Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:- Vijiji 17 pekee kati ya vijiji 64 ndivyo vilivyopata umeme katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki na ni vijiji saba tu vya Ludewa, Mtego wa Simba, Kidugaro, Lung’ala, Mangala na Kinonko vilivyo katika orodha ya kupatiwa umeme katika REA III awamu ya kwanza ya mwaka 2017/2018. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vijiji 47 vilivyosalia?

Supplementary Question 1

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kama Serikali ilivyosema katika jibu lake la msingi kwamba kuna vijiji saba ambavyo umeniongeza kwa hiyo, je, nataka kuvijua vijiji hivi saba ni vipi na ni lini vitaanza kupatiwa umeme?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa, katika Kata ya Mkulazi kuna miradi miwili nya kielelezo inayofanyiwa kazi sasahivi na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli, Kiwanda cha Mkulazi cha Sukari pia na ujenzi wa Bwawa la Kidunda, je, Serikali ina mkakati gani wa kupeleka umeme katika kata hii yenye vijiji vinne na Kijiji cha Kwaba, ambavyo ni vijiji vya Kwaba, Kidunda pamoja na Usungura?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa Mheshimiwa Mgumba nakupongeza sana unavyoshughulikia masuala ya umeme katika Jimbo lako. Tulipokutana Morogoro ulituomba tukuongezee vijiji na tumekuongezea, lakini vijiji alivyotaka tumuongezee Mheshimiwa Mbunge pamoja na kwamba tumeshapeleka umeme katika vijiji vingine vikiwemo vijiji vya Mtego wa Simba pamoja na Kinonko, tunampelekea kwenye vijiji vingine ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameomba.
Mheshimiwa Naibu Spika, na vijiji ambavyo ameomba tumpelekee ni pamoja na Kibuko, Luhorole, Kizinga, Pangawe pamoja na Usungura. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nikupe, kama vijiji ambavyo tumepeleka na vijiji vingine 40 tutakupelekea Mheshimiwa Mbunge, wala hakuna wasiwasi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la pili kwamba ipo miradi ya vielelezo katika maeneo ya Usungura, ni kweli kabisa. Maeneo yale kutajengwa viwana vya sukari, lakini kadhalika kuna bwawa la maj. Kwa hiyo, tumemuongezea mbali na vijiji vingine vile 11 nilivyotaja na wala sio saba, tunaviongezea vijiji vingine vitatu vikijumlisha na Bwawa la Kidunda, ili tupeleke umeme Kidunda, Usungura pamoja na Kwaba. Kwa hiyo, nimpe imani Mheshimiwa Mbunge kwamba vijiji vyote vya Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki vitapatiwa umeme kupitia mradi wa tatu wa REA. (Makofi)

Name

Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:- Vijiji 17 pekee kati ya vijiji 64 ndivyo vilivyopata umeme katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki na ni vijiji saba tu vya Ludewa, Mtego wa Simba, Kidugaro, Lung’ala, Mangala na Kinonko vilivyo katika orodha ya kupatiwa umeme katika REA III awamu ya kwanza ya mwaka 2017/2018. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vijiji 47 vilivyosalia?

Supplementary Question 2

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana kwa kupata fursa hii. Kama alivyouliza Mheshimiwa Mgumba, majimbo ya vijijini yana matatizo makubwa sana ya umeme hasa katika center za Kata ya Mpwayungu, Kata ya N’ninyi, Manzase na Makao Makuu ya Kata ya Muungano ambako hakuna umeme kabisa. Sasa je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika maeneo haya hususan katika Kata ya Muungano? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa katika Jimbo la Mtera tunapeleka umeme katika vijiji (a) Katika maeneo aliyoyataja kimsingi nimhakikishie Mheshimiwa Lusinde kwamba katika maeneo ya Manzese, Muungano, Mpwayungu pamoja na eneo ambalo hujalitaja linaitwa N’ninyi wanaanza Ijumaa inayokuja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nichukue nafasi hii kumueleza Mheshimiwa Mbunge. Nichukue nafasi hii kwa sababu Waheshimiwa wengi wamesimama, kuwaeleza rasmi Waheshimiwa Wabunge kwamba kuanzia tarehe 20 mwezi huu wakandarasi wote katika mikoa 21 tuliyosaini mikataba wanaanza kazi rasmi ya ujenzi wa mradi wa REA Awamu ya Tatu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mikoa miwili ya Katavi pamoja na Kigoma, taratibu tunazikalimisha wiki ijayo na mwanzoni mwa mwezi Desemba wanaanza ujenzi katika mikoa hiyo miwili. (Makofi)

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:- Vijiji 17 pekee kati ya vijiji 64 ndivyo vilivyopata umeme katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki na ni vijiji saba tu vya Ludewa, Mtego wa Simba, Kidugaro, Lung’ala, Mangala na Kinonko vilivyo katika orodha ya kupatiwa umeme katika REA III awamu ya kwanza ya mwaka 2017/2018. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vijiji 47 vilivyosalia?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA S. MWAIFUGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Tatizo lililopo Morogoro Kusini Mashariki ni tatizo ambalo linafanana na Jimbo la Tabora Manispaa katika Kata 11 za vijijini ambapo mpaka sasa hazijaanza kupelekewa umeme wa REA III. Je, ni lini Serikali itaanza utaratibu huo? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwanza mkandarasi yupo Tabora na ameshakamilisha kazi ya survey na wiki iliyopita amekamilisha Igunga. Kwa hiyo, nimuambie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama nilivyosema tarehe 20 na bahati nzuri tunaanza kuwakagua ujenzi wa wakandarasi kuanzia Tabora na Dodoma.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mkandarasi atakuwa site kuanzia tarehe 20 baada ya kumaliza Igunga na ataendelea na ujenzi wa vijiji vyote 16 katika Mkoa wa Tabora. (Makofi)

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:- Vijiji 17 pekee kati ya vijiji 64 ndivyo vilivyopata umeme katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki na ni vijiji saba tu vya Ludewa, Mtego wa Simba, Kidugaro, Lung’ala, Mangala na Kinonko vilivyo katika orodha ya kupatiwa umeme katika REA III awamu ya kwanza ya mwaka 2017/2018. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vijiji 47 vilivyosalia?

Supplementary Question 4

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo hili la Morogoro Kusini linafanana kabisa na Jimbo la Mtwara Mjini ambako umeme unatoka pale lakini bado kuna vijiji vingi kwa mfano Naulongo, Mkunjanguo, Namayanga na Mawala Chini kule kote mtandao wa umeme haujafika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa nimemweleza Mheshimiwa Waziri mara nyingi sana, je, yupo tayari hivii sasa kutoa kauli ya mwisho kwamba ni lini mtandao wa umeme utapita kwenye vijiji hivi nilivyovitaja? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa kama alivyosema, wiki mbili zilizopita nilikuwa Mtwara kushughulikia tatizo la umeme kukatika katika. Nilipita katika vijiji 16 na bahati nzuri vijiji vingine alivyosema Mheshimiwa Maftaha hivi leo mkandarasi yupo kule. Kwa hiyo, wakandarasi wameshaanza kazi Mheshimiwa Mbunge, asante sana. (Makofi)