Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- (a) Je, ni viwanda vingapi vimeanzishwa tangu Serikali ya Awamu ya Tano ianze utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda? (b) Je ni viwanda vingapi vilibinafsishwa na kushindwa kuendelezwa ambavyo vimerejeshwa Serikalini tangu kuanza utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda? (c) Je sekta ya viwanda inachangia kiasi gani pato la Taifa?

Supplementary Question 1

MHE. USSI S. PONDEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza ningependa Hansard isomeke vizuri, mimi sio Mbunge wa Chumbageni, ni Mbunge wa Chumbuni, Zanzibar, Chumbageni ipo Tanga, kwa hiyo ningependa hansard isomeke vizuri.

Mheshimiwa Mwneyekiti, nina maswali mawili ya nyongeza ambayo ningependa kumuuliza Mheshimiwa Waziri. Kwanza angetupatia tafsiri ya viwanda, katika majibu yake mazuri ametuambia kuna viwanda vidogo na viwanda vidogo sana; kwa hiyo tungependa tupate tafsiri nini tofauti ya viwanda vidogo na viwanda vidogo sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ningependa kumuuliza, kwa kuwa Wizara yake haihusiki na uwekezaji wa viwanda katika Serikali ya Zanzibar; hadi sasa wawekezaji wakitaka kuwekeza Zanzibar wanatakiwa wachukue leseni zitoke BRELA. Je, Serikali haioni sasa umefika wakati wa kuiachia Wizara ya Viwanda ya Serikali ya Zanzibar kuweza kusimamia kazi hii ya utoaji wa leseni?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimuombe radhi kwa kukosea Jimbo lake na nashukuru amesahihisha. Pili, napenda kusema kwamba viwanda vidogo sana ni vile ambavyo mtaji wake hauzidi milioni tano na wafanyakazi wake hawazidi wane. Viwanda ni vidogo vile ambavyo mtaji wake ni ule ambao hauzidi milioni 200 na wafanyakazi wake hawazidi 49.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa suala la leseni; suala hilo umelizungumza lakini kimsingi ni kwamba Wizara ya Viwanda na Biashara inashirikiana kwa karibu sana na Wizara ya Viwanda Zanzibar kiasi kwamba shughuli nyingi tunafanya pamoja. Hata hivyo maboresho yoyote yanayolenga kurekebisha na kuleta urahisi wa kuwekeza yatafanyiwa kazi ili kuwawezesha wananchi wetu na wadau mbalimbali wanaopenda kuwekeza wafanye shughuli zao bila shida na kwa uharaka iwezekanavyo.

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- (a) Je, ni viwanda vingapi vimeanzishwa tangu Serikali ya Awamu ya Tano ianze utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda? (b) Je ni viwanda vingapi vilibinafsishwa na kushindwa kuendelezwa ambavyo vimerejeshwa Serikalini tangu kuanza utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda? (c) Je sekta ya viwanda inachangia kiasi gani pato la Taifa?

Supplementary Question 2

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Sera ya Viwanda Tanzania imetamalaki. Sasa nipende kumuuliza Mheshimiwa Waziri Kiwanda cha Kufua Chuma pale Liganga kitaanza lini?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ngalawa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi chuma cha Liganga kinahitaji uwekezaji mkubwa sana na pale tunazungumzia kuwekeza katika suala la ufuaji wa chuma, ambacho kimechanganyika na madini ya aina nyingine ikiwemo Titanium, Vanadium na Aluminium; wakati huo huo kuna suala la kufua umeme. Hayo yote yanafanyiwa kazi na ikizingatiwa kwamba hivi karibuni tulipitisha sheria zetu ya kutunza rasilimali zetu na kuwawezesha Watanzania kunufaika zaidi, hayo yote yanaangaliwa kwa umakini na tutakapo kuwa tayari, shughuli hiyo itaanza mara moja.

Name

Saed Ahmed Kubenea

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- (a) Je, ni viwanda vingapi vimeanzishwa tangu Serikali ya Awamu ya Tano ianze utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda? (b) Je ni viwanda vingapi vilibinafsishwa na kushindwa kuendelezwa ambavyo vimerejeshwa Serikalini tangu kuanza utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda? (c) Je sekta ya viwanda inachangia kiasi gani pato la Taifa?

Supplementary Question 3

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuongeza swali la nyongeza. Kwa kuwa miongoni mwa viwanda ambavyo vimebinafsishwa na Serikali, ni Kiwanda cha Nguo cha Urafiki. Katika Kiwanda cha Nguo cha Urafiki mwekezaji hakuja na mtaji, badala yake Serikali ndiyo ilikwenda kukopa katika Benki ya Exim ya China na ikampa mwekezaji mtaji wa kuendesha Kiwanda cha Urafiki. Je, ni lini Serikali itakirejesha Kiwanda cha Urafiki mikononi mwa wananchi wa Dar es Salaam?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kubenea kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo umezungumza, Kiwanda cha Urafiki kinatokana na urafiki kati ya nchi ya China na Tanzania. Ni Kiwanda ambacho msingi wake ulijengwa katika mahusiano hayo ya nchi mbili ya Kidiplomasia. Kwa hiyo, tunatamani kuona kiwanda hicho kikifanya kazi vizuri zaidi na wote tumekifuatilia na kujua kwamba kuna maeneo yanayohitajika kufanyiwa marekebisho. Hivyo, Serikali hizi mbili zinashughulika kwa pamoja kuona ni namna gani kiwanda hicho kitaendelezwa vizuri zaidi. (Makofi)

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- (a) Je, ni viwanda vingapi vimeanzishwa tangu Serikali ya Awamu ya Tano ianze utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda? (b) Je ni viwanda vingapi vilibinafsishwa na kushindwa kuendelezwa ambavyo vimerejeshwa Serikalini tangu kuanza utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda? (c) Je sekta ya viwanda inachangia kiasi gani pato la Taifa?

Supplementary Question 4

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo tu la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aomba niiulize Serikali, kwa kuwa Kiwanda cha Nyuzi cha Tabora hakifanyi kazi; na kwa kuwa mpaka sasa kimeiondolea Tabora kupata mapato ya uhakika na vijana kupata ajira: Je, Serikali iko tayari sasa kukinyang’anya na kukirejesha kiwanda hicho Serikalini? Hakifai kabisa. (Makofi)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kimsingi Kiwanda hicho kimezungumzwa siku nyingi na mmekuwa mkikifuatilia. Niseme tu kwamba kabla ya kukirejesha kiwanda Serikalini, hatua ya kwanza ni sisi kukitembelea na kujiridhisha, kwa nini hakiwezi kufanya kazi zake inavyopaswa, ikizingatiwa kwamba Tanzania ni nchi ambayo inalima pamba kwa wingi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakapomaliza Bunge, nitatembelea kiwanda hicho ili kujiridhisha na niweze kutoa ushauri Serikalini juu ya utekelezaji utakaofuata. (Makofi)