Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Wilaya ya Kigamboni ina uwekezaji mkubwa katika sekta ya nyumba na viwanda, mahitaji ya umeme kwa sasa ni zaidi MW 20; lakini ni MW 8 tu zinazopatikana, nao umekuwa ukikatika mara kwa mara kutokana na mahitaji makubwa pamoja na uchakavu wa miundombinu ya umeme. (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha Kigamboni inapatikana umeme wa uhakika? (b) Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha kupoozea umeme (substation) katika Wilaya ya Kigamboni kutokana na mahitaji makubwa ya umeme?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ambayo yanatupa matumaini wananchi wa Kigamboni hususani kwa changamoto ambayo inatukabili. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, katika mwaka
wa fedha 2017/2018 Wilaya ya Kigamboni haikupata miradi mipya na hii inatokana na kwamba miradi ya mwaka jana (2016/2017) haikutekelezwa kikamilifu. Changamoto moja ilikuwa ni hali ya upatikanaji wa vifaa kwa maana ya transfoma, nguzo ndogo pamoja nyaya. Je, Naibu Waziri anaweza akatuhakikishia kwamba katika mwaka huu wa fedha transfoma zaidi ya 30, nyaya kilometa zaidi ya 30 na nguzo takribani 1,000 ambazo tunazihitaji tunaweza tukazipata ili kutekeleza miradi hii?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, Kigamboni iliingizwa katika REA Awamu ya Pili na kuna vijiji ambavyo vilirukwa. Je, utekelezaji wa REA Awamu ya Tatu kwa maeneo ambayo yalibaki unaanza lini?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda nichukue nafasi hii kumshukuru na kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge wa Kigamboni jinsi anavyofuatilia maendeleo ya wananchi wa Kigamboni.(Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini kuhusiana na suala la vifaa, kwanza kabisa tukiri kwamba kulikuwa na shida ya upatikanaji wa nguzo, transfoma pamoja miundombinu ya TANESCO, lakini kuanzia mwezi Juni kwa niaba ya wananchi wa Kigamboni na Watanzania wengine wote, sasa nguzo zinapatikana hapa nchini na zinatosha kupeleka miundombinu katika maeneo yote. Nitoe tu tamko kwamba katika nchi nzima tulikuwa na wateja 29,000 ambao hawajaunganishiwa umeme wakati wameshalipia kuunganishiwa umeme, lakini wananchi hao wamepelekewa umeme bado wananchi 32 tu. Kigamboni eneo ambalo ni muhimu sana hadi sasa tumepeleka nguzo 2,100 na wateja waliobaki ni 30. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, wananchi wako wa Kigamboni Mheshimiwa Ndugulile kule Mwanzo Mgumu tumeshawapelekea nguzo, Msongozi kwa Mpika Chai na Cheka tumeshapeleka nguzo. Kwa hiyo, wananchi wataendelea kuunganishiwa umeme kama kawaida. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na miradi mingine ya Jimbo la Kigamboni, ni kweli kabisa tulipeleka miradi ya REA katika vijiji viwili Kigamboni kwa sababu Kigamboni kimsingi ni mitaa kwa sababu ipo Jijini Dar es Salaam, lakini tulipeleka mradi wa REA Kisarawe II kwenye eneo la Cheka pamoja na Kimbiji. Tuna mradi mwingine ambao upo chini ya TANESCO na umeshaanza ambao utapeleka umeme kwenye vijiji vya Mheshimiwa Ndugulile. Vijiji ambavyo vitapelekewa umeme ni pamoja ni Changanyikeni, Gezaulole pamoja na maeneo yote ya Dege.
Sambamba na hilo, tumepeleka mradi mwingine, kule Kigamboni kulikuwa na transfoma moja yenye uwezo wa MW 5 tu, sasa tumeing’oa tumeweka yenye MW 100 ambayo itapeleka umeme kwenye vijiji vyote vya Kigamboni. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nimpe tu faraja mhesimiwa Mbunge wa Kigamboni kwamba matatizo ya umeme Kigamboni sasa yanaelekea kuisha. Utekelezaji wa REA umeshaanza tangu Juni, 2017 na utakamilika Machi, 2019.(Makofi)

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Wilaya ya Kigamboni ina uwekezaji mkubwa katika sekta ya nyumba na viwanda, mahitaji ya umeme kwa sasa ni zaidi MW 20; lakini ni MW 8 tu zinazopatikana, nao umekuwa ukikatika mara kwa mara kutokana na mahitaji makubwa pamoja na uchakavu wa miundombinu ya umeme. (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha Kigamboni inapatikana umeme wa uhakika? (b) Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha kupoozea umeme (substation) katika Wilaya ya Kigamboni kutokana na mahitaji makubwa ya umeme?

