Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Kata za Gare, Kwai, Kwemashai, Makanya, Kilole, Ngwelo na Ubiri hazikufikiwa na REA III mpaka sasa:- Je, ni lini sasa Serikali itafikisha umeme kwenye kata hizo?

Supplementary Question 1

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu pia niendelee kumpongeza Waziri Kalemani na Naibu pamoja na timu yake kwa kutuma wataalam kuja ku-survey katika Kata za Kwekanga, Mbwei, Migambo, Nguli, Lushoto, Magamba na Mlola.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, je, pamoja na ku-survey kata zote hizo pamoja na alilozitaja, ni lini sasa wananchi wangu watakuja kupimiwa hawa ili waweze kupata umeme kwani umeme ni huduma ambayo walikuwa wanaisubiri kwa muda mrefu sasa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mkandarasi aliyepewa kazi ya kujenga umeme katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto tokea mwaka jana mpaka leo hii amejenga kitongoji kimoja tu ambacho ni cha Magamba Mabughai. Hii inaonyesha uchelewaji mkubwa sana, je, Serikali haioni sasa kuwa kuna haja ya kubadilisha mkandarasi huyu kuweka mkandarasi mwingine ambaye anaendana na kasi ya hapa kazi tu?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Shekilindi anavyofuatilia masuala ya umeme katika Jimbo lake la Lushoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunakubali kupokea pongezi kwa kazi nzuri zinazofanywa na sehemu nyingine ya mkandarasi lakini zipo changamoto kweli kwa mkandarasi na nimeongea na Mheshimiwa Mbunge. Kwanza nilikuwa nimempa vijiji vinne tu kati ya vijiji kumi na mbili, nimpe taarifa Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya wananchi wa Lushoto tumemuongezea vijiji vingine vinane vipya ambavyo vimeshafanyiwa survey na mkandarasi anaanza kuvifanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu lini vitapelekewa umeme, tunapoongea hapa mkandarasi ameshaweka magenge mawili, anaendelea na usambazaji wa nguzo pamoja na kufunga nyaya katika Kijiji cha Magamba pamoja na Mabughai. Kwa hiyo, ni matarajio yetu kwamba ndani ya mwezi huu wataviwasha vijiji hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pilli la uwezo wa mkandarasi, ni kweli mkandarasi huyu alianza kwa kususasua lakini tumeshakaa naye na ameshaweka magenge kumi na mawili kwenye Jimbo la Mheshimiwa Mbunge ni matarajio yetu mbali ya kumbadilisha tutamsimamia, tutamshinikiza, tutahakikisha kwamba anafanya kazi na anakamilisha ndani ya wakati.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Kata za Gare, Kwai, Kwemashai, Makanya, Kilole, Ngwelo na Ubiri hazikufikiwa na REA III mpaka sasa:- Je, ni lini sasa Serikali itafikisha umeme kwenye kata hizo?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID R. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Mimi naona wivu wenzangu wanapotoa pongezi kwamba maeneo yao umeme umeshapatikana, sasa mimi nina masikitiko makubwa kwamba bado katika Jimbo la Mlalo, Halmashauri hiyohiyo ya Lushoto, kata nne bado umeme haujawaka katika Kata za Mbalamo, Shagayu, Mbalu na Hemtoe. Barua ya kutoka REA kwenda kwa mkandarasi imetoka tangu mwaka jana. Nataka Mheshimiwa Waziri anipe commitment ni lini katika kata hizi na zenyewe umeme utawaka katika Jimbo la Mlalo, Halmashauri ya Lushoto?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Shangazi kwa maswali yake mazuri na kweli naungana na yeye kwamba kati ya maeneo ambayo mkandarasi alikuwa hajaanza kazi rasmi ni pamoja na Jimbo la Mheshimiwa Shangazi. Tunapoongea hapa na leo asubuhi tumeongea na Mheshimiwa Shangazi na mkandarasi ameshapeleka makundi manne, ni matarajio yetu atafanya kazi vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimuahidi Mheshimiwa Shangazi kwa niaba ya wananchi wake, mimi baada ya Bunge hili kuisha Mheshimiwa Shangazi tutafuatana mimi na naye tutakwenda kusimamia mguu kwa mguu mpaka vijiji vyake vyote ambavyo havijapatiwa umeme sasa vitapatiwa umeme. Awape uhakika wananchi wake kwamba Serikali hii haina mchezo kwenye suala la umeme vijijini.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Kata za Gare, Kwai, Kwemashai, Makanya, Kilole, Ngwelo na Ubiri hazikufikiwa na REA III mpaka sasa:- Je, ni lini sasa Serikali itafikisha umeme kwenye kata hizo?

