuala mengine ya kijamii? Ahsante sana.(Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukulia aliyoyasema ni mapendekezo, tumepokea mapendekezo yake na kwa sababu anajua kile kituo cha Nyamisati hivi sasa ndiyo kinaanza kufanyiwa kazi ya kujengwa basi watakapokuja katika hatua za ujenzi watu wa TPA wafikirie vilevile mapendekezo ambayo Mheshimiwa Dau ameyatoa ili yaweze kushughulikiwa.