Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa shamba la Efatha Mkoani Rukwa?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsnate sana. Tangu alipouziwa hilo shamba, leo ni miaka 12, lakini mpaka leo hajaendeleza hata ekari moja, imekuwa ni shamba pori na kusababisha vijiji vilivyozunguka hilo shamba vya Sikaungu, Songambele na Msanda Muungano kukosa sehemu ya kulima. Mkoa wa Rukwa, wananchi wote wanategemea kilimo, sasa kwa nini wanasitasita wasimpelekee Mtukufu Rais kulifyekelea mbali hili shamba, kulifuta kama alivyofuta mashamba mengine?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Hilo shamba linamilikiwa na Halmashauri ya Sumbawanga DC na Manispaa. Cha ajabu, vigezo gani vilitumika, mkataba uliingia peke yake na Manispaa ya Sumbawanga kuuza hilo shamba bila Manispaa ya Sumbawanga DC kushirikishwa?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Keissy kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la ufutaji mashamba halianzii kwenye Wizara ya Ardhi, suala la ufutaji mashamba kama halijaendelezwa wahusika wa kwanza ni zile mamlaka zenyewe za upangaji miji katika maeneo yao. Kwa hiyo, kama wao waliona kwamba hili shamba pengine halijakidhi vigezo, linatakiwa kufutwa, walitakiwa wao walete mapendekezo hayo kwa Waziri na Waziri angemshauri Mheshimiwa Rais kulifuta.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama hiyo haitoshi, walikuwa pia na mgogoro naye na walipelekana Mahakamani. Halmashauri yenyewe husika ikatoa shauri Mahakamani na wakakubali ku-settle nje ya court. Kwa hiyo, sisi kama Wizara hatuwezi kuingilia makubaliano yao. Kwa hiyo, kama bado wanaona hajaendeleza, basi warudi tena wao wachukue maamuzi kama waliyokuwa wamechukua mwanzoni ya kuchukua hatua. Wakileta, sisi tutashughulikia vinginevyo itakuwa kidogo ni tatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili anaongelea kwamba shamba lile linaingia katika Halmashauri mbili; nadhani katika ziara yangu niliyofanya mwaka 2017 suala hili nililipata na nililitolea maelekezo. Nilisema kama pale ambapo unakuta shamba la mwekezaji limeingia katika Halmashauri mbili tofauti, ni jukumu la Halmashauri husika kuzungumza naye kuweza kuona ni namna gani Halmashauri zote mbili zitafaidika na mwekezaji huyo kama ameingia katika maeneo yao. Sasa sisi kama Wizara hatuwezi kuwapangia namna ya kukubaliana, kwa sababu ni mazungumzo kati ya mwenye eneo na mwenye mamlaka ya upangaji miji na yule mwekezaji aliyeko katika eneo lao. Kama itashindikana, wanahitaji ushauri kutoka Wizarani, tuko tayari kuwasaiia kwa suala hili.

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa shamba la Efatha Mkoani Rukwa?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nami niulize swali dogo la nyongeza. Kumekuwa na migogoro ya muda mrefu sana katika Jimbo la Mikumi, hasa kwenye Kata ya Kilangali kati ya wananchi na SumaGrow; Kata ya Masanze kati ya Miyombo Estate na wananchi; Kata ya Tindiga kati ya Mauzwi Estate na NARCO na wananchi lakini pia Kata ya Kisanga Estate na wananchi pamoja na WEDO na Stignati:-

Je, Serikali imejipanga vipi kumaliza migogoro hii ambayo ipo katika Jimbo la Mikumi ambayo kwa kweli inahatarisha sana maisha ya wananchi wa Jimbo la Mikumi?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, migogoro hii ameileta hapa na hatujajua wao wenyewe wamefikia wapi. Kwa sababu migogoro mingi Wizara inaingilia kati pale ambapo Halmashauri inakuwa imeshindwa. Mheshimiwa Mbunge amezungumza ni migogoro ya muda mrefu lakini katika ile migogoro ambayo tuko nayo mgogoro anaotaja hatuko nao.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwahidi tu kwamba kama kuna migogoro kati ya wawekezaji na kata alizozitaja, basi tuko tayari kusaidiana nao kuitatua ili mradi tu tuweze kujua wao wenyewe wamefikia wapi. Kwa sababu mazungumzo lazima yaanzie kwenye eneo husika. Wizara haiwezi kuingia moja kwa moja mpaka ijue wapi wamekwama. Hatujalipokea na wakilileta tutalifanyia kazi.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa shamba la Efatha Mkoani Rukwa?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza. Matatizo yaliyoko huko kwenye Shamba la Efatha Mkoa wa Rukwa yanafanana kabisa na matatizo yaliyoko katika Halmashauri ya Itigi shamba lililokuwa linamilikiwa na shirika ambalo limekufa la Tanganyika Packers. Serikali haitoi tamko la moja kwa moja, liko chini ya Msajili wa Hazina, lakini hakuna mwekezaji aliyejitokeza hadi leo hii.

Je, Serikali imekubali sasa kulirudisha shamba hili kwa wananchi kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Itigi?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli suala analolizungumzia Mheshimiwa Massare ni la muda mrefu, lakini naomba tu nimpe uhakika kwamba masuala yote ambayo yanasimamiwa na Msajili wa Hazina alishaanza kuyapitia na kuweza kuona mashamba yale au uwekezaji ambao ulikuwepo na ukakwama uko chini ya Hazina sasa hivi, anapitia shamba moja baada ya lingine na akishakamilisha basi anaweza kutoa nini kitawezakufanyika. Hatuwezi kusema sasa hivi kwamba tunalirudisha kwa wananchi wakati Msajili wa Hazina bado anafanyia kazi mashamba hayo.