Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Serikali inajitahidi sana kukabiliana na tatizo la maji katika Manispaa ya Morogoro, lakini tatizo hilo lipo kwenye baadhi ya Kata:- Je, Serikali ina mikakati gani ya makusudi ya kumaliza tatizo hili katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nashukuru sana kwa majibu ya Naibu Waziri, ni kweli muda mfupi umeanza ambao ni mzuri sana, ambao wanaweza wakatoa maji kwenye kata mbalimbali, lakini kuna Kata ya Magadu ambao waliahidiwa maji, ambao hakuna maji kabisa na ilikuwa wachimbiwe kisima cha muda mfupi angalau waweze kupata maji, lakini mpaka sasa hivi Kata ya Magadu wana shida sana ya maji. Je, ni lini wataweza kupatiwa hicho kisima au kuchimbiwa maji wakaweza wakapata maji?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, mradi huu ambao unafadhiliwa kwa Euro milioni 70 umechukua muda mrefu na tukiwa tunasubiri kwa muda mrefu wa miaka zaidi ya mitatu sasa tunaambiwa kuwa imebaki kusainiwa; je, kwa sababu wananchi wa Morogoro Manispaa wanategemea maji yao kutoka bwawa la Mindu, kuna mkakati gani wa muda mfupi ambao Serikali inaweza ikafanya kukarabati bwawa la Mindu?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, mama yangu, Mheshimiwa Christine Ishengoma, kwa kazi kubwa ambayo anaifanya katika kuhakikisha anawasemea wananchi wake wa Mkoa wa Morogoro. Kubwa ni kuhusu suala zima la maji katika Kata ya Magadu. Nimuagize tu Mhandisi wa Maji wa Mkoa, sisi ni Wizara ya Maji, siyo Wizara ya ukame, ahakikishe anasimamia suala hili la uchimbaji wa kisima wananchi wa Magadu waweze kupata maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala zima la mradi huu mkubwa wa Euro milioni 70. Tunapozungumzia maji, ni rasilimali muhimu sana, lakini sasa hivi Morogoro kumekuwa na uhitaji mkubwa sana, uzalishaji wetu sisi ni lita milioni 30 lakini kutokana na ongezeko la watu pamoja na taasisi na viwanda, kumekuwa na uhitaji wa zaidi ya lita milioni 59 na ndiyo maana sisi kama Serikali tukaona haja sasa ya kuwekeza kwa maana ya kuongeza bwawa la Mindu, katika kuhakikisha kwamba linakuwa na uzalishaji mkubwa ili wananchi wa Morogoro waweze kupata maji safi, salama na kuweza kukuza uchumi wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kilio hiki cha muda mrefu, lakini kubwa nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, utekelezaji wa miradi ya maji unategemeana na fedha, kwa hiyo, pamoja na utoaji huu wa fedha lazima tufuate utaratibu. Nataka nimtie moyo kwamba wawe na subira, subira yavuta heri na heri itapatikana katika upatikanaji wa maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Serikali inajitahidi sana kukabiliana na tatizo la maji katika Manispaa ya Morogoro, lakini tatizo hilo lipo kwenye baadhi ya Kata:- Je, Serikali ina mikakati gani ya makusudi ya kumaliza tatizo hili katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Jimbo la Rombo lina shida kubwa sana ya maji, pamoja na hayo Serikali ina jitihada inazofanya kama za kupata maji katika Ziwa Chala, kupanua lile bomba kubwa linalotoa maji Marangu kuleta Rombo na kadhalika. Hata hivyo, shida hii inakuzwa sana na jinsi KILIWATER (Taasisi ya Wananchi) inavyogawa maji kule Rombo, inagawa kwa upendeleo, inagawa kwa baadhi ya watu, haifungii watu mita na kadhalika. Baraza la Madiwani…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Selasini uliza swali tafadhali.

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Sasa kwa kuwa tulishaazimia taasisi hii iondolewe na Serikali ilishakubali; je, Mheshimiwa Naibu Waziri, yuko tayari kwa muda wake twende Rombo ili akakague shughuli za hii taasisi na kuipa amri ya kugawa maji kwa haki wakati hizo hatua nyingine zikiendelea kuchukuliwa na Serikali?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri, lakini kubwa tunapozungumzia suala la maji, maji ni uhai na maji hayana mbadala na hakuna sababu ya kutoa maji kwa upendeleo. Nimwahidi niko tayari kuongozana na yeye katika kuhakikisha kama ipo changamoto hiyo tuweze kuitatua kwa haraka ili wananchi wa Jimbo la Rombo waweze kupata maji safi na salama. Ahsante sana.

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Serikali inajitahidi sana kukabiliana na tatizo la maji katika Manispaa ya Morogoro, lakini tatizo hilo lipo kwenye baadhi ya Kata:- Je, Serikali ina mikakati gani ya makusudi ya kumaliza tatizo hili katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza, pamoja na shukrani nyingi za wananchi wa Bagamoyo kwa Serikali kwa kuwajengea tanki kubwa la maji lita milioni sita Bagamoyo Mjini, naomba kuuliza swali la nyongeza kwamba, sasa ni lini shughuli ya mradi wa kusambaza au kulaza mabomba, mtandao huu mpya wa mabomba ya maji katika Mji wa Bagamoyo na Kata zinazozunguka Mji wa Bagamoyo utaanza kwa sababu tanki lile sasa hivi halileti tija ya kutosha kwa wananchi wa Bagamoyo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua changamoto kubwa sana ya maji katika eneo la Dar es Salaam pamoja na Pwani kwa maana ya Bagamoyo, Serikali imewekeza zaidi ya dola milioni 32 katika kuhakikisha wananchi wa maeneo haya wanapata maji. Nimhakikishie, hii ni hatua ya kwanza na tunamwagiza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Salama Dar es Salaam kuhakikisha mradi huu unaanza haraka ili wananchi wa Bagamoyo waweze kupata maji safi na salama.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Serikali inajitahidi sana kukabiliana na tatizo la maji katika Manispaa ya Morogoro, lakini tatizo hilo lipo kwenye baadhi ya Kata:- Je, Serikali ina mikakati gani ya makusudi ya kumaliza tatizo hili katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 4

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na jitihada nzuri za Serikali kuwapatia wananchi maji, kuna mradi mmoja wa KfW wa tangu mwaka 2008 ambao ulikuwa uhudumie Mikoa saba ya Manyara, Babati, Mtwara, Kigoma, Lindi na maeneo mengine. Mikoa mingine mitano ilishapatiwa huduma ya maji bado Babati na Mtwara na tulikuwa tumepangiwa shilingi bilioni 20 na kila mkoa shilingi bilioni 10. Mpaka sasa mradi huu haujasainiwa na wenzetu wa Ujerumani pamoja na Serikali ya Tanzania. Naomba nifahamu ni lini mradi huu sasa utasainiwa kwa sababu tunahitaji hizo shilingi bilioni 10 zitusaidie kuondoa tatizo la maji Babati na Mtwara ambako kumesalia.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge wa Babati na mimi nilishafika Babati pamoja na huu mradi mkubwa lakini zipo jitihada pale za utekelezaji wa mradi wa maji. Nataka nimhakikishie, kama tulivyoahidi tutatekeleza lakini tutalifanya hili jambo kwa haraka ili wananchi wake wa Babati waweze kupata maji safi na salama. Ahsante sana.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Serikali inajitahidi sana kukabiliana na tatizo la maji katika Manispaa ya Morogoro, lakini tatizo hilo lipo kwenye baadhi ya Kata:- Je, Serikali ina mikakati gani ya makusudi ya kumaliza tatizo hili katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyo Morogoro naishukuru sana Serikali kuona tatizo la Mji Mkuu wa Wilaya ya Hanang na kuweza kuwapangia zaidi ya shilingi bilioni 2. Naomba kuuliza naona kama speed ni ndogo, je, mradi ule utafikisha maji kata 20 kwa sababu wanachotaka kuona wananchi wanakunywa maji na wanatumia maji.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge mama yangu Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu, maeneo yenye changamoto kubwa sana ni katika jimbo lake lakini sisi kama Serikali tuna mradi mkubwa sana pale ambao tumeuwekeza kwa ajili ya kutatua tatizo la maji Hanang. Nataka nimhakikishie sisi kama Wizara na viongozi wa Wizara hii tunamwagiza mkandarasi lazima afanye kazi usiku na mchana, kama atashindwa kufanya kazi ile kwa haraka sisi tutamwondoa tutamweka mkandarasi ambaye anaweza kufanya ile na kuweza kukamilisha mradi kwa mujibu wa mkataba kama ulivyopangwa. Ahsante sana.