Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, katika bajeti ya Serikali 2016/2017 Serikali ilitarajia kuanzisha Vyuo vingine vya ufundi ikiwemo Nyang’hwale?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwa kuwa swali langu lilikuwa la Wilaya ya Nyang’hwale na nimejibiwa kimkoa, Nyang’hwale imeshajipanga tayari na imetenga maeneo ya kuweza kujenga Chuo cha Ufundi. Je, Serikali imeshaweka ndani ya mpango 2018/2019 mpango huu wa kujenga VETA katika Wilaya ya Nyang’hwale?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Serikali huwa mipango yake inaenda taratibu na Nyang’hwale ina vijana wengi ambao hawana ujuzi. Je, Serikali iko tayari kuchukua angalau vijana 50 na kuwapeleka katika maeneo mengine mbalimbali nchini kwenda kujifunza ujuzi?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Spika, kuhusu kama katika bajeti ya mwaka 2017/2018 tumetenga fedha kwa ajili ya kujenga Chuo cha VETA Nyang’hwale; nimweleze Mheshimiwa Mbunge kwamba tunajitahidi kutenga fedha kadri tunapopata kwa ajili ya kujenga Vyuo mbalimbali vya VETA. Kwa sasa hakuna fedha ambazo zimetengwa kwa ajili ya Nyang’hwale; lakini nimwahidi tu kwamba kwa sababu mpango wetu ni kuhakikisha Wilaya zote zinakuwa na Vyo vya VETA tutaendelea kupangilia na kutafuta fedha na kujenga kadri inavyowezekana.
Mheshimiwa Spika, kuhusu kama tuko tayari kupeleka vijana 50 kwenye Vyuo vingine nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, kama wao watajipanga kama Wilaya sisi tuko tayari kushirikiana nao kuhakikisha kwamba vijana hao wanapata nafasi katika Vyuo vingine.