Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. MUSSA R. NTIMIZI aliuliza:- Wananchi Halmashauri ya Wilaya ya Tabora kwa kushirikiana na Mbunge wamejenga kituo kikubwa cha Polisi katika Kata ya Loya kilichogharimu zaidi ya Sh.100,000,000/= lakini mpaka sasa hakijaanza kufanya kazi:- • Je, Serikali ipo tayari kutenga bajeti kusaidia ujenzi wa nyumba za askari na kurekebisha upungufu mbalimbali uliopo? • Je, Serikali ipo tayari kutoa gari jipya ili kusaidia kurahisisha kazi ya Ulinzi na Usalama katika eneo hilo kwani kituo hicho kipo kilomita 120 kutoka Makao Makuu ya Wilaya – Isikizya?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Pia nashukuru majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kama alivyosema na kutupongeza wananchi, Mkurugenzi na mimi kwa nia nzuri ambayo tumeionesha ya kushirikiana na Jeshi la Polisi katika uhakikisha kero za ujambazi na usalama wa wananchi wetu zinatekelezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo hiki kimekamilika takribani miaka mitatu sasa na hayo marekebisho ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri ameyasema kama Mbunge nilikwishatoa fedha kwa maana mifuko ya simenti na nondo kurekebisha ile Amari ili kituo hiki kiweze kuanza kazi, takribani mwaka mmoja uliopita. Je, ananihakikishia vipi Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba kituo hichi sasa kitaenda kufunguliwa haraka kutokana na mahitaji yake?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini (b) Wilaya yetu ya Uyui ni Wilaya kubwa katika Mkoa wa Tabora ina majimbo mawili ya Igalula, Tabora Kaskazini lakini katika majibu yake amesema tuna magari matatu ambayo kwa kweli hayakidhi haja ya mahitaji ya Wilaya yetu. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kutuletea magari pamoja na mgao mkubwa wa mafuta ili kuweza kutoa huduma zilizo bora katika Wilaya yetu? Ahsante sana.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue fursa hii kuendelea kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa jitihadi zake ambazo amekuwa akizifanya katika kuhakikisha kwamba kituo hiki kinakamilika haraka. Ni sahihi kabisa Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo nimesema awali kwamba, amechangia katika kukamilika ujenzi wa Kituo cha Loya, ni jambo jema. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi kwamba, si dhamira ya Serikali kuona jitihada zake na wananchi ambao wametumia nguvu zao kujenga kituo hiki ziende bure bure kwa kuchelewesha kukitumia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu katika swali la msingi ni kwamba, tatizo lililopo ni kwamba tunahitaji kukamilisha Lockup pamoja na amari ili ziwe katika hali nzuri kabla ya matumizi. Jambo hilo tunatarajia kulikamilisha katika muda mfupi sana ujao. Nitahakikisha kwamba nitakapotoka hapa nitafuatilia ili katika kipindi cha mwezi mmoja tuweze kukamilisha vitu hivyo viwili na kituo hiki kianze kutumika mara moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na magari, ni sahihi kwamba katika Wilaya ambazo zina changamoto za magari mojawapo ni Wilaya ya Uyui katika Mkoa wa Tabora. Ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba maeneo yote ikiwemo Wilaya ya Uyui hasa kulingana na ukubwa wa kijiografia wa Wilaya ile yanapata magari ya kutosha zaidi ya yale magari matatu ambayo nimeyazungumza katika jibu langu la msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu ambacho tunaweza kusema kwamba sasa hivi kinatukwaza au kinatukwamisha kutekeleza hilo ni kwamba bado mgao huo haujafanyika kutokana na changamoto mbalimbali ambazo zinakabili programu zima ya uletaji wa magari yaliyodhamiriwa kuletwa katika Serikali. Changamoto hizo zitakapopata ufumbuzi na magari hayo yatakapokuwa tayari kugawiwa, basi nina uhakika basi Mkoa wa Tabora ikiwemo Wilaya ya Uyui na Wilaya nyingine kama Nzega haina gari hata moja zitapewa kipaumbele.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. NTIMIZI aliuliza:- Wananchi Halmashauri ya Wilaya ya Tabora kwa kushirikiana na Mbunge wamejenga kituo kikubwa cha Polisi katika Kata ya Loya kilichogharimu zaidi ya Sh.100,000,000/= lakini mpaka sasa hakijaanza kufanya kazi:- • Je, Serikali ipo tayari kutenga bajeti kusaidia ujenzi wa nyumba za askari na kurekebisha upungufu mbalimbali uliopo? • Je, Serikali ipo tayari kutoa gari jipya ili kusaidia kurahisisha kazi ya Ulinzi na Usalama katika eneo hilo kwani kituo hicho kipo kilomita 120 kutoka Makao Makuu ya Wilaya – Isikizya?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mkoa wa Arusha ni Mkoa ambao una shughuli nyingi sana haswa za kipolisi, zikiwemo na ku-escort viongozi mbalimbali, lakini inasikitisha sana Mkoa wa Arusha RPC wetu hana gari la polisi kutokana na gari lake lilipata ajali muda mrefu. Je, Serikali haioni ni muhimu kulichukulia jambo hili kama la dharura na kumpelekea RPC wetu wa Mkoa wa Arusha gari?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna umuhimu mkubwa RPC kuwa na gari. Nataka tu nimthibitishie kwamba kama gari la RPC limepata ajali basi tutaangalia uwezekano wa kulifanyia ukarabati gari hilo, likishindikana basi RPC wa Tabora tutampatia gari nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Samahani ni RPC wa Arusha.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. MUSSA R. NTIMIZI aliuliza:- Wananchi Halmashauri ya Wilaya ya Tabora kwa kushirikiana na Mbunge wamejenga kituo kikubwa cha Polisi katika Kata ya Loya kilichogharimu zaidi ya Sh.100,000,000/= lakini mpaka sasa hakijaanza kufanya kazi:- • Je, Serikali ipo tayari kutenga bajeti kusaidia ujenzi wa nyumba za askari na kurekebisha upungufu mbalimbali uliopo? • Je, Serikali ipo tayari kutoa gari jipya ili kusaidia kurahisisha kazi ya Ulinzi na Usalama katika eneo hilo kwani kituo hicho kipo kilomita 120 kutoka Makao Makuu ya Wilaya – Isikizya?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ukizunguka Tanzania nzima kwenye vituo vya polisi vyote utakuta magari mengi sana mabovu ambayo ni ya polisi wenyewe kwa maana ya kwamba ni ya Serikali hayajatengenezwa na hayafai tena kutengenezwa yanavyoonekana mengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo ukija Jimbo la Ndanda, Kituo cha Polisi cha Ndanda ambacho kinahudumia jimbo zima na tuna kituo kimoja tu cha polisi hivi karibuni tuliletewa gari ambalo nalo linaonekana ni bovu kwa sababu toka limefika halijawahi kutumika. Sasa nataka Waziri atuambie ni lini mahususi kabisa wataamua kutengeneza gari la Kituo cha Polisi cha Ndanda kwa ajili ya kuweza kutoa huduma maeneo ya Jimbo la Ndanda ambayo yanasaidia pia na Jimbo la Ruangwa.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nizungumze kwa ujumla kwamba, tunakiri juu ya uwepo wa baadhi ya magari chakavu katika maeneo mbalimbali nchini. Hata hivyo, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine wote waliopo humu ndani na wananchi kwa ujumla kwamba tuna jitihada mbalimbali zinafanyika. Nyingine zinafanyika katika mikoa lakini nyingine zinafanyika katika ngazi ya Kitaifa kuhakikisha kwamba magari haya yanakuwa katika hali nzuri. Magari mengi tu ambayo yapo katika maeneo mbalimbali nchini tumeanza kuyafufua yanatumika, yale ambayo yanawezekana kufufulika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala la gari hii ya Ndanda specifically kwanza nataka nilichukue hili suala kwa sababu ni jambo ambalo haliingii akilini kwamba gari inapelekwa katika kituo na wakati huo gari haijaanza kutumika inakuwa mbovu. Kwa hiyo, nijue kwanza gari hii ilitoka wapi na kwa nini iwe haitumiki? Halafu tuangalie sasa baada ya hapo nini kifanyike ili kuweza kurekebisha.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. MUSSA R. NTIMIZI aliuliza:- Wananchi Halmashauri ya Wilaya ya Tabora kwa kushirikiana na Mbunge wamejenga kituo kikubwa cha Polisi katika Kata ya Loya kilichogharimu zaidi ya Sh.100,000,000/= lakini mpaka sasa hakijaanza kufanya kazi:- • Je, Serikali ipo tayari kutenga bajeti kusaidia ujenzi wa nyumba za askari na kurekebisha upungufu mbalimbali uliopo? • Je, Serikali ipo tayari kutoa gari jipya ili kusaidia kurahisisha kazi ya Ulinzi na Usalama katika eneo hilo kwani kituo hicho kipo kilomita 120 kutoka Makao Makuu ya Wilaya – Isikizya?

