Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. PROF. NORMAN A. SIGALLA KING) aliuliza:- Kumekuwa na maandalizi ya kuzalisha umeme katika Mto Lumakali uliopo Balogwa Makete na ni miaka 11 sasa wananchi wanaendelea kusubiri ambapo mwaka 2015/2016 Serikali ilitoa kauli kwamba ujenzi huo ungeanza mwaka 2017. Je, ni lini Serikali itaanza kujenga bwawa hilo kwa ajili ya kuzalisha umeme?

Supplementary Question 1

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri na kazi nzuri ambayo Wizara ya Nishati na Madini inafanya, sasa naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu ulianza toka mwaka 1998, mpaka leo ni takribani miaka 20. Namwomba Mheshimiwa Naibu Waziri, kama atakuwa tayari sasa kuambatana na Mheshimiwa Profesa Norman King Sigalla ili kwenda kujionea mwenyewe hali inayoendelea ili wananchi wa Makete ambako kumekuwa na matatizo mengi kule yanatokea na barabara hawana, waweze kuwa na imani na Serikali yao.

Swali la pili linalohusu umeme; kwa kuwa kilio na hamu ya Watanzania ni kuona umeme unapita kila sehemu: Je,
sasa, Mheshimiwa Naibu Waziri aliwahi kutoa ushauri kwamba sehemu ambako kuna miradi mikubwa na hakuna umeme, umeme uweze kupelekwa; kikiwepo Kijiji cha Iyai, ambako Mheshimiwa Naibu Waziri ulifika, Kijiji cha Kising’a, Winome, Nyanzwa, Ilindi, Msosa, Kitimbo na Ikula? Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha hizo ambazo ilitoa ahadi yenyewe umeme unafika ili wananchi wale waweze kupata umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ya Mheshimiwa Mwamoto ameuliza kwa niaba ya Mheshimiwa Profesa Norman, kwamba ni lini nitakuwa tayari kutembelea Jimbo la Makete? Nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba tulifanya ziara Jimbo la Makete mwaka 2018 mwezi Desemba. Katika mambo mbalimbali ambayo nilishuhudia ni uwepo wa uhitaji wa umeme, lakini uwepo wa vyanzo vingi vya kuzalisha umeme hususan vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana Serikali kupitia agizo la Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, kwamba sasa mchakato wa ujenzi wa bwawa la Lumakali uanze na kwa hatua za awali tumepata mfadhili ambaye ni World Bank ambaye ana-support hatua hizi za kurudia tena upembuzi yakinifu kwa sababu ulichukua muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimthibitishie tu Mheshimiwa Mbunge kama jibu langu la msingi lilivyosema, kwamba mradi huu utaanza kama ilivyokusudiwa, mapema mwezi Januari, 2021, kwa sababu Serikali ina dhamira ya dhati ya kuongeza uzalishaji wa umeme kupitia chanzo hiki cha maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, Mheshimiwa Mbunge ameyataja maeneo. Ni kweli tumefanya ziara katika Jimbo la Kilolo zaidi ya mara tatu. Mwezi Machi, 2018, mwezi Novemba, 2018 na hivi karibuni tulikuwa na Kamati ya Bunge katika Jimbo lake katika maeneo ya Dinganayo, Ikuvala, lakini maeneo hayo pia tumewasha umeme na wiki hii tutawasha umeme katika maeneo ya Ngelango, Itungi na Mlavu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ameeleza jambo la msingi, kwamba kwa kuwa Serikali tulitoa maelekezo, maeneo yote ambako miradi hii ya umeme vijijini yanaunganishiwa, taasisi za Umma na hasa maeneo ya viwanda yapewe kipaumbele. Naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge, mara baada tu ya kujibu swali hili, naomba tukutane naye, tuelekee ofisini tuone namna ya kufuatilia na kwa kuwa amekuwa mfuatiliaji mzuri sana wa miradi ya nishati vijijini na hasa hili eneo la viwanda ambalo amelitaja, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, kabla ya mwaka huu wa fedha haujaisha, eneo hilo litakuwa limepatiwa umeme ili wananchi wale wapate ajira na pia Serikali ipate mapato kupitia vile viwanda. Ahsante sana.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. PROF. NORMAN A. SIGALLA KING) aliuliza:- Kumekuwa na maandalizi ya kuzalisha umeme katika Mto Lumakali uliopo Balogwa Makete na ni miaka 11 sasa wananchi wanaendelea kusubiri ambapo mwaka 2015/2016 Serikali ilitoa kauli kwamba ujenzi huo ungeanza mwaka 2017. Je, ni lini Serikali itaanza kujenga bwawa hilo kwa ajili ya kuzalisha umeme?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza nafasi kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la umeme limekuwa na kasi na hali ni mbaya katika Jimbo la Mbulu Vijijini na Mheshimiwa Naibu Waziri amefika na vile vijiji alivyoahidi mpaka sasa umeme haujapatikana: Je, atatusaidiaje angalau umeme uweze kupatikana kwenye vijiji alivyoahidi Mbulu Vijijini?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nilitaarifu Bunge lako, kwamba miradi inayoendelea ya kupeleka umeme vijijini, miradi hii inachukua miezi 24. Kwa mujibu wa taratibu na kwa kuwa hizi LC (Letter of Credit) zilifunguliwa mwezi wa Saba mwaka 2018, naomba niwatie moyo Waheshimiwa Wabunge kwamba tunao muda wa kutekeleza huu mradi na kasi inaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Flatei amekuwa mfuatiliaji mzuri, msimamizi mzuri, nimeshafanya ziara kwenye Jimbo lake, Mheshimiwa Waziri ameshaenda, tutamsimamia karibu Mkandarasi ambaye anafanya mradi katika maeneo hayo na miradi itakamilika kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.