Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:- Wabunge wa Viti Maalum ni sawa na Wabunge wengine wa Majimbo kwa sababu hakuna tofauti ya kiapo cha Wabunge wa Majimbo na wale wa Viti Maalum. Je, ni kwa nini Wabunge wa Viti Maalum hawaingii kwenye Vikao vya Kamati ya Fedha za Halmashauri zao?

Supplementary Question 1

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum ni Wabunge sawa na Wabunge wa Majimbo, hivyo basi, Serikali haioni kwamba kuwanyima Wabunge wa Viti Maalum kuhudhuria kwenye Kamati za Fedha inawasababisha wasielewe mipango ya fedha kwenye Halmashauri zao? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni kwa nini basi hii sheria isiletwe humu Bungeni ikabadilishwa ili kuweka usawa na kuondoa ubaguzi wa jinsia kwa sababu kutomruhusu Mbunge wa Viti Maalum kuingia kwenye Kamati za Fedha ni ubaguzi wa jinsia ya mwanamke na mwanaume ambayo inaanzia kwenye sheria zetu za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza, ni kweli kama alivyosema ni vigumu sana kujua kwa kina yale ambayo yamejadiliwa na kikao husika kama wewe siyo Mjumbe. Hiyo ni kweli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili kuhusu kwa nini Serikali isilete Bungeni marekebisho ya sheria ili kusudi Wabunge wa Viti Maalum wawe Wajumbe, naomba tu nilipokee hili sasa kwa niaba ya Serikali ili tukalizungumze ndani ya Serikali kwa kuwa Vyama vya Siasa ambavyo viliwateua Wabunge wa Viti Maalum na kila Mbunge wa Viti Maalum amepangiwa Halmashauri fulani ya kuhudhuria vikao na kupiga kura. Basi nadhani hiyo inaweza ikawa ni mwanzo mzuri wa kuangalia ni namna gani tuweze kuleta marekebisho ya hiyo sheria. (Makofi)

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:- Wabunge wa Viti Maalum ni sawa na Wabunge wengine wa Majimbo kwa sababu hakuna tofauti ya kiapo cha Wabunge wa Majimbo na wale wa Viti Maalum. Je, ni kwa nini Wabunge wa Viti Maalum hawaingii kwenye Vikao vya Kamati ya Fedha za Halmashauri zao?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum wamekuwa na majukumu makubwa sana ndani ya mikoa yao; je, ni lini sasa Serikali itaanza kuwapatia Wabunge wa Viti Maalum Mifuko ya Jimbo kama walivyo Wabunge wa Majimbo? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli mapendekezo yamekuwepo mengi nje na ndani ya Bunge kuhusu Wabunge wa Viti Maalum nao kupewa sehemu ya fedha kama Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa maelekezo yaliyoko kwenye sheria hiyo, mpaka sasa hivi bado Wabunge wa Viti Maalum hawajaingizwa kwenye huo mfumo. Sasa kwa sababu ni pendekezo ambalo linahitaji majadiliano ya awali ndani ya Serikali kwanza, naomba nalo nilichukue.

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:- Wabunge wa Viti Maalum ni sawa na Wabunge wengine wa Majimbo kwa sababu hakuna tofauti ya kiapo cha Wabunge wa Majimbo na wale wa Viti Maalum. Je, ni kwa nini Wabunge wa Viti Maalum hawaingii kwenye Vikao vya Kamati ya Fedha za Halmashauri zao?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Wabunge wa Viti Maalum uwakilishi wao uko kimkoa, lakini sasa Wabunge hawa wa Viti Maalum wamekuwa wakipata changamoto nyingi katika kutekeleza majukumu yao ya Kibunge hususan katika kufanya mikutano ya hadhara. Sasa ni nini kauli ya Serikali katika hili? Ahsante. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la mikutano ya hadhara linahusisha idara nyingi, ikiwemo Idara ya Polisi ambayo iko chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu kwamba kama kuna mawasiliano mazuri kati ya Wabunge wa Viti Maalum na mamlaka zinazohusika, wakiwemo Wabunge wa Majimbo, hakuna matatizo yoyote. Inawezekana ukaandaliwa mkutano, hasa Mbunge wa Jimbo anaweza akaandaa mkutano ambao vilevile utahutubiwa na Mbunge wa Viti Maalum kwenye eneo lake. (Makofi)