Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Ardhi ya Njombe inahitaji mbolea kwa wingi zaidi kuliko mikoa mingine. Je, Serikali ina mkakati gani wa uanzishaji wa Kiwanda cha Mbolea Mkoani Njombe?

Supplementary Question 1

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza, nina maswali mawili ya nyongeza. La kwanza; kwa kuwa kiwanda cha mbolea hakiwezi kujengwa Njombe kutokana na kutopatikana kwa malighafi; na kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Njombe wanalima mwaka mzima, je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha mbolea inapatikana katika Mkoa wa Njombe kila wakati?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Njombe mwaka jana wamelima kwa wingi mahindi ambayo yamekosa soko na hata mwaka huu bado wamelima mahindi kwa wingi yatakosa soko vile vile. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha inawatafutia soko la uhakika hawa wananchi wa Mkoa wa Njombe?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi Serikali imekuwa ikifanya hivyo kuhakikisha kwamba mbolea inapatikana na si mara moja Waziri wa kilimo amekuwa akitoa taarifa juu ya upelekaji wa mbolea katika maeneo husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili kuhusu suala la masoko ya mahindi; kimsingi nizidi tu kuwakumbusha, ni kwamba Serikali imekuwa ikiendelea kutafuta masoko. Pamoja na kutafuta masoko tunazidi kusisitiza kuhakikisha kwamba mbali ya kuuza mahindi yakiwa ghafi ni vyema kuhakikisha kwamba mahindi hayo kwanza yanatengenezwa kama unga au chakula cha mifugo au kuhakikisha kwamba yameongezwa thamani badala ya kuyasafirisha mahindi ghafi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi ambayo inapenda kusafirisha mali zake zikiwa ghafi kwa kweli si nchi ambayo itaweza kupiga hatua kubwa katika uchumi hususani katika malengo ya nchi, haya ya uchumi huu wa viwanda.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri aliyoyatoa. Niombe tu kuliarifu Bunge kwamba katika muda wa wiki moja ijayo tutafanya semina ya Bunge zima kuwaeleza mchakato mzima wa upatikanaji wa mbolea nchini. Tunatumaini kwamba katika semina hiyo Wabunge sasa tutakuwa tumekuwa na uelewa wa pamoja wa nini Serikali inafanya na kama zipo changamoto, basi hiyo itakuwa fursa nzuri ya kuzijadili ili tuweze kwenda kwa pamoja sawasawa.

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Ardhi ya Njombe inahitaji mbolea kwa wingi zaidi kuliko mikoa mingine. Je, Serikali ina mkakati gani wa uanzishaji wa Kiwanda cha Mbolea Mkoani Njombe?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Sisi Wabunge wa Mkoa wa Njombe kwa ujumla wetu tumekuwa tukilalamika sana juu ya upatikanaji wa mbolea katika mkoa wetu; na wananchi wetu ni wakulima ambao hawatumwi na mtu kwenda kufanya kazi ya kilimo. Je, ni lini sasa TFC watakuwa na godowns za kutosha ili ku-supply mbolea katika Mkoa wa Njombe?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza niwapongeze sana Waheshimiwa Wabunge wa Njombe kwa jitihada kubwa wanayoifanya katika kuhakikisha kwamba Tanzania inakuwa na kilimo kinachotosheleza katika ulishaji wa Taifa na kuweza kuuza nje. TFC imekuwa na maghala karibu katika kila Mkoa na hata sasa bado kuna mazungumzo yanayoendelea ya kuona kwamba pengine iweze kuwa moja kwa moja chini ya Wizara ya Kilimo ili sasa masuala hayo yaende vizuri zaidi.

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Ardhi ya Njombe inahitaji mbolea kwa wingi zaidi kuliko mikoa mingine. Je, Serikali ina mkakati gani wa uanzishaji wa Kiwanda cha Mbolea Mkoani Njombe?

Supplementary Question 3

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mkoa wa Singida unastawisha sana zao la alizeti na wananchi wa Mkoa wa Singida wameelewa sana dhana ya viwanda. Sasa tatizo linakuja kwenye zao la alizeti kwa sababu Serikali haijaweka msisitizo katika kuleta ruzuku ya mbegu ili zao lile lilimwe kwa wingi kukidhi viwanda vinavyojengwa Mkoani Singida. Ahsante.

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inao mkakati mahsusi wa zao la alizeti ambao mkakati huo pamoja na mambo mengine umelenga kwanza kuongeza uzalishaji wa alizeti hapa nchini na usindikaji wa mazao yanayotokana na alizeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati huu kwa kuanzia umeanza kwanza na kuhakikisha kwamba upatikanaji wa mbegu bora za alizeti unakuwa na utoshelevu. Tumeshapata sasa aina nne za alizeti variety mpya ambayo tija (productivity) yake ni kubwa kuliko mbegu hizi ambazo au variety hizi ambazo tumekuwa tunatumia hapa nchini kwa muda mrefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo ni kweli kwamba kwa miaka ya nyuma mbegu ya alizeti ilikuwa haitoshi, mbegu yenye ubora lakini sasa mbegu inayoweza kutoa mafuta megi zaidi na katika kiwango kidogo imeshapatikana, ni variety hizo nne na zitaanza kusambazwa kwa wakulima hapa nchini.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Ardhi ya Njombe inahitaji mbolea kwa wingi zaidi kuliko mikoa mingine. Je, Serikali ina mkakati gani wa uanzishaji wa Kiwanda cha Mbolea Mkoani Njombe?

Supplementary Question 4

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa ujenzi wa Kiwanda cha Mbolea Kilwa ni suala la Ilani ya Uchanguzi wa Chama cha Mapinduzi lakini pia ni ukombozi mkubwa kwa Mikoa ya Lindi na Mtwara na mapinduzi kwa kilimo chetu. Mwaka jana Serikali ilitoa ahadi kwamba mchakato unaendelea vizuri, nataka kujua mchakato huo umefikia wapi kwa sasa.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Wakati najibu swali la msingi kama Mheshimiwa Nape hakunisikiliza vizuri; ni kwamba nilisema tayari kuna wawekezaji ambao wameshaonesha nia wa Makampuni ya HELM na FERROSTAAL wa Ujerumani, kwa hiyo mchakato unaendelea katika mazingira hayo.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Ardhi ya Njombe inahitaji mbolea kwa wingi zaidi kuliko mikoa mingine. Je, Serikali ina mkakati gani wa uanzishaji wa Kiwanda cha Mbolea Mkoani Njombe?

Supplementary Question 5

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa kilichokuwa Kiwanda cha Mbolea cha Tanga kimebinafsishwa na sasa zinaendelea shughuli nyingine pale ambazo hazihusiani na mbolea. Kwa mahitaji haya ambapo bado mbolea inahitajika nchini, je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa wa kukirejesha kiwanda kile ili kiweze kuzalisha mbolea?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimshukuru kwa jinsi ambavyo anafuatilia shughuli zetu za viwanda na kulifanya swali letu kuwa makini katika eneo husika. Niseme tu kwamba ni kweli eneo hilo ambalo lilikuwa Kiwanda cha Mbolea Tanga kimebadilishwa na sasa kinashughulika na shughuli za mafuta.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba lengo la kubinafsisha ilikuwa si tu kwamba lazima kuendeleza kiwanda kile kilichopo hata kama mashine zilizopo zilikuwa hazifai. Kimsingi mashine zile zilikuwa zimezeeka sana na mwekezaji alitoa mapendekezo akaandika umuhimu wa kuwekeza katika mafuta kwa misingi ya kupokea mafuta, kuhifadhi na kusambaza na sasa hivi ana uwezo wa kusambaza mafuta kufikia lita za ujazo milioni 126.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli imekuwa ni mkombozi kwa wananchi na wafanyabiashara wote wa maeneo ya Tanga, Arusha na maeneo ya Kaskazini hata Kigoma. Kwa hiyo, binafsi nampongeza kwa uwekezaji huo kwa sababu lengo letu sisi ni kuongeza tija katika shughuli zote za kiuwekezaji.

Name

Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Ardhi ya Njombe inahitaji mbolea kwa wingi zaidi kuliko mikoa mingine. Je, Serikali ina mkakati gani wa uanzishaji wa Kiwanda cha Mbolea Mkoani Njombe?

Supplementary Question 6

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante Mtemi. Wilaya ya Kakonko mwaka jana ilipata shida kubwa ya mbolea mpaka nikadiriki kumpigia Waziri wa Kilimo juu ya ukosefu wa mbolea katika Wilaya ya Kakonko. Tatizo hili lilitokana na wale suppliers ambao hawakuwa na uwezo kabisa wa kununua mbolea na kuiuza kwa bei elekezi kwa sababu ilikuwa inatoka mbali. Nataka Waziri, tena bila kumumunya maneno, anihakikishie kama wananchi wa Kakonko watapata mbolea mwaka huu bila usumbufu? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na kwa niaba ya Waziri Wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, naomba tu nimhakikishie rafiki yangu Mheshimiwa Kasuku Bilago kwamba mfumo huu ambao tunataka kuwasiminisha Wabunge wote utampa huo uhakika anaoutaka. Naomba nimhakikishie kwamba mbolea itapatikana kwa wakati wote nchini.