Supplementary Question 2

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba na mimi nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, umeme wa REA unatarajiwa kuwa
ni tegemeo kubwa sana kwa wananchi, lakini pia kuinua uchumi kwa ajili ya viwanda vidogo vidogo, lakini Kaliua umeme wa REA umekuwa unakatika mara kwa mara, Mheshimiwa Waziri nimeshakuja kwako mara nyingi tu kuhusiana na suala hili. Kwa siku zaidi ya masaa nane, masaa manne unawaka, masaa nane hauwaki, kwa hiyo lile tegemeo halipo tena kwa wananchi wale. Mheshimiwa Waziri aliahidi kujenga substation pale Kaliua alivyotembelea mwaka 2015.
Naomba kujua sasa Serikali ina mpango mkakati gani kuhakikisha kwamba inajenga substation pale Kaliua ili umeme wa REA uweze kuwa na tija na kuinua uchumi wa wanachi wa Kaliua? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa, Mheshimiwa Sakaya nilipokuja kwako nilitembea na wewe sana na naomba niendelee kutembea na wewe nikija tena. Lakini pia … (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, ni kweli alivyosema Mheshimiwa Mbunge, umeme unaosafiri kwenda Kaliua ni ule unaotoka Tabora - Urambo, - Kaliua hadi Uvinza, kwa hiyo, ni umbali mrefu sana. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Mbunge anavyosema, transfoma ya kusafirisha umeme iliyopo Tabora ndiyo inayohusika kusafirisha umeme katika Majimbo ya Kaliua, Urambo mpaka Uvinza, umbali wa kilometa 372. Mkakati madhubuti wa kumaliza tatizo hili la kukatika kwa umeme ni kuwa Serikali sasa inajenga substation katikati ya Kaliua pamoja na Urambo katika eneo la Gologolo.
Kwa hiyo, utaratibu umeanza na wakati utekelezaji
wa REA utakapoanza basi wananchi watapata umeme huo lakini katika jibu langu litakalofuata kwa swali la msingi nitaeleza kwa upana zaidi lakini nimpe uhakika Mheshimiwa Mbunge utaratibu fedha zimeshatengwa na survey imekamilika na ujenzi utaanza hivi karibuni.

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Wilaya ya Kigamboni ina uwekezaji mkubwa katika sekta ya nyumba na viwanda, mahitaji ya umeme kwa sasa ni zaidi MW 20; lakini ni MW 8 tu zinazopatikana, nao umekuwa ukikatika mara kwa mara kutokana na mahitaji makubwa pamoja na uchakavu wa miundombinu ya umeme. (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha Kigamboni inapatikana umeme wa uhakika? (b) Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha kupoozea umeme (substation) katika Wilaya ya Kigamboni kutokana na mahitaji makubwa ya umeme?

Supplementary Question 3

MHE. DESTERY B. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na hasa niendelee kuanidka Kiswaga. Kwa kuwa swali langu linafanana kabisa na suala hili la Kigamboni, Wilaya ya Magu ambayo ni Jimbo lina vijiji 82, ni vijiji 29 tu vina umeme. Je, vijiji 53 ni lini vitapatiwa umeme ambavyo hata Mheshimiwa Dkt. Kalemani anavifahamu? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimsahihishe kidogo Mheshimiwa Kiswaga, vijiji ambavyo havijapata umeme katika Jimbo la Magu siyo 53 vipo 56. Kwa hiyo, Mheshimiwa Kiswaga tutakupelekea umeme.
Mheshimiwa Spika, niseme tu utekelezaji wa REA Awamu ya Tatu umeshaanza na katika Wilaya yake, maeneo yote yameshafanyiwa survey na Mheshimiwa Mbunge tumeenda naye na tumetembelea maeneo hayo na nimhakikishie vile Vijiji vya Mahala, Igombe, Shishani, Nyasato, Kayera mpaka Mahala vitapatiwa umeme na utekelezaji huo umeshaanza. Nikupe tu uhakika kwamba survey itakamilika tarehe 10 mwezi huu na wakandarasi wataanza kazi rasmi. Kama nilivyosema tuliboresha kwa sababu vile vijiji vyako vitatu vimepelekewa nguzo moja moja kwa hiyo sisi tunahesabu kama vijiji vyote havijapata umeme, kwa hiyo, ni 56 katika Jimbo la Magu.