Supplementary Question 4

MHE. BONIPHANCE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Vituo vya polisi vya Nyamuswa, Mgeta vimejengwa miaka ya 60, majengo yake sasa hivi ni hatarishi na wananchi wako tayari kusaidiana na Serikali kujenga vituo vile kwa kutoa nguvu kazi ya tofali, maji, kokoto na mawe. Je, Serikali iko tayari kushirikiana na wananchi kujenga vituo hivyo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Getere kwa jitihada zake za kuhamasisha wananchi kuweza kupata vifaa ambavyo amevizungumza kwa ajili ya ujenzi wa vituo. Nataka nimhakikishie kwamba, Serikali itahakikisha kwamba tunaunga mkono jitihada hizo ili kuweza kufanikisha malengo ambayo wameyakusudia.

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. MUSSA R. NTIMIZI aliuliza:- Wananchi Halmashauri ya Wilaya ya Tabora kwa kushirikiana na Mbunge wamejenga kituo kikubwa cha Polisi katika Kata ya Loya kilichogharimu zaidi ya Sh.100,000,000/= lakini mpaka sasa hakijaanza kufanya kazi:- • Je, Serikali ipo tayari kutenga bajeti kusaidia ujenzi wa nyumba za askari na kurekebisha upungufu mbalimbali uliopo? • Je, Serikali ipo tayari kutoa gari jipya ili kusaidia kurahisisha kazi ya Ulinzi na Usalama katika eneo hilo kwani kituo hicho kipo kilomita 120 kutoka Makao Makuu ya Wilaya – Isikizya?

Supplementary Question 5

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Hali ya vituo vya Polisi vya Kata pale Temeke ni mbaya sana, mapaa yameoza kabisa na Polisi muda mwingi wanafanya kazi chini ya miti badala ya kukaa kwenye ofisi kwa sababu hazikaliki. Hata hivyo, hata zile ofisi chache ambazo tumezijenga kwa nguvu za wananchi kama pale Makangalawe na Buza ambazo tumeshindwa kumalizia vyumba vya mahabusu na vya kutunzia silaha Serikali nayo imeshindwa kuvimalizia ili viweze kufanya kazi masaa 24. Sasa labda kwa sababu Mawaziri hawafahamu hali halisi iliyopo huko kwenye vituo hivyo ndio maana kila siku wamekuwa wakisema wanasubiri bajeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, kwa kadri watakavyoweza kujipanga ni lini watakuwa tayari kuja kufanya ziara Temeke ili wakajionee hali halisi ya vituo hivi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza si sahihi kwamba hatufahamu au hatujafika. Binafsi nimeshafanya ziara katika Jimbo lake na Wilaya yake na nimeshiriki katika ujenzi wa kituo pale nimesahau jina la kile kituo, lakini ni maeneo ya Mbagala. Hali kadhalika nikashiriki katika uzinduzi wa kituo kingine cha Polisi nikizindua maeneo ya kule Wilaya hiyo ya Temeke lakini Jimbo la Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni kwamba hali ya vituo vya Polisi vya Temeke tunaifahamu vizuri, kwa sababu physically nimekwenda na nimeshuhudia na tumeshiriki na wananchi kuweza kufanya kazi ya kuvijenga na kuvikarabati vituo vingine ambavyo ni vichakavu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu ambacho ningemwomba Mheshimiwa Mbunge atusaidie ni kwamba, naye aendelee kuunga jitihada zetu hizi mkono kwa sababu si rahisi kuweza kukabiliana na changamoto hizi za vituo kwa wakati mmoja. Ndio maana tunafanya kazi hizi kwa awamu na kuhamasisha wadau kama sio wananchi na Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo niliwapongeza Waheshimiwa Wabunge waliopita hapa, Mheshimiwa Getere, Mheshimiwa Ntimizi katika suala hili hili la msingi ambalo nimejibu, basi na Mheshimiwa Mtolea naye tunakukaribisha aweze kuhamasisha wananchi hata kama akiamua fedha yake ya Mfuko wa Jimbo aingize katika kukarabati vituo hivi, tutamshukuru sana.