Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Primary Question

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO (K.n.y. MHE. LAMECK AIRO) aliuliza:- Wilaya ya Rorya iliyoanzishwa mwaka 2007 sasa ina wakazi wapatao 400,000 na ina kata 26 na vijiji takriban 87 na ina vituo vya afya 4 lakini haina Hospitali ya Wilaya na wananchi wake hulazimika kutembea umbali wa takribani kilomita 30 kufuata huduma za afya Tarime na akina mama ambao ni asilimia 52 wanahitaji huduma ya hospitali kamili:- Je, ni lini Wilaya ya Rorya itajengewa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza nimshukuru Waziri kwa majibu yake mazuri na kueleza mkakati, lakini naomba niulize swali moja la nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hizi hospitali 67 ambazo zitajengwa, je, Wilaya ya Songea Mjini ipo? Kwa sababu kuna wakazi 300,000, Kata 21 na hakuna Hospitali ya Wilaya na kuna kituo hata kimoja tu cha afya. Je, Wilaya ya Songea Mjini ambapo Jimbo la Songea Mjini lipo itapata hizo hospitali 67?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Damas Ndumbaro, Mbunge wa Songea Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, tukumbuke nilipo-table budget speech yangu mwaka huu tarehe 14, niliainisha hospitali hizo ambapo kwa mara ya kwanza tunakwenda kuweka historia katika nchi yetu. Katika Mkoa wa Ruvuma tunakwenda kujenga hospitali Namtumbo, Songea DC pamoja na Nyasa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme wazi kwamba kwa Songea Mjini bado hatujatenga bajeti yake kwa sababu pale tuna Hospitali ya Mkoa. Hata hivyo, namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge tumewasiliana mara kadhaa. Tulichokifanya ni nini? Hapa katikati tutafanya resource mobilization kusaidia watu wa Songea Mjini waweze kupata japo kituo kingine acha afya as a backup strategy kupunguza idadi ya wagonjwa ambao wengi wanakwenda katika hospitali ya mkoa. Kwa hiyo, tutakwenda kulifanyia kazi suala hili katika kuimairisha vituo vya afya.

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO (K.n.y. MHE. LAMECK AIRO) aliuliza:- Wilaya ya Rorya iliyoanzishwa mwaka 2007 sasa ina wakazi wapatao 400,000 na ina kata 26 na vijiji takriban 87 na ina vituo vya afya 4 lakini haina Hospitali ya Wilaya na wananchi wake hulazimika kutembea umbali wa takribani kilomita 30 kufuata huduma za afya Tarime na akina mama ambao ni asilimia 52 wanahitaji huduma ya hospitali kamili:- Je, ni lini Wilaya ya Rorya itajengewa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Hivi karibuni katika kuboresha shughuli za afya nchini, Serikali ilitoa ahadi kwamba itatoa pesa kwa ajili ya kuboresha Kituo cha Afya cha Wampembe pamoja na kile kinachojengwa na wananchi cha Kasu. Nataka kuuliza, ni lini pesa hizi zitatolewa ili wananchi waweze kunufaika na huduma hizo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mipata, Mbunge wa Nkasi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumesema wazi kwamba tunajenga, tunaboresha vituo vya afya kwa mara ya kwanza 208 na tutatumia takribani shilingi bilioni 156 pamoja na kuimarisha miundombinu mingine hasa ya wahasibu. Hata hivyo, naomba nikiri wazi, juzi juzi tumeweka katika ile batch ya mwisho ya vituo 25 na muda siyo mrefu hapa nilikuwa naongea na Mheshimiwa Nkamia kuhusu fedha hizo. Kwa hiyo, tuta-cross checks vizuri ili katika maeneo yote tuliyoyapa kipaumbele fedha ziweze kufika.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika halmashauri ya Mheshimiwa Mbunge ambapo kulikuwa na changamoto ya ukosefu wa Hospitali ya Wilaya, katika mpango wetu wa Serikali wa kujenga hospitali 67 na wilaya yake tunakwenda kuipatia Hospitali ya Wilaya. Ni kwa imani yangu kubwa kwamba wananchi wa Nkasi kwa ujumla wake watapata huduma nzuri za afya katika maeneo yao.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO (K.n.y. MHE. LAMECK AIRO) aliuliza:- Wilaya ya Rorya iliyoanzishwa mwaka 2007 sasa ina wakazi wapatao 400,000 na ina kata 26 na vijiji takriban 87 na ina vituo vya afya 4 lakini haina Hospitali ya Wilaya na wananchi wake hulazimika kutembea umbali wa takribani kilomita 30 kufuata huduma za afya Tarime na akina mama ambao ni asilimia 52 wanahitaji huduma ya hospitali kamili:- Je, ni lini Wilaya ya Rorya itajengewa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Changamoto za huduma za afya zilizopo Rorya zinafanana na Jimbo la Nanyamba. Naishukuru Serikali imetupa ujenzi wa vituo vitatu na kituo kimoja cha Dijecha ujenzi umekamilika. Je, ni lini Serikali italeta watumishi kwa sababu kituo kile kina watumishi saba na mahitaji ya sasa ni watumishi 41?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ridhaa yako, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nimepata concern hii na kwa sababu tunajenga hivi vituo vya afya vipya 208 au tunaviboresha lengo letu kubwa ni ili viweze kufanya huduma ya upasuaji, tunajua tuna mahitaji makubwa ya wataalam. Hata hivyo, takribani wiki mbili zilizopita tumeshatangaza ajira zipatazo 6,180. Lengo kubwa ni kwamba watu wale tutakapowaajiri tuwapeleke katika vituo hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, imani yangu Mheshimiwa Chikota wala asihofu kwa sababu Nanyamba vilevile ni miongoni mwa eneo ambalo tunalenga kuja kujenga Hospitali ya Wilaya tunajua mahitaji yatakuwa ni makubwa zaidi. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba ni mpango wa Serikali wale watumishi 6,180 tutawagawanya maeneo mbalimbali lakini hata hivyo hatutaishia hapo itabidi tuongeze watumishi wengine kwa lengo la kuwasaidia Watanzania.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO (K.n.y. MHE. LAMECK AIRO) aliuliza:- Wilaya ya Rorya iliyoanzishwa mwaka 2007 sasa ina wakazi wapatao 400,000 na ina kata 26 na vijiji takriban 87 na ina vituo vya afya 4 lakini haina Hospitali ya Wilaya na wananchi wake hulazimika kutembea umbali wa takribani kilomita 30 kufuata huduma za afya Tarime na akina mama ambao ni asilimia 52 wanahitaji huduma ya hospitali kamili:- Je, ni lini Wilaya ya Rorya itajengewa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 4

