Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI aliuliza:- Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa hupata posho shilingi elfu ishirini kwa mwezi kiasi ambacho ni kidogo ikilinganishwa na kazi kubwa wanayoifanya:- Je, ni lini Serikali itaongeza posho kwa Wenyeviti hao?

Supplementary Question 1

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi mara ya pili kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, Wenyeviti wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji hawana ofisi za kufanyia kazi. Je, ni lini Serikali itawajengea ofisi za kufanyia kazi?

Mheshimiwa Spika, Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa wana wajumbe wanaosaidiana nao katika kazi za utendaji wa kazi za kila siku. Je, ni lini Serikali itawapa posho wale wajumbe?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS – TAMISEMI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru naomba ku-declare kwamba mimi pia ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa mstaafu. Naomba nimjibu Mheshimiwa Mbunge maswali yake mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza anaulizia kuhusu Ofisi za Serikali za Mitaa. Sasa hivi tunaenda kwenye Bunge la Bajeti na mpango wa kujenga ofisi za mitaa, vijiji na vitongoji ni mpango wa halmashauri husika. Kwa hiyo kama kuna upungufu mkubwa, tunatarajia kwamba halmashauri hizo na vijiji watakuwa wameweka kwenye bajeti yao ili waweze kuleta kwenye Bunge lako Tukufu iweze kupitishwa na waweze kujenga ofisi hizo.

Mheshimiwa Spika, swali la pili anaulizia juu ya posho, kama nilivyojibu kwenye swali langu la msingi ni kwamba posho za wenyeviti na wajumbe wao zinapatikana kwenye halmashauri husika kulingana na vipato vyao. Kwa hiyo kama kuna sababu ya kulipa posho tofauti na ilivyo kwa Wenyeviti wa Mitaa hili nalo pia lilifanyiwa kazi kwenye ngazi ya chini ya halmashauri husika kulingana na mapato yao, kama wana uwezo wataendelea kuwalipa.

Hata hivyo, sifa ya msingi ya kugombea kama ilivyo kwenye uchaguzi mwezi wa Kumi wajumbe hawa na Wenyeviti wa Mitaa, Vitongoji na Vijiji wanajua wanapaswa kufanya kazi ya kujitolea. Kwa hiyo tunatarajia kwamba watafanya kazi kama ambavyo waliamua kugombea na kupata nafasi hizo kama kuna uwezo wa posho watalipana, kama haupo wafanye kazi kama ambavyo waliamua kugombea nafasi hizo.