Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

CAN.RTD Ali Khamis Masoud

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mfenesini

Primary Question

MHE. KANALI MST. MASOUD ALI KHAMIS (K.n.y. MHE. IBRAHIM HASSANALI MOHAMMEDALI) aliuliza:- Jiji la Dar es Salaam linakabiliwa na tatizo la ombaomba wengi na katika baadhi ya maeneo wamejenga miundombinu ya kulala. Je, ni lini Serikali itachukua hatua ya kuwaondoa ombaomba katika Jiji la Dar es Salaam?

Supplementary Question 1

MHE. KANALI MST. MASOUD ALI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, tatizo la ombaomba lina muda mrefu na limekuwa likishughulikiwa na Serikali na likiulizwa mara kwa mara lakini bado ombaomba wanaonekana wakirudi mitaani. Je, ni hatua gani madhuhuti sasa Serikali imeziweka ili hao ombaomba wasirudi tena?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni kweli kama alivyosema Naibu Waziri, wakamatwe na washtakiwe, lakini je, hawa hawafanyi kwa makusudi, wanafanya kutokana na hali ngumu ya maisha. Je, wanapotoka huko gerezani baada ya kuwafunga na vitu vingine, hatua gani za Serikali zinachukuliwa kuwasaidia kimaisha?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, hatua ambazo Serikali inazichukua ni kutoa fursa kwa wananchi wote ili waweze kuzitumia kwa ajili ya kujikomboa kiuchumi na kupambana na umaskini. Hatua hizo nimezitaja kwenye jibu la msingi kama vile kutoa fursa mbalimbali za mikopo, kuwepo kwa ardhi ya kutosha yenye rutuba na vilevile kuwa na programu nyingi za kuboresha huduma mbalimbali katika maeneo ya vijijini ili watu wasitoke vijijini wakaja mijini kufuata huduma hizo. Kwa hiyo, hiyo ni mojawapo ya hatua madhubuti lakini hii hatua ya kuwakamata na kuwarudisha makwao imeonekana ni kama vile haisaidii sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la pili, hali ya maisha ni ngumu ni kweli na ndiyo maana nimesema kwamba tutumie hizo fursa. Kwa kusema ukweli fursa ya Elimu Msingi Bila Malipo ni muhimu sana tuifuatilie vizuri ili watoto wetu wote ambao wanastahili kuwa shuleni wawe shuleni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombaomba wengi wamekuwa wanatumia watoto ambao wanatakiwa kuwa shuleni na wanazagaa hovyo mitaani, ndiyo maana nikatoa wito kwamba Sheria ile ya Elimu na Kanuni ya Adhabu itumike kikamilifu katika kuhakikisha kwanza watoto wote warudishwe shuleni na vilevile wazazi ambao hawatekelezi wajibu wao nao vilevile wachukuliwe hatua za kisheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hali ngumu ya maisha, fursa ziko nyingi, naomba sana zitumike ili kujikomboa na hali ngumu ya maisha.

Name

Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. KANALI MST. MASOUD ALI KHAMIS (K.n.y. MHE. IBRAHIM HASSANALI MOHAMMEDALI) aliuliza:- Jiji la Dar es Salaam linakabiliwa na tatizo la ombaomba wengi na katika baadhi ya maeneo wamejenga miundombinu ya kulala. Je, ni lini Serikali itachukua hatua ya kuwaondoa ombaomba katika Jiji la Dar es Salaam?

Supplementary Question 2

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, amezungumza kwamba sababu nyingine inayochangia ni pamoja na imani za kidini na hali ngumu ya maisha. Ni kwa nini sasa Serikali isichukue jukumu la makusudi, kwa sababu tatizo la ombaomba kwa watu wengi ni mindset, la kuelimisha jamii kwa vipindi mbalimbali vya redio na television kuhakikisha tunabadilisha mtazamo kusudi hawa watu kama ni imani za kidini waende kwenye imani wanazoziamini wakapate misaada huko badala ya kuwa barabarani?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wake ni mzuri na yeye ni kiongozi wa dini. Nadhani sababu mojawapo ya kuwepo kwa ombaomba wengi kama nilivyosema kwenye jibu la msingi ni kwamba watu wengine wanatoa misaada kama sehemu ya ibada. Ndiyo maana unakuta ombaomba wengi siku kama za Ijumaa na Jumapili wanakuwa wengi zaidi katika maeneo hayo ambayo ni ya ibada ni kwa sababu watu wengine wanatoa fedha kama misaada. Kwa hiyo, kwa kweli kama ushauri wake ulivyotolewa tunauchukua kwa ajili ya kuupangia bajeti ya kutoa elimu kwa umma ili kusudi kupunguza hili tatizo la ombaomba.

Name

Saada Salum Mkuya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Welezo

Primary Question

MHE. KANALI MST. MASOUD ALI KHAMIS (K.n.y. MHE. IBRAHIM HASSANALI MOHAMMEDALI) aliuliza:- Jiji la Dar es Salaam linakabiliwa na tatizo la ombaomba wengi na katika baadhi ya maeneo wamejenga miundombinu ya kulala. Je, ni lini Serikali itachukua hatua ya kuwaondoa ombaomba katika Jiji la Dar es Salaam?

Supplementary Question 3

MHE. SAADA MKUYA SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mheshimiwa Naibu Waziri katika majibu yake ya msingi fursa ambazo amezionesha ni pamoja na mikopo lakini tunajua kiukweli wale ombaomba hawana asset yoyote na taasisi zetu za kifedha mara nyingi zinahitaji at least uwe na asset au uwe na jambo linguine.
Sasa Serikali haioni umuhimu wa kupanga mkakati maalum specifically kwa ajili ya hawa ombaomba ili waondokane na hii hali waliyokuwanayo rather than ku- generalise wapate mikopo ambayo sio rahisi kiukweli?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama alivyosema kwamba taasisi nyingi za kifedha zinadai collateral ili watu wapate mikopo, lakini kwenye utaratibu wetu wa Serikali kwa mujibu wa Sheria ya Fedha ambayo tumeipitisha mwaka huu hapa Bungeni ni kwamba, mtu atapata mkopo kutokana na shughuli anayofanya. Ndiyo maana nimetoa wito kwamba watumie fursa ya ardhi yenye rutuba kuzalisha mali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama hawa ombaomba watapata elimu nzuri kupitia halmashauri zao, Maafisa Maendeleo ya Jamii watoe elimu hiyo, wakajiunga kwenye vikundi vya uzalishaji mali wanayo fursa ya kupata mikopo kupitia halmashauri, ile 10% ambapo 4% inakwenda kwa vijana 4% inaenda kwa wanawake na 2% inaenda kwa walemavu. Kwa hiyo, hiyo ni fursa mojawapo ambayo ni nzuri ya kupata mkopo bila kuwa na collateral au kuwa na asset yoyote. Jambo la muhimu sana ni Maafisa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii watumike kuelimisha wananchi ili watumie fursa zilizopo.