Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa walimu madai yao ya kusimamia mtihani wa kidato cha nne mwaka 2015 na mtihani wa kidato cha pili mwaka 2016?

Supplementary Question 1

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa jibu la Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini napenda tu kujua, maana sasa wamesimamia kwa muda mrefu tangu mwaka 2015/2016 ni muda mrefu sasa.
Je, ni lini sasa uhakiki huu utaweza kukamilika ili walimu waweze kulipwa madai yao? (Makofi)
Swali la pili, katika madai hayo, walimu tu Wilaya yetu ya Geita wanadai zaidi ya shilingi milioni 120, napenda pia kujua ni lini walimu hawa wanaotoka Wilaya yangu ya Geita wataweza kulipwa madai yao? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, katika level mbalimbali, mchakato huu wa uhakiki wa deni umeshakamilika. Kwa hiyo, nadhani Hazina sasa hivi wanajipanga, wakati wowote deni hili litaweza kulipwa ili mradi kila mtu haki iweze kupatikana.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo najua Mheshimiwa Bukwimba ni mpiganaji mkubwa sana wa watumishi wake katika jimbo lake, lakini siyo jimbo lake peke yake isipokuwa katika maeneo mbalimbali. Katika eneo la Jimbo lako kwamba lini watalipwa mgao huu wa deni hili ambalo Hazina wanalishughulikia, likilipwa lote litalipwa kwa pamoja.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba tuvute subira kwa sababu Hazina ndiyo walikuwa wanafanya uhakiki wa madeni mbalimbali siyo wa walimu ni mchakato wa kulipa madeni mbalimbali. Jambo hili litakamilika na wananchi wa Busanda kule katika jimbo lako Geita wananchi wa eneo lile watapata hasa hasa watumishi wa Serikali ambao ni walimu watapata madai yao kama ilivyokusudiwa.