Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:- Kumekuwa na migogoro ya mipaka kati ya hifadhi na wananchi kwenye vijiji vinavyopakana na Hifadhi hizo kama vile Ruhembe, Kitete, Kikwalaza, Mji Mpya, Ihambwe, Mululu na sasa Kitongoji cha Lugawilo, Kata ya Uleling’ombe:- Je, ni lini Serikali itaweka mipaka ili wananchi hao wasiendelee kunyang’anjywa ardhi yao kwa kisingizio cha kuwa wameingia kwenye Hifadhi?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Awali ya yote, nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kufanya ziara Jimboni kwangu Mikumi, pindi ambapo simba walivamia zizi la mwanakijiji wetu pale Kikwalaza na akaweza kuzungumza na wananchi. Pia alifanikiwa kwenda Ruhembe, bahati mbaya sana ni kwamba Mheshimiwa Naibu Waziri hakuwasiliza wananchi bali alisikiliza haya ambayo anaambiwa na viongozi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza niseme tu, kama kweli tunaipenda nchi yetu, sisi tunajua kwamba kuwa na Hifadhi ya Taifa ya Mikumi siyo laana bali ni baraka kutoka kwa Mungu, lakini ukweli ni kwamba wananchi wa Kata ya Ruhembe, Kijiji cha Kitete Msindazi na Kielezo wanateseka sana kwa sababu ya kunyimwa haki zao za msingi za kuishi maeneo yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie tu Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na ziara aliyoifanya, yale yote aliyoyazungumza kule hakuna hata kimoja kilichotekelezwa. Nimwombe asiwasikilize hawa wanaomwandikia hivi vitu, aje awasikilize wananchi wa Kata wa Ruhembe wamwambie A, B, C na vitu vingine vyote. Kwa hiyo, hiyo ndiyo rai yangu kwake kwamba namkaribisha tena Mikumi, azungumze na wananchi hawa viongozi wanaomwambia yote yamekamilika na kwamba kuna amani, wanafanyakazi yake iwe ngumu sana kwa kutokuwa na amani katika Kata yetu na Jimbo la Mikumi kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sasa hivi wananchi wa Mikumi, napata ukakasi kusema kama wanapotea au wanachukuliwa na watu wasiojulikana, kuna watu wanatoka Usalama na TANAPA wananchi wa Mikumi wanakufa na wanapotea na wengine wanarudi wakiwa vilema kwa sababu tu wanaonekana kuchukuliwa katika hali ambayo haipo na tukiwatafuta katika Vituo vya Polisi hatuwapati, tunaambiwa wamepelekwa Dar es Salaam. Je, Serikali inasemaje kuhusu wananchi wa Mikumi wanaopotea? Mpaka sasa takribani wananchi 40 kutoka Kata za Muhenda, Ruhembe, Kidodi wamepotea hatujui wako wapi. Serikali inataka kutuambia nini kuhusu hawa ndugu zetu? Tumechoka kuzika nguo na ndugu zetu hatuwaoni? Ahsante sana.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph Leonard Haule, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa nimeshatembelea eneo hilo na ni kweli kabisa nilikaa na wananchi tukaweza kuzungumza na wakabainisha mambo mengi na tuliyawekea mkakati wa namna ya kuyatatua. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kipindi kati ya sasa na mwezi Septemba, tena wakati nakwenda Kilombero, nitapita kwenye eneo hilo ili tuweze kukutana na hao wananchi ili tuone kama kweli matatizo yao yanaendelea kuwepo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu hao wananchi ambao anasema kwamba wanapotea bila sisi kujua, nadhani hizi taarifa kama Serikali hatunazo. Kama Mheshimiwa Mbunge anayo majina na anasema wananchi karibu 40 wote wamepotea, nadhani ni wakati muafaka tupatie hayo majina ili nasi Serikali tuweze kushirikiana na wananchi kubaini hao wananchi wote watakuwa wamekwenda wapi. Ni msimamo wetu kama Serikali kwamba kazi yetu ni kulinda wananchi na kuhakikisha wanaendelea kuishi vizuri na kufanya shughuli zao.

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:- Kumekuwa na migogoro ya mipaka kati ya hifadhi na wananchi kwenye vijiji vinavyopakana na Hifadhi hizo kama vile Ruhembe, Kitete, Kikwalaza, Mji Mpya, Ihambwe, Mululu na sasa Kitongoji cha Lugawilo, Kata ya Uleling’ombe:- Je, ni lini Serikali itaweka mipaka ili wananchi hao wasiendelee kunyang’anjywa ardhi yao kwa kisingizio cha kuwa wameingia kwenye Hifadhi?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Maliasili ndani ya Jimbo la Mlimba wamepeleka barua kwamba wananchi wakulima na wafugaji mwezi Julai waondoke wakati wa mipaka ya bonde hilo haijafanyiwa kazi na Waziri aliunda timu, kwenda kurekebisha mipaka ya Ramsar. Nini kauli ya Serikali kuhusu vitisho kwa wananchi hawa ambao hata mazao yao hawajavuna?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Susan Kiwanga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa mnamo mwaka jana tulitembelea bonde lote na tukazungumza na wananchi. Wananchi waliomba badala ya kuhama katika kipindi kile wapatiwe muda wa kutosha wa kujiandaa na waweze kuvuna mazao yao ndipo wahame. Ndipo Serikali ikatoa agizo kwamba ifikapo mwisho wa mwezi Agosti, 2018 wananchi hao wote wawe wamehama na wamevuna mazao yao yote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kama unaniambia kwamba wameambiwa wahame mwezi wa Julai, ni kinyume na agizo tulilokuwa tumelitoa awali. Agizo la Serikali tulisema wananchi wale waachwe, wavune mazao yao lakini ikifika tarehe 31 Agosti, 2018, wananchi wote wawe wameshahama katika eneo hilo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Susan na wananchi wake waendelee kutulia, wavune kwa utaratibu ili kusudi wahamie katika yale maeneo ambayo watakuwa wameelekezwa na Serikali.