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi. Hospitali au Kituo cha Afya cha Sinza maarufu kama Hospitali ya Palestina ilipandishwa hadhi na kuwa Hospitali ya Wilaya lakini bado iko katika mazingira madogo sana yaani eneo lake ni dogo sana na hata bajeti yake inakwenda kwenye masuala ya kituo cha afya. Je, ni lini sasa Serikali itatoa bajeti ya kutosha lakini vilevile kupanua mazingira yake ili wananchi wa Sinza na Ubungo kwa ujumla waweze kupata huduma stahiki? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la dada na mama yangu Mheshimiwa Susan Lyimo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, anachokisema Mheshimiwa Susan ni kweli. Wiki tatu zilizopita nilikuwa katika Kituo hicho cha Palestina, nilikwenda kukagua ujenzi, hasa miundombinu. Pale kulikuwa na ukarabati unafanyika lakini ukarabati ule nilipata mashaka kama value for money ipo? Nimekwenda kuangalia pale na population niliyoikuta pale ilikuwa ni kubwa sana. Ndiyo maana mpango wa Serikali kwa Wilaya ya Ubungo, kwanza yenyewe haina Hospitali ya Wilaya. Kile Kituo cha Afya hata ukiangalia mazingira yake siyo rafiki zaidi kupandishwa kuwa hospitali ya wilaya. Ndiyo maana mwaka huu sasa katika Jiji la Dar es Salaam tunakwenda kujenga hospitali tatu kuanzia Kigamboni, Ilala maeneo ya Kivule pamoja na Ubungo lakini wenyewe wata-decide wapi hospitali hizo zitakwenda kujengwa. Kwa hiyo, ni jukumu letu kuboresha huduma za afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, nimemweleza pale Mkurugenzi kwamba ukusanyaji wa mapato sikuridhika nao. Leo hii Kituo kile cha Palestina, thamani ya fedha inayokusanywa hailingani na idadi ya watu. Kwa hiyo, maana yake kuna mianya mikubwa ya upotevu wa mapato. Kwa hiyo, nilitoa maagizo, imani yangu kubwa ni kwamba eneo lile marekebisho yatafanyika kwa maslahi mapana ya wakazi wa Ubungo.