Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza:- Kituo cha afya Kisesa kiliombewa kibali ili kipandishwe hadhi kuwa Hospitali kamili:- Je, ni lini Serikali itatoa kibali?

Supplementary Question 1

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Kwa kuwa Kituo hiki cha Afya kinahudumia maeneo makubwa katika eneo la Ilemela, Usagara Wilaya ya Misungwi, pamoja na Jimbo la Sumve na ni Kituo cha Afya ambacho kiko highway, wakati wowote watu wanapata matatizo wanaposafiri wanahitaji huduma hii kubwa. Kwa kuwa sera ya mwaka 2007 ni kama imepitwa na wakati ukilinganisha na mazingira:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kubadilisha ili angalau kulingana na mazingira ya Kituo hiki cha Afya cha Kisesa, kiweze kupandishwa hadhi na kuwa hospitali ya wilaya ili kiweze kuhudumia maeneo makubwa?
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
6
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali iko hatua za mwisho, mkataba wa kujenga jengo la X-ray, jengo la upasuaji, limeanza mwaka 2013. Kama ni hatua za mwisho, leo ni miaka mitatu. Serikali haioni kwamba hii ni aibu, miaka mitatu inajenga majengo haya bila kukamilika na yanasubiri tu shilingi milioni 77 ili yaweze kukamilika? Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kuniambia hizi shilingi milioni 77 zikipatikana hata kesho ili huduma hizi zianze kutolewa, yuko tayari kunipa fedha hizi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikiri wazi, kituo cha Kisesa, junction yake ukiiangalia na ukubwa wake sasa hivi wa population ya pale, kweli ni eneo ambalo lina-capture watu wengi sana. Ukiangalia hata Kata jirani wanategemea sana Kituo cha Afya cha Kisesa. Kubwa zaidi, kwa mujibu wa sera siwezi kusema hapa kwamba tutabadilisha sera hii, kwa sababu nyie mnafahamu, lengo letu ni kuzifikia kila Halmashauri kupata hospitali za wilaya. Hivi sasa mnaona tuna deficit na tunaenda kwa kasi ili mradi angalau sasa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tuna wilaya zipatazo 139 na Halmashauri 181. Lengo letu ni kwamba kila Wilaya angalau ipate hospitali ya wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu kubwa ni kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi, tutafanya juhudi kituo hiki kiweze kukamilika na suala la upasuaji liweze kuendelea na huduma nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili ni kwamba, X-ray kwa muda mrefu imesuasua katika kituo hiki. Kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa sababu yeye alikuwa ni Mwenyekiti wa Halmashauri hii ya Magu ambayo naizungumza hivi leo. Kwa hiyo, hata mambo yanayoendelea huko, naye alichangia kwa kiwango kikubwa mpaka kufanikisha ujenzi huo unaendelea, naye anajua wazi tunaendaje. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mikakati iliyofanyika katika hicho kituo, sasa hivi tuko katika hali ya mwisho. Kwa sababu najua juhudi ya Mheshimiwa Mbunge aliyokuwa anaifanya hata nilipokuwa Jimboni kwake kule mwezi wa Kwanza katika harakati kubwa za kuboresha huduma ya afya hiyo na hata alikuwa anaomba hata ingewezekana watu walioasisi mifumo mizuri ya afya, Dkt. Pembe arudi Magu kwa ajili ya kuhakikisha afya inakwenda vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo kubwa ni kuhakikisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI kama tulivyofanya mawasiliano na Mkurugenzi kule, tutaweka nguvu ili ikifika mwezi wa Sita jengo lile liweze kukamilika na wa Kisesa waweze kupata huduma kama ilivyokusudiwa.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza:- Kituo cha afya Kisesa kiliombewa kibali ili kipandishwe hadhi kuwa Hospitali kamili:- Je, ni lini Serikali itatoa kibali?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa upandishaji hadhi wa vituo vya afya nchini umekuwa na urasimu sana kwa sababu vibali lazima vitolewe na Serikali Kuu: Je, Serikali sasa haioni kwamba kuna umuhimu wa upandishaji hadhi wa vituo tu vya afya ukarudi kwenye Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kuliko kusubiri iende Serikali Kuu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kuna jambo moja hapa, kwa sababu katika mchakato wa upandishaji wa vituo vya afya, siyo Serikali tu inaamua. Jukumu kubwa ni kuhakikisha kwamba kuna vikao halali ambavyo vinakaa na mwisho wa siku yale maamuzi yote yaliyopitishwa mpaka katika Baraza la Madiwani yanakwenda Wizara ya Afya. Baadaye wakaguzi wanakuja kuangalia na mwisho kile kituo kinapandishwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima kurudisha katika Serikali za Mikoa; katika Mikoa kwa mujibu wa sera za afya, tuna Wakaguzi wa Kanda za Afya. Ni kwa nini zinafika mpaka Wizarani? Lengo ni kupata wataalam ambao watahakikisha quality control inafanyika na kituo kile kinakidhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni mawazo mazuri, huko mbele au siku za usoni tutaangalia ni jinsi gani tutafanya, ikiwezekana katika ku-decentralize, tukaweka timu za kufaa katika ngazi za mikoa ambapo wakati mwingine tunaweza tukafanya jambo hilo likaendeshwa katika huko, lakini kwa sasa hivi huo ndiyo utaratibu, lakini wazo ni zuri, huko siku za usoni inawezekana tukalifanyia kazi.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza:- Kituo cha afya Kisesa kiliombewa kibali ili kipandishwe hadhi kuwa Hospitali kamili:- Je, ni lini Serikali itatoa kibali?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Vituo vya Afya vya Mwese, Karema na Mishamo ni vituo ambavyo vinahudumia wananchi wengi kwenye Jimbo la Mpanda Vijijini. Vituo hivi havina huduma ya kimsingi ya wataalam na hasa suala zima la ambulance. Naomba kujua, Mheshimiwa Naibu Waziri atavisaidia vipi hivi vituo vya afya ambavyo vinahitaji huduma ya Serikali ili kuokoa maisha ya wananchi kwenye Jimbo hilo?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Kakoso kama ifuatavyo:-
Ni kweli kwamba yako mahitaji ambayo hayatoshelezi katika vituo vyetu vya afya na hospitali zetu, lakini hospitali hizi zipo kwenye Halmashauri na Halmashauri ndizