Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Chemba?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri na ya uhakika ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Nilikuwa na swali moja tu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya Chemba ni moja kati ya Wilaya kubwa sana katika Mkoa huu wa Dodoma na pengine kwa Tanzania kwa ujumla. Je, Serikali wakati inasubiri kujenga jengo la Mahakama katika Makao Makuuya Wilaya iko tayari sasa kuimarisha mahakama za Mrijo na kwa Mtoro ili kupunguza adha inayowafanya wananchi kutembea zaidi ya kilometa 170 kufuata huduma za mahakama Wilayani Kondoa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli anachokisema Mheshimiwa Mbunge kwamba Wilaya ya Chemba ni kubwa sana, na kwa sababu mahakama hii ya wilaya itaanza kujengwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2018/2019 niseme tu kwamba nimepokea ombi na mawazo ya Mheshimiwa Mbunge na sisi kama Serikali tutaona namna bora ya kuweza kuimarisha huduma katika maeneo ya Mrijo ili wananchi wasipate shida kutembea umbali mrefu kwa sababu alipokusema huko Mheshimiwa Nkamia ni mbali sana mpaka kufika katika makao makuu ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kama Serikali katika mpango wetu wa kuhakikisha kwamba tunasogeza huduma hizi kwa wananchi tutahakikisha pia tunalifanyia kazi jambo hilo la kuboresha huduma za mahakama katika maeneo hayo ili wakati tunaendelea kujipanga katika ujenzi wa Mahakama ya Wilaya wananchi waendelee kupata huduma katika maeneo ya Mrijo na maeneo mengineyo. (Makofi)