Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika Jimbo la Tunduru Kusini kuna vituo vitatu vya afya ambapo Kituo cha Afya Mtina kina zaidi ya miaka 30 hakijafanyiwa ukarabati na pia hakuna wodi ya wazazi. Je, ni lini Serikali itajenga wodi ya wazazi katika kituo hicho na kufanya ukarabati ili kiweze kutoa huduma bora kwa wakazi wa Kata za Nasya, Semeni, Nyerere, Angalia na wakazi wa Kata ya Mchesi, Vijiji vya Likumbula, Tuwemacho na Namasakata?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, asante na Mheshimiwa Naibu Waziri asante kwa majibu mazuri. Kwa kuwa kituo hiki kinahudumia zaidi ya Kata Tano, Kata ya Mtina, Lukumbulem Mchesi, Masakata na Tuwemacho.
Je, ni lini sasa Serikali itaona umuhimu wa kuboresha kituo hiki ili kiweze kutoa huduma za upasuaji kwa wakina mama na wajawazito?
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kampeni ya mwaka 2010 Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga kituo cha afya katika Kata mbili za Nalase ambazo zipo katika Mji mmoja na Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru imekuwa inatenga kila mwaka na mpaka sasa imeishia kujenga msingi tu. Je, ni lini Serikali itaona haja ya kutimiza ahadi ile ya Rais wa Awamu ya Nne ili wapate kituo cha afya pale Nalasi? Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba uniruhusu nimpongeze kwa dhati jinsi ambavyo Mheshimiwa Mpakate anapigania kuhakikisha kwamba wananchi wake wanapata huduma ya afya iliyo bora. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali la kwanza ameuliza lini, na unaweza ukaona nia njema ya Serikali jinsi ambavyo inahakikisha huduma ya afya inapatikana na hasa katika ujenzi wa vituo vya afya katika kata husika. Hii ndio maana katika Halmashauri yake tumeanza na hiyo Kata ya kwanza na hiyo kata nyingine kwa kadri pesa itakavyopatikana. Nia njema ya Serikali ni kuhakikisha vituo vya afya vinajengwa katika kata zote.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili, ni kweli kwamba kuna ahadi iliyotolewa na aliyekuwa Rais wa Awamu ya Nne kwamba vingejengwa vituo vya afya katika kata mbili alizozitaja na yeye mwenyewe amekiri kwamba katika hizo kata mbili kazi ambayo imefanyika mpaka sasa hivi ni ujenzi wa msingi. Naomba nimuombe Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana na wananchi aendelee kuwahimiza ujenzi sio msingi tu, hebu waendelee kujenga mpaka kufikia usawa wa lenta na Serikali itaenda kumalizia ujenzi huo.

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika Jimbo la Tunduru Kusini kuna vituo vitatu vya afya ambapo Kituo cha Afya Mtina kina zaidi ya miaka 30 hakijafanyiwa ukarabati na pia hakuna wodi ya wazazi. Je, ni lini Serikali itajenga wodi ya wazazi katika kituo hicho na kufanya ukarabati ili kiweze kutoa huduma bora kwa wakazi wa Kata za Nasya, Semeni, Nyerere, Angalia na wakazi wa Kata ya Mchesi, Vijiji vya Likumbula, Tuwemacho na Namasakata?

