Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Tulia Ackson

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. DKT. TULIA ACKSON (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:- Wilaya ya Rungwe ina vyanzo vingi vya maji ambavyo vinatiririsha maji. Je, ni lini Serikali itarekebisha miundombinu ili kuongeza kiwango cha maji ambayo kwa sasa hayatoshi kiasi cha kufanya Idara ya Maji kufunga baadhi ya maeneo kama vile Vijiji vya Ibungila, Lubiga na kadhalika?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. TULIA ACKSON: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, yanayoonesha kwamba sasa Vijiji vya Ibungila na Lubiga vitapata maji kupitia mradi huu, upo mradi wa Masoko Group ambao umesuasua kwa muda mrefu, naomba Mheshimiwa Naibu Waziri atuambie ni lini mradi huu utakamilika ili wananchi wa vijiji vya Kata ya Masoko waweze kupata maji?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, uchakavu wa miundombinu katika Kata mbalimbali za Mbeya Jiji hususan Kata ya Ilomba, Mtaa wa Hayanga – Ituha, Tonya na Ihanda, Kata ya Iganzo Mtaa wa Igodima na Mwambenja, Kata ya Iyunga Mtaa wa Sistila, Kata ya Ghana Mtaa wa Magharibi na Mashariki, Iganjo Mtaa wa Iganga na Igawilo Mtaa wa Sokoni na Chemi: Ni lini Kata hizi zitapelekewa miradi ili ziweze kupata maji?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, Dkt. Tulia kwa kazi nzuri sana anayoifanya na katika kuhakikisha anawatetea wananchi waweze kupata maji. Kubwa sana ni kuhusu suala zima la kusuasua kwa mradi wa maji wa Masoko Group.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge, nilifanya ziara katika eneo lile la Masoko Group na tukaona usuaji wa mradi ule, tukaagiza timu ya Wizara ili iweze kufika na kuongeza nguvu katika kuhakikisha mradi ule unakamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Naibu Katibu Mkuu Engineer Kalebelo, alifika na timu ya Wizara pale na wakazungumza na Mkandarasi na wakampa mikakati mpaka sasa asilimia 60 ya mradi umeshakamilika na wananchi wa Mpera gwasi na Nsanga sasa hivi wanapata maji safi na salama na ya kutosheleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, sisi kama Wizara ya Maji tutahakikisha tunausimamia mradi ule kwa dhati kabisa ili uweze kukamilika na vijiji takribani 15 vilivyopangwa kunufaika, viweze kunufaika na mradi wa maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la pili, Mheshimiwa Mbunge hii ni wiki ya pili ananiulizia swali la maji katika Jiji la Mbeya. Nataka nikuhakikishie, ukimwona mtu mzima analia, ujue kuna jambo. Hivyo, katika wiki ya kwanza tuna maswali mawili katika Jiji la Mbeya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, nipo tayari sasa kukutana na wataalam wetu wa Jiji la Mbeya kwa maana ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Jiji la Mbeya ili tujipange ni namna gani tunaweza tukapeleka maji kwa haraka katika maeneo ambayo ameyasema ya Ilomba, Iganzo, Iyumba, Ghana na Iganjwa.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. DKT. TULIA ACKSON (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:- Wilaya ya Rungwe ina vyanzo vingi vya maji ambavyo vinatiririsha maji. Je, ni lini Serikali itarekebisha miundombinu ili kuongeza kiwango cha maji ambayo kwa sasa hayatoshi kiasi cha kufanya Idara ya Maji kufunga baadhi ya maeneo kama vile Vijiji vya Ibungila, Lubiga na kadhalika?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na kuishukuru Serikali kwa mradi wa maji wa Ziwa Victoria na mradi wa visima 25 katika Jimbo la Nzega, sasa nilitaka nimwombe Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza kutupatia commitment Halmashauri ya Mji wa Nzega kupatiwa fedha kiasi cha shilingi bilioni 1.2 katika mwaka wa fedha unaokuja ili kukamilisha mradi wa maji katika Vijiji vya Mhogola, Monyagula, Migua, Itangili, Igilali, Mwanzoli na Kitengwe?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, labda kifupi kwanza, nimpongeze Mbunge, kaka yangu Mheshimiwa Hussein Bashe, kwa kazi kubwa anayoifanya katika Jimbo lake la Nzega, lakini kubwa tunatambua utekelezaji wa miradi ya maji inategemeana na fedha, nimwombe basi tukutane mimi na yeye, pamoja na Wataalam wetu wa Wizara, tuangalie namna gani tunaweza tukasaidiana. Ahsante sana.