Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Gereza katika Wilaya ya Chunya?

Supplementary Question 1

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Serikali imetoa majibu kitaalam sana na Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri mwenyewe kwamba uwepo wa gereza mahalI unapunguza gharama za usafiri, unaharakisha uendeshaji wa kesi, vilevile unapunguza msongamano magerezani ambao ni kubwa sana kwa sasa. Pamoja na majibu hayo mazuri, nina maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, Chunya ni Wilaya kongwe sana hapa nchini. Katika Wilaya tatu kongwe Chuya imo, mwaka huu inatimiza karibu miaka 80. Je, rasilimali fedha itakapopatikana Mheshimiwa Waziri ananihakikishia kwamba ataipa Chunya kipaumbele kujenga gereza Wilayani?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika kipindi cha mpito kabla ya kujengwa kwa gereza hilo, je, Serikali ipo tayari kujenga walau chumba, siyo gereza, chumba cha mahabusu ili kuweza kupunguza gharama hizi ambazo Serikali imezisema?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mhehimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Victor Mwambalaswa, Mbunge wa Rukwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba pale bajeti itakapokaa vizuri Chunya itakuwa eneo la kipaumbele. Kwanza, nichukue fursa hii kumpongeza yeye binafsi kwa kushirikiana na wananchi wa eneo hilo kuanza mchakato ambao unaendelea wa ujenzi wa bweni moja na jengo la kuishi Askari ambao umefikia 90%.

Mheshimiwa Spika, ni matarajio yetu kwamba litakapokamilika kwa 100% tutaanza kupeleka wafungwa na kuanzisha kambi ambapo wafungwa hao tutawatumia kwa ajili ya kufyetua matofali ikiwa ni maandalizi ya ujenzi wa gereza. Wakati tunasubiri bajeti ikae vizuri Serikali tutaunga mkono nguvu hizo kwa kuhamasisha wafungwa na kutumia rasilimali zilizopo Chunya ili tuweze kutatua tatizo hili angalau kwa kuanzia gereza la mahabusu ili kupunguza msongamano.

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Gereza katika Wilaya ya Chunya?

Supplementary Question 2

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Katika majibu yake Mheshimiwa Naibu Waziri amesema ujenzi wa magereza katika maeneo mbalimbali vilevile utasaidia kupunguza msongamano wa mahabusu. Pia amesema kuwa ujenzi huo kwa sasa unakwamishwa na uhaba wa rasilimali.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ujenzi huu hauwezi kuendelea kwa haraka kwa sasa; na kwa kuwa kuna msongamo mkubwa wa mahabusu katika magereza mbalimbali kutokana na kubambikiziwa kesi ama mashtaka yasiyokuwa na dhamana na hukumu ambazo kimsingi zinajaza tu magereza yetu, je, Serikali ipo tayari sasa kutekeleza operesheni maalum ya kupunguza mahabusu katika magereza mbalimbali nchini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mhehimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa John Mnyika, Mbunge wa Ubungo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nirekebishe kauli yake si kwamba msongamano wa mahabusu chanzo chake kikubwa ni ubambikiziwaji wa kesi. Tunajua tuna changamoto ya ubambikiziwaji wa kesi na pale ambapo tunabaini na tumekuwa tukifanya kazi hiyo ya kuhakikisha wale ambao wanahusika na upambikaji kesi wanachukuliwa hatua za kisheria.

Mheshimiwa Spika, lakini msongamano wa mahabusu unatokana na changamoto za uhaba wa magereza. Magereza yetu yamejengwa muda mrefu na idadi ya watu inaongezeka na changamoto ya uhalifu inasababisha msongamano huu pia kuongezeka. Hata hivyo, Serikali tumefanya jitihada mbalimbali za kuhakikisha kwamba tunapunguza msongamano huu.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali lake kuhusu operesheni, hivi tunavyozungumza tuna utaratibu wa kamati za kuharakisha kesi ambazo zinahusisha wadau mbalimbali ambapo wanahakikisha wale ambao wanatakiwa dhamana kwa haraka wanasikilizwa. Vilevile, tumekuwa tukitumia sheria zetu mbalimbali, kwa mfano, Sheria ya Bodi ya Parole, Sheria ya Huduma za Jamii, Sheria ya EML na msamaha Mheshimiwa Rais ambao amekuwa akitoa kila mwaka, yote haya yanasaidia kupunguza msongamano wakati Serikali ikiendelea na jitihada zake za kujenga mabweni na kuongeza na kupanua idadi ya magereza yetu ili yaweze kuchukua idadi kubwa zaidi ya wafungwa.

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Gereza katika Wilaya ya Chunya?

Supplementary Question 3

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2014 Serikali ilitenga eneo la hekari zaidi ya 30 katika Kata ya Ushokora kwa ajili ya kujenga Gereza la Wilaya lakini kwa miaka sita (6) sasa wananchi wa Pozamoyo pale Ushokora hawajawahi kuambiwa chochote na waliondolewa kwenye makazi na mashamba yao wameenda kujibanza kwenye maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango gani sasa angalau kufidia wananchi wale iliyowahamisha pale ambao wamepanga maeneo mbalimbali waweze kwenda kutafuta makazi sahihi na wakati huo huo Serikali iweze kujenga hilo gereza maana ni muda mrefu sasa? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mhehimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Magdalena Sakaya, Mbunge wa Kaliuwa na Naibu Katibu Mkuu mpya wa Chama cha CUF, kama ifuatavyo:- (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama nimeelewa vizuri swali lake anazungumzia wananchi ambao wametakiwa kuhamishwa kwa ajili ya ujenzi wa gereza na ambao pengine anadhani wanahitaji kulipwa fidia. Kama hivyo ndivyo kwa sababu swali lake hili ni mahsusi naomba nilipokee na tuweze kulifanyia kazi na nitampatia mrejesho.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Gereza katika Wilaya ya Chunya?

Supplementary Question 4

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kama ilivyo kwa Wilaya ya Chunya, Wilaya ya Kyela haina mahabusu ya wanawake hivyo kupelekea kupelekwa Wilaya ya Rungwe. Je, ni lini Serikali itajenga mahabusu ndogo ya wanawake kwa Wilaya ya Kyela?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimezungumza kwamba changamoto inayosababisha tusiwe na ujenzi wa magereza yetu ambao siyo wa kasi kubwa sana ni kutokana na ufinyu wa bajeti. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Gereza la Wanawake Kyela ni miongoni mwa maeneo ambayo tunayaangalia kwa jicho la kipaumbele sana. Kwa hiyo, pale ambapo bajeti itakaa vizuri Gereza la Wanawake Kyela litakuwa ni jambo la kipaumbele.