Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asha Mshimba Jecha

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA aliuliza:- Kituo cha Polisi Dunga kimechakaa sana kwani kuta zake zimepasuka na baadhi ya vyumba havitumiki kutokana na kuhatarisha usalama wa askari na wananchi wanaofika kwa ajili ya kupata huduma. Je, ni lini Serikali itajenga upya kituo hicho?

Supplementary Question 1

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu yenye kutia moyo ya Mheshimiwa Waziri, hivi anafahamu kituo hiki sasa hivi kimefunga huduma zake na wanatoa huduma kwenye jengo la kuazima? Je, ni lini tathmini hii itafanyika ili gharama ijulikane na umuhimu wa kukijenga pia uonekane? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini pia anawahakikishia vipi wananchi wanaotumia kituo hiki umuhimu wa kujengwa na kuweza kukitumia kama walivyozoea? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge, mama yangu Asha, kwa kweli kwa kufuatilia sana suala la kituo hiki. Mbali na swali la hapa amekuwa pia akiulizia mara zote anapopata fursa ya kutembelea ofisini ama kwenye shughuli za Kamati.
Mheshimiwa Spika, niseme tu, kwa umuhimu huo na kwa ufuatiliaji wake, jambo hili tumesema lifanyiwe tathmini kwa upekee kwa maana ya Kituo cha Dunga kama kituo peke yake mbali ya vituo vingine kwenye maeneo mengine ambavyo vinafanana kama kituo hicho.
Mheshimiwa Spika, mara tathmini hiyo itakapokuwa imekamilika ambapo tunaamini ni katika kipindi hikihiki, basi utaratibu wa upatikanaji wa fedha utaanza na hapo ndipo tunaposema tunatoa rai hata kwa wadau mbalimbali ili tuweze kufanya kama ni jambo mahsusi kufuatana na mazingira ya pale.
Mheshimiwa Spika, mara ukarabati wake utakapokamilika basi niwahakikishie wananchi kwamba matumizi yake yatarejea katika hali ya kawaida na wataendelea kumpongeza na kumpigia kura Mheshimiwa Mbunge ambaye amelitetea sana jambo hili. (Makofi)

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA aliuliza:- Kituo cha Polisi Dunga kimechakaa sana kwani kuta zake zimepasuka na baadhi ya vyumba havitumiki kutokana na kuhatarisha usalama wa askari na wananchi wanaofika kwa ajili ya kupata huduma. Je, ni lini Serikali itajenga upya kituo hicho?

Supplementary Question 2

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na nina swali moja tu dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, ni muda mrefu hapa Bungeni Serikali imekuwa ikiahidi kukitengeneza Kituo cha Polisi cha Kengeja ambacho ni kibovu, chakavu na cha zamani ambacho mnasema mlirithi kutoka kwa wakoloni lakini mara nyingi hamkitengenezi na kimekuwa kikihatarisha maisha ya askari na baadhi ya wale wanaowekwa pale kwa muda.
Je, ni lini Serikali hasa itaandaa mazingira ya ziada kuhakikisha mnakikarabati kituo hiki ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nishukuru kwa swali la nyongeza kutoka kwa Mheshimiwa Mjumbe makini wa Kamati inayosimamia Wizara ya Mambo ya Ndani, naye nimhakikishie tu kwamba kikosi chetu kinachosimamia masuala ya ukarabati kitafanyia tathmini pamoja na kituo anachokiongelea.
Mheshimiwa Spika, ni kipaumbele cha Wizara kufanya ukarabati na kukamilisha majengo ya vituo ambavyo vimeshafikia hatua za kuweza kutumika ili vianze kutumika na cha kwake tutaweka umuhimu huo kama alivyohitaji kwenye swali.