Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini wanaipongeza Serikali kwa kuanzisha Wilaya ya Kipolisi Mbalizi. • Je, ni lini Ofisi ya Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi pamoja na nyumba za askari zitajengwa? • Je, Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi ina magari mangapi na Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya vituo vya polisi katika Halmashauri ya Wilaya Mbeya?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, kwanza nianze kabisa kuipongeza Serikali pamoja na changamoto zote hizi za miundombinu na idadi ndogo ya askari lakini bado wameimarisha ulinzi katika Wilaya ya Mbeya na hususani Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi.
Swali la kwanza, je, ni lini Serikali itapeleka shilingi milioni 120 ambazo zitaunga mkono shilingi milioni 200 walizotumia wananchi kukamilisha Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi?
Swali la pili; je, ni lini Serikali itajenga Vituo vya Polisi katika miji inayochipukia ya Mjele, Ilembo pamoja na Igoma? Ahsante.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika umaliziaji pamoja na majengo mapya aliyoyasemea tutaweka kipaumbele katika mwaka huu wa fedha pamoja na bajeti zitakazofuatia kulingana na upatikanaji wa rasilimali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze tu Mheshimiwa Mbunge, amefanya jitihada kubwa sana katika jengo hili ambalo tunalisemea na aendelee na moyo huo huo na ndiyo maana wananchi wa Mbalizi pamoja na Mbeya Vijijini wanaendelea kumuamini na kuchangua.

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini wanaipongeza Serikali kwa kuanzisha Wilaya ya Kipolisi Mbalizi. • Je, ni lini Ofisi ya Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi pamoja na nyumba za askari zitajengwa? • Je, Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi ina magari mangapi na Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya vituo vya polisi katika Halmashauri ya Wilaya Mbeya?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona.
Wilaya ya Igunga ina Kata 35 na ina Vituo vya Polisi saba, Kituo cha Igunga, Nanga, Ziba, Simbo, Sungwizi na Choma na Igurubi lakini ina magari mawili tu ya polisi. Nauliza ni lini Serikali itasaidia Wilaya ya Igunga ikapata magari mengi ili kuhudumia wananchi wetu?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Kafumu kwa kulileta swali ambalo linaungwa mkono na jiografia ya Wilaya ya Igunga na naitambua Wilaya ya Igunga na natambua umuhimu wa swali alilouliza Mheshimiwa Kafumu, niseme tu tutaweka uzito pale tutakapokuwa tunagawa vitendea kazi kulingana na upatikanaji wake.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini wanaipongeza Serikali kwa kuanzisha Wilaya ya Kipolisi Mbalizi. • Je, ni lini Ofisi ya Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi pamoja na nyumba za askari zitajengwa? • Je, Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi ina magari mangapi na Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya vituo vya polisi katika Halmashauri ya Wilaya Mbeya?

Supplementary Question 3

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mwaka jana Mheshimiwa Waziri Mkuu alipotembelea Jimbo la Mtama alikuta tunajenga Kituo cha Polisi pale Mtama na akaahidi kwamba tukimaliza ujenzi wa kile kituo atatupatia gari kwa ajili ya kusaidia huduma za usalama katika lile eneo. Ni lini sasa ahadi hii ya Waziri Mkuu itatekelezwa?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa Nape kwa ufuatiliaji wake wa masuala ya jimboni kwake. Niseme tu kwamba ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ni maelekezo na sisi tutafanyia kazi maelekezo hayo.

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini wanaipongeza Serikali kwa kuanzisha Wilaya ya Kipolisi Mbalizi. • Je, ni lini Ofisi ya Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi pamoja na nyumba za askari zitajengwa? • Je, Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi ina magari mangapi na Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya vituo vya polisi katika Halmashauri ya Wilaya Mbeya?

Supplementary Question 4

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni kumezuka tabia mbaya ya Jeshi la Polisi, wanapokwenda kumkamata mtuhumiwa wakimkosa wanakamata mtu mbadala akiwa mke au watoto.
Naomba kufahamu Jeshi la Polisi linatoa wapi mamlaka haya ambapo wanashindwa kutumia mbinu zao za kiintelijensia kukamata mtuhumiwa badala yake wanarahisisha na kukamata mke au watoto na kuwatesa?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Devotha Minja, shemeji yangu na niseme tu kwa Jeshi la Polisi linafanya kazi kwa mujibu wa sheria na niseme hakuna mtu anayeruhusiwa kufanya adhabu kwa mbadala. Kosa linabaki kuwa la mkosaji. Kwa hiyo, nielekeze tu popote pale ambapo pana mtu amefanya kosa atafutwe yule yule aliyekosa na kama wengine wanaweza wakasaidia basi wasaidie katika namna ya kuelezea jinsi wanavyoweza kufahamu, lakini siyo kuchukua adhabu ya mtu mwingine aliyekosa.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini wanaipongeza Serikali kwa kuanzisha Wilaya ya Kipolisi Mbalizi. • Je, ni lini Ofisi ya Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi pamoja na nyumba za askari zitajengwa? • Je, Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi ina magari mangapi na Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya vituo vya polisi katika Halmashauri ya Wilaya Mbeya?

Supplementary Question 5

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa kipaumbele cha watu wa Kinole ni ujenzi wa Kituo cha Polisi ambacho tumeshajenga ambacho kimefikia mtambaa wa panya kinasubiri kuezekwa pamoja na ujenzi wa kituo cha afya; na kwa kuwa katika Kata ya Kinole kuna SACCOSS ya mfano yenye mtaji wa zaidi ya shilingi bilioni mbili na wakulima wakubwa wa matunda na viungo lakini kuna mzunguko mkubwa sana wa pesa lakini usalama ni mdogo na Serikali imepeleka pesa kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Kituo cha Kisimbi.
Je, Serikali iko tayari kuhamisha pesa hizi ilizopeleka katika ujenzi wa Kisimbi ambao ni ujenzi wa kituo cha utalii ambao siyo kipaumbele cha wananchi na kuna tatizo la mgogoro wa fidia na kupeleka kwenye umaliziaji wa Kituo cha Polisi kwenye mapato ya ndani?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo alilolisema Mheshimiwa Mbunge ni pendekezo. Niseme tu kama Serikali tunapokea pendekezo, lakini nimuombe Mheshimiwa Mbunge tupate fursa tuongee kwa undani zaidi ili tuweze kuhusisha na wadau wengine na Wizara zingine ambazo zinahusika.