Supplementary Question 2

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, Wilaya ya Karatu ina zaidi ya umri wa miaka 20 na haina hospitali ya wilaya. Hivi sasa uongozi wa wilaya unakamilisha taratibu za kupata eneo kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo. Je, Serikali iko tayari sasa kuanza kutenga fedha katika bajeti inayokuja ili kuanza ujenzi wa hospitali hiyo? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba Serikali iko tayari kuanza kutenga, nia na azma ya Serikali ni kuhakikisha kwamba ujenzi wa Hospitali za Wilaya unafanyika katika Wilaya 64 zote ambazo hatuna hospitali za Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kama ambavyo yeye mwenyewe amesema katika swali lake, ndiyo wameanza kutenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Naomba tuongeze kasi ya kutenga hilo eneo, lakini pia kutokana na Halmashauri yenyewe kwa sababu ni hitaji letu, tuanze kutenga pesa na Serikali ije kumalizia.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika Jimbo la Tunduru Kusini kuna vituo vitatu vya afya ambapo Kituo cha Afya Mtina kina zaidi ya miaka 30 hakijafanyiwa ukarabati na pia hakuna wodi ya wazazi. Je, ni lini Serikali itajenga wodi ya wazazi katika kituo hicho na kufanya ukarabati ili kiweze kutoa huduma bora kwa wakazi wa Kata za Nasya, Semeni, Nyerere, Angalia na wakazi wa Kata ya Mchesi, Vijiji vya Likumbula, Tuwemacho na Namasakata?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru kwa kunipa nafasi hii, kwa kuwa Kituo cha Afya cha Mwese ni cha muda mrefu sana, kina zaidi ya miaka 40 hakijafanyiwa ukarabati wa aina yoyote na Serikali iliahidi kukikarabati kituo hicho. Je, Serikali ni lini itapeleka fedha kwa ajili ya kituo hicho ili kiweze kuwasaidia wananchi wa Kata hiyo ya Mwese?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na Kituo cha Afya Mwese ambacho ni cha muda mrefu, je, ni lini Serikali itakuwa tayari kutenga pesa ili kufanya ukarabati?
Mheshimiwa Naibu Spika, utakubaliana kwamba ni kiu ya Waheshimiwa Wabunge wengi wangependa vituo vya afya viweze kukarabatiwa, na ndiyo maana Serikali kwa kujua umuhimu huo tumeanza na vituo vya afya 205, si haba. Naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira awamu kwa awamu na kwa kasi tunayoenda nayo naamini muda si mrefu na kituo cha afya cha kwake kitapata fedha.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika Jimbo la Tunduru Kusini kuna vituo vitatu vya afya ambapo Kituo cha Afya Mtina kina zaidi ya miaka 30 hakijafanyiwa ukarabati na pia hakuna wodi ya wazazi. Je, ni lini Serikali itajenga wodi ya wazazi katika kituo hicho na kufanya ukarabati ili kiweze kutoa huduma bora kwa wakazi wa Kata za Nasya, Semeni, Nyerere, Angalia na wakazi wa Kata ya Mchesi, Vijiji vya Likumbula, Tuwemacho na Namasakata?

Supplementary Question 4

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, Serikali imesema kwamba itakarabati vituo 205 kikiwemo pia na Kituo cha Afya cha Malya, ninapenda kujua Mheshimiwa Waziri, ni formula gani mnayotumia kupelekwa kwa baadhi ya vituo vya afya shilingi milioni 500 na vingine milioni 400 wakati mlichagua kwamba vituo vyote 205 vikarabatiwe kwa pamoja. Ni formula gani mnayotumia? Lakini ni lini pesa zingine ambazo mliahidi kwamba mtapeleka shilingi milioni 500 kwa kila kituo, kwa nini 400 na kwa nini 500? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni formula gani ambayo inatumika katika kupeleka kupeleka fedha katika vituo vya afya sehemu nyingine milioni 500 sehemu nyingine milioni 400?
Mheshimiwa Naibu Spika, formula zipo nyingi, kwanza ya kwanza inategemea na source of funding, ni nani ambaye ameleta fedha ili ziweze kwenda kwenye kituo cha afya. Lakini pia formula nyingine ni namna ambavyo ukarabati unaohitajika, kuna baadhi ya maeneo ni majengo machache tu ndiyo ambayo yanaongezwa kiasi kwamba ikipelekwa shilingi milioni 400 inatosha kabisa kuweza kufanya ujenzi ule ukakamilika. Kwa hiyo, inategemea source lakini pia na ukarabati ni kwa kiasi gani unakwenda kufanyika katika eneo husika.