Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO (K.n.y. MHE. JUMA S. NKAMIA) aliuliza:- Wilaya ya Chemba haina hospitali jambo linalowalazimu wananchi wake zaidi ya laki tatu kwenda kupata huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Kondoa. Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuhakikisha Wilaya hiyo inapata hospitali?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru sana kwa majibu ya Serikali ambayo yana matumaini ya ujenzi ya Hospitali ya Wilaya.
Swali la kwanza, kwa kuwa Serikali iliahidi na mipango yake inachukua muda mrefu, je, Serikali ina mpango gani wakati inajipanga kuweza kukiboresha kituo cha afya cha Hamai ili kiweze kutoa huduma nzuri sambamba na kuchimba kisima ambacho ni tatizo kwenye eneo la kituo hicho cha afya?
Swali la pili, kwa kuwa matatizo ya Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ni sawa na tatizo lililoko kwenye Wilaya ya Tanganyika na Naibu Waziri analifahamu hili. Serikali iliahidi kujenga kituo cha afya Majalila. Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga kituo hicho cha Majalila?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika Halmashauri ya Chemba tunao huu mpango wa kuhakikisha tunajenga Hospitali ya Wilaya. Kwa vile changamoto ya Jimbo la Chemba ni kubwa ndiyo maana Serikali katika mpango wake wa kuboresha vile vituo vya afya 100, kituo cha afya cha Hamai ni miongoni mwa vituo vya afya ambacho tunaenda kukiwekea ufanisi mkubwa wa ujenzi wa miundombinu ambapo imani yangu ni kwamba si muda mrefu mchakato huo utaanza.
Kwa hiyo, naomba nikuhakikishie kwamba kwa wananchi wa Chemba na hili tumeshaongea na Mheshimiwa Nkamia kwamba tutafanya kila liwezekanalo katika kipindi kifupi kijacho tutaenda kukiboresha kile kituo cha afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la Wilaya ya Tanganyika Mheshimiwa Mbunge unafahamu tulikuwa wote Tanganyika nilivyokuja Jimboni kwako. Tulitembelea Makao Makuu yako na Wilaya yako ya Tanganyika ambayo ni mpya, ndiyo maana tumepanga katika mpango wa kuboresha Wilaya hii katika eneo la Majalila kile kituo cha afya ambacho kinasuasua sana tutamekiingiza katika mpango wa vituo vya afya 100.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba nikuhakikishe kwamba wananchi wa Tanganyika wawe na imani kwamba Serikali inaenda kufanya investment kubwa eneo lile ili wananchi wa Tanganyika wapate huduma nzuri za afya.

Name

Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO (K.n.y. MHE. JUMA S. NKAMIA) aliuliza:- Wilaya ya Chemba haina hospitali jambo linalowalazimu wananchi wake zaidi ya laki tatu kwenda kupata huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Kondoa. Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuhakikisha Wilaya hiyo inapata hospitali?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, kwa kuniona.
Matatizo yanayowakabili wananchi wa Wilaya Chemba kwa kukosa huduma za Hospitali za Wilaya yanalingana kabisa na ya Wilaya ya Malinyi ambapo wananchi hawana Hospitali ya Wilaya. Halmashauri ya Malinyi imeweka utaratibu kuomba TAMISEMI kuifanya Hospitali ya Lugala ambayo inamilikiwa na taasisi ya kidini kuwa Hospitali ya Wilaya, lakini ombi hilo na utaratibu huu TAMISEMI wamesimamisha.
Je, Serikali ina utaratibu gani wa haraka wa kuwasaidia wananchi wa Wilaya ya Malinyi kupata hospitali ya Wilaya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ukiangalia Ulanga, Malinyi wana changamoto kubwa ya sekta ya afya. Katika mpango wa haraka Mheshimiwa Mponda, naomba nikuhakikishie kwamba kuna kituo cha afya cha Mtimila ambacho tumekiwekea kipaumbele tunakuja kukiwekea miundombinu muda si mrefu, kuanzia huu mwezi wa sita kwenda mwezi wa saba inawezekana mchakato huo utaanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwahakikishe wananchi wa Malinyi kwamba Serikali imewaona, tutaenda kufanya kazi kubwa pale ambayo mtakuja kuona ikifika mwezi wa nane hapo Mungu akijalia, inawezekana hali ikawa ni tofauti wananchi watakwenda kupata huduma nzuri sawa sawa na kituo cha afya cha Lupilo katika Jimbo la Ulanga (Makofi)