Supplementary Question 3

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru sana kuniruhusu niulize hili la nyongeza, lakini kwanza nianze na shukurani kubwa sana, Mheshimiwa Waziri wa Nishati alikuja jimboni kwangu kuzindua REA III. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri kwa nini mkandarasi hajaanza kazi kwenye barabara ile ya kuja nyumbani kwangu, kijiji cha kwetu Kasenga, Majengo, Ikongolo, Kanyenye na Nzubuka?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Maige kwa swali lake la nyongeza. Kwanza nikubaliane na Mheshimiwa Maige, ameshafanya vijiji kumi na viwili kwenye jimbo lake lakini vijiji vya barabara ndiyo anaendelea navyo. Kwa hiyo, ni shauku ya Mheshimiwa Maige na wananchi kwamba vijiji vyote vingepatiwa umeme kwa siku moja. Nimhakikishie Mheshimiwa Maige kwamba hivi sasa anaendelea na Kijiji cha Lipogolo na kuna Kitongoji kinaitwa Kwa Muni ndipo anakosimika nguzo. Kwa hiyo, niungane na Mheshimiwa Mbunge kwamba ameshamaliza vijiji vya ndani sasa ameanza kufanya kazi katika vijiji vya kandokando mwa barabara. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Maige vijiji vyake kumi na moja vilivyobaki, vyote vitapelekewa umeme katika round hii ya kwanza.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Kata za Gare, Kwai, Kwemashai, Makanya, Kilole, Ngwelo na Ubiri hazikufikiwa na REA III mpaka sasa:- Je, ni lini sasa Serikali itafikisha umeme kwenye kata hizo?

Supplementary Question 4

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Tarehe 11 Julai, 2017, narudia tarehe 13 Julai, 2017 Mheshimiwa Waziri alikuja Nyamatala kuzindua umeme Kimkoa na uzinduzi ulifanyika katika Kijiji cha Nyamatala hadi leo ni kijiji kimoja tu ambacho kimeshawashwa umeme lakini kisingizio wanasema hakuna nyaya, nguzo na transfoma. Naomba majibu ya Serikali, hivi vijiji ambavyo vilikuwa vimepangwa kuwashwa umeme vitawashwa lini?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Ndassa na kwa kweli niseme tu katika Mkoa mzima wa Mwanza nitoe marekebisho kidogo ya hoja ya Mheshimiwa Ndasa, ni vijiji 21 tayari vimeshawashwa umeme siyo kijiji kimoja. Ni kweli kabisa katika jimbo lake Kijiji cha Nyamatala ambapo tulifanya uzinduzi tayari kimeshawashwa umeme na sasa wanaendelea na kijiji kinachofanya kwenda Sangabuye. Nikubaliane na Mheshimiwa Ndassa kwamba speed ya mkandarasi haikuwa nzuri, lakini tangu wiki iliyopita ameshaleta nguzo 500 katika jimbo lake ni matarajio yetu kwamba sasa speed itaongezeka. Nimwombe Mheshimiwa Ndassa tushikiriane atuletee maeneo yenye changamoto ili kazi iianze kutekelezwa haraka iwezekanavyo.