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:- Kumekuwa na migogoro ya mipaka kati ya hifadhi na wananchi kwenye vijiji vinavyopakana na Hifadhi hizo kama vile Ruhembe, Kitete, Kikwalaza, Mji Mpya, Ihambwe, Mululu na sasa Kitongoji cha Lugawilo, Kata ya Uleling’ombe:- Je, ni lini Serikali itaweka mipaka ili wananchi hao wasiendelee kunyang’anjywa ardhi yao kwa kisingizio cha kuwa wameingia kwenye Hifadhi?

Supplementary Question 3

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Ni lini Serikali itatatua mgogoro wa muda mrefu wa mpaka kati ya Hifadhi ya Uwanda na Vijiji vya Ilambo, Mpande, Kilangawana, Legeza, Kapenta, Mkusi na Iwelamvua ili kuondoa manyanyaso ambayo wananchi wanapata kwa kunyang’anywa mazao, vifaa vyao vya kilimo na kuwapiga na mwaka juzi mtu mmoja aliuwawa? Ni lini Serikali itatatua mgogoro huu?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Malocha, Mbunge machachari kweli kweli, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba kumekuwepo na changamoto ya mgogoro ambayo imekuwepo katika eneo lile. Hivi sasa tumejipanga katika kipindi hiki, Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii atakwenda kuona eneo hilo. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane ili kusudi apate ratiba kamili ni lini atakuja, mtatembelea maeneo ya vijiji vyote hivyo na kuona ni hatua gani zichukuliwe kuhakikisha kwamba hiyo migogoro ambayo imedumu muda mrefu basi yote inatatuliwa kwa kipindi hiki.

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:- Kumekuwa na migogoro ya mipaka kati ya hifadhi na wananchi kwenye vijiji vinavyopakana na Hifadhi hizo kama vile Ruhembe, Kitete, Kikwalaza, Mji Mpya, Ihambwe, Mululu na sasa Kitongoji cha Lugawilo, Kata ya Uleling’ombe:- Je, ni lini Serikali itaweka mipaka ili wananchi hao wasiendelee kunyang’anjywa ardhi yao kwa kisingizio cha kuwa wameingia kwenye Hifadhi?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Awali ya yote, nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kufanya ziara Jimboni kwangu Mikumi, pindi ambapo simba walivamia zizi la mwanakijiji wetu pale Kikwalaza na akaweza kuzungumza na wananchi. Pia alifanikiwa kwenda Ruhembe, bahati mbaya sana ni kwamba Mheshimiwa Naibu Waziri hakuwasiliza wananchi bali alisikiliza haya ambayo anaambiwa na viongozi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza niseme tu, kama kweli tunaipenda nchi yetu, sisi tunajua kwamba kuwa na Hifadhi ya Taifa ya Mikumi siyo laana bali ni baraka kutoka kwa Mungu, lakini ukweli ni kwamba wananchi wa Kata ya Ruhembe, Kijiji cha Kitete Msindazi na Kielezo wanateseka sana kwa sababu ya kunyimwa haki zao za msingi za kuishi maeneo yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie tu Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na ziara aliyoifanya, yale yote aliyoyazungumza kule hakuna hata kimoja kilichotekelezwa. Nimwombe asiwasikilize hawa wanaomwandikia hivi vitu, aje awasikilize wananchi wa Kata wa Ruhembe wamwambie A, B, C na vitu vingine vyote. Kwa hiyo, hiyo ndiyo rai yangu kwake kwamba namkaribisha tena Mikumi, azungumze na wananchi hawa viongozi wanaomwambia yote yamekamilika na kwamba kuna amani, wanafanyakazi yake iwe ngumu sana kwa kutokuwa na amani katika Kata yetu na Jimbo la Mikumi kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sasa hivi wananchi wa Mikumi, napata ukakasi kusema kama wanapotea au wanachukuliwa na watu wasiojulikana, kuna watu wanatoka Usalama na TANAPA wananchi wa Mikumi wanakufa na wanapotea na wengine wanarudi wakiwa vilema kwa sababu tu wanaonekana kuchukuliwa katika hali ambayo haipo na tukiwatafuta katika Vituo vya Polisi hatuwapati, tunaambiwa wamepelekwa Dar es Salaam. Je, Serikali inasemaje kuhusu wananchi wa Mikumi wanaopotea? Mpaka sasa takribani wananchi 40 kutoka Kata za Muhenda, Ruhembe, Kidodi wamepotea hatujui wako wapi. Serikali inataka kutuambia nini kuhusu hawa ndugu zetu? Tumechoka kuzika nguo na ndugu zetu hatuwaoni? Ahsante sana.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph Leonard Haule, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa nimeshatembelea eneo hilo na ni kweli kabisa nilikaa na wananchi tukaweza kuzungumza na wakabainisha mambo mengi na tuliyawekea mkakati wa namna ya kuyatatua. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kipindi kati ya sasa na mwezi Septemba, tena wakati nakwenda Kilombero, nitapita kwenye eneo hilo ili tuweze kukutana na hao wananchi ili tuone kama kweli matatizo yao yanaendelea kuwepo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu hao wananchi ambao anasema kwamba wanapotea bila sisi kujua, nadhani hizi taarifa kama Serikali hatunazo. Kama Mheshimiwa Mbunge anayo majina na anasema wananchi karibu 40 wote wamepotea, nadhani ni wakati muafaka tupatie hayo majina ili nasi Serikali tuweze kushirikiana na wananchi kubaini hao wananchi wote watakuwa wamekwenda wapi. Ni msimamo wetu kama Serikali kwamba kazi yetu ni kulinda wananchi na kuhakikisha wanaendelea kuishi vizuri na kufanya shughuli zao.

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:- Kumekuwa na migogoro ya mipaka kati ya hifadhi na wananchi kwenye vijiji vinavyopakana na Hifadhi hizo kama vile Ruhembe, Kitete, Kikwalaza, Mji Mpya, Ihambwe, Mululu na sasa Kitongoji cha Lugawilo, Kata ya Uleling’ombe:- Je, ni lini Serikali itaweka mipaka ili wananchi hao wasiendelee kunyang’anjywa ardhi yao kwa kisingizio cha kuwa wameingia kwenye Hifadhi?

Supplementary Question 5

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Maliasili ndani ya Jimbo la Mlimba wamepeleka barua kwamba wananchi wakulima na wafugaji mwezi Julai waondoke wakati wa mipaka ya bonde hilo haijafanyiwa kazi na Waziri aliunda timu, kwenda kurekebisha mipaka ya Ramsar. Nini kauli ya Serikali kuhusu vitisho kwa wananchi hawa ambao hata mazao yao hawajavuna?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Susan Kiwanga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa mnamo mwaka jana tulitembelea bonde lote na tukazungumza na wananchi. Wananchi waliomba badala ya kuhama katika kipindi kile wapatiwe muda wa kutosha wa kujiandaa na waweze kuvuna mazao yao ndipo wahame. Ndipo Serikali ikatoa agizo kwamba ifikapo mwisho wa mwezi Agosti, 2018 wananchi hao wote wawe wamehama na wamevuna mazao yao yote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kama unaniambia kwamba wameambiwa wahame mwezi wa Julai, ni kinyume na agizo tulilokuwa tumelitoa awali. Agizo la Serikali tulisema wananchi wale waachwe, wavune mazao yao lakini ikifika tarehe 31 Agosti, 2018, wananchi wote wawe wameshahama katika eneo hilo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Susan na wananchi wake waendelee kutulia, wavune kwa utaratibu ili kusudi wahamie katika yale maeneo ambayo watakuwa wameelekezwa na Serikali.

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:- Kumekuwa na migogoro ya mipaka kati ya hifadhi na wananchi kwenye vijiji vinavyopakana na Hifadhi hizo kama vile Ruhembe, Kitete, Kikwalaza, Mji Mpya, Ihambwe, Mululu na sasa Kitongoji cha Lugawilo, Kata ya Uleling’ombe:- Je, ni lini Serikali itaweka mipaka ili wananchi hao wasiendelee kunyang’anjywa ardhi yao kwa kisingizio cha kuwa wameingia kwenye Hifadhi?

Supplementary Question 6

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Ni lini Serikali itatatua mgogoro wa muda mrefu wa mpaka kati ya Hifadhi ya Uwanda na Vijiji vya Ilambo, Mpande, Kilangawana, Legeza, Kapenta, Mkusi na Iwelamvua ili kuondoa manyanyaso ambayo wananchi wanapata kwa kunyang’anywa mazao, vifaa vyao vya kilimo na kuwapiga na mwaka juzi mtu mmoja aliuwawa? Ni lini Serikali itatatua mgogoro huu?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Malocha, Mbunge machachari kweli kweli, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba kumekuwepo na changamoto ya mgogoro ambayo imekuwepo katika eneo lile. Hivi sasa tumejipanga katika kipindi hiki, Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii atakwenda kuona eneo hilo. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane ili kusudi apate ratiba kamili ni lini atakuja, mtatembelea maeneo ya vijiji vyote hivyo na kuona ni hatua gani zichukuliwe kuhakikisha kwamba hiyo migogoro ambayo imedumu muda mrefu basi yote inatatuliwa kwa kipindi hiki.