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO (K.n.y. MHE. JUMA S. NKAMIA) aliuliza:- Wilaya ya Chemba haina hospitali jambo linalowalazimu wananchi wake zaidi ya laki tatu kwenda kupata huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Kondoa. Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuhakikisha Wilaya hiyo inapata hospitali?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuwa hii hospitali ya Wilaya ya Kondoa inahudumia Halmashauri tatu; na kwa kuwa imepata ufinyu mdogo sana wa bajeti na kuleta changamoto katika madawa na vifaa tiba. Sasa Serikali inaona lini wakati inafikiria kuwapatia watu wa Chemba hospitali yao, hospitali hii ikaongezewa bajeti ili kuweza kuhudumia vyema Wilaya hizi tatu? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Kondoa changamoto ni kubwa na ndiyo maana ukiangalia kuna Majimbo matatu tofauti ambayo ni Chemba, Kondoa Vijijini na Kondoa Mjini lakini hospitali inayotumika sasa hivi ni Hospitali ile ya Kondoa na ukiangalia population mpaka watu wengine kutoka katika wilaya especially kama Wilaya ya Hanang’ walioko mpakani wengine wanakuja hapa Kondoa.
Kwa hiyo, jambo hili ni kubwa na tumeliona ndiyo maana katika mpango wetu wa bajeti wa mwaka huu sasa hasa ukiangalia basket fund tumebadilisha utaratibu wa basket fund tumeongeza bajeti katika eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu ni kuangalia ni jinsi gani tutafanya ili wananchi wapate huduma. Hata hivyo tumetoa maelekezo maeneo mbalimbali, kwa mfano tuna Halmashauri ya Kondoa Mji na Halmashauri ya Kondoa Vijijini lakini hospitali ni moja. Nimewahitaji Wakurugenzi wa maeneo yale waangalie katika suala zima la basket fund katika Halmashauri ambapo ile hospitali iko na jinsi gani kufanya kwa kuweka utaratibu wa kusaidia ile hospitali angalau kwa hali ya sasa iweze kufanya vizuri kwa sababu wananchi wote wanaohudumiwa ni watu kutoka maeneo hayo ambapo ni hospitali yetu lazima tutakuja kuweka nguvu wananchi wapate huduma nzuri. Kwa hiyo, nikushukuru sana Serikali inaifanyia kazi jambo hili.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nataka kuongeza kwenye swali la Mheshimiwa Sware.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kugawanya fedha kwa ajili ya dawa, vifaa na vifaa tiba tunazingatia vigezo vikuu vitatu. Kigezo cha kwanza ni idadi ya walengwa wanaopewa huduma katika hospitali hiyo (service population) ambapo inachukua asilimia 70, kigezo cha pili ni hali ya umaskini katika eneo husika ambacho kinabeba asilimia 15 na kigezo cha tatu ni hali ya vifo vya watoto chini ya miaka mitano. Kwa hiyo, nilikuwa namuomba Mheshimiwa Sware Halmashauri hizi tatu ambazo zinatumia Hospitali ya Wilaya ya Kondoa wakae pamoja watuletee mapendekezo yao Wizara ya Afya kwamba hospitali hii inahudumia Halmashauri tatu na sisi tutazingatia katika kuwaongezea bajeti ya dawa. Ninakushukuru sana. (Makofi)

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO (K.n.y. MHE. JUMA S. NKAMIA) aliuliza:- Wilaya ya Chemba haina hospitali jambo linalowalazimu wananchi wake zaidi ya laki tatu kwenda kupata huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Kondoa. Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuhakikisha Wilaya hiyo inapata hospitali?

Supplementary Question 4

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, asante kwa kuwa swali la msingi linafanana kabisa na Wilaya mpya za Mkalama pamoja na Ikungi na wanatimiza vigezo vyote ambavyo Waziri amevitaja hapa.
Je, Serikali ni lini sasa italeta huduma za hospitali za Wilaya katika Wilaya hizo za Mkalama na Ikungi? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mkalama ni Halmashauri mpya na imegawanyika kutoka Halmashauri ya Iramba, tunaenda kuhakikisha tunaboresha kile kituo cha afya cha Inimbila kwa sasa lengo kubwa ni kwamba kiweze kuwa na suala zima la upasuaji kuondoa haya mambo ya referral system, ambapo tunajua kwamba jambo hili tukilifanya litasaidia sana wananchi wa Jimbo la Mkalama kuweza kupata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, hali kadhalika katika kituo cha afya cha Ikungi tunaenda kuweka uboreshaji mkubwa wa miundombinu ya afya ambayo kwa wananchi wa eneo lile wataweza kupata huduma mzuri hivi sasa ambapo kama nilivyosema awali tumeingiza katika mpango ule wa vituo vya afya 100 ambao Serikali iko katika hatua za mwisho kwa sababu kila kitu kimeshakamilika, tegemeeni Waheshimwa Wabunge katika maeneo hayo Serikali imewasikia na itafanya mambo hayo kwa kadri iwezekanavyo. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO (K.n.y. MHE. JUMA S. NKAMIA) aliuliza:- Wilaya ya Chemba haina hospitali jambo linalowalazimu wananchi wake zaidi ya laki tatu kwenda kupata huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Kondoa. Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuhakikisha Wilaya hiyo inapata hospitali?

Supplementary Question 5

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri ulifika Babati ukaona hospitali yetu ya Mrara na tukakueleza kwamba tunapata wagonjwa kutoka Kondoa ambalo ndiyo swali la msingi siku ya leo. RCC tulishakaa kwamba hospitali yetu ipandishwe hadhi kutoka kituo cha afya kwenda hospitali ya Wilaya naomba nifahamu Mheshimiwa Naibu Waziri ni lini pendekezo letu hilo la RCC mtalifanyia kazi maana hospitali ya Mrara ina hali mbaya na wagonjwa ni wengi tunashindwa kuwahudumia?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nimefika na Mheshimiwa Mbunge tuliambatana pamoja siku ile tukitembea. Ni kweli wanachangamoto kubwa sana ni kwa vile utaratibu wa upandishaji wa vituo uko kwa mujibu wa sheria na utaratibu ambao ninyi mmeshakamilisha jambo hilo lote na hivi sasa liko Wizara ya Afya katika final stages, nadhani Wizara ya Afya itakapokamilisha hilo jambo mtapata mrejesho, kwa sababu dhamira ya Serikali ni kuwahudumia wananchi wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, kama mambo yote katika Mkoa yamekamilika naamini Wizara ya Afya ita- finalizes hilo jambo lengo kubwa ni kuwasaidia wananchi wa Babati waweze kupata huduma vizuri. (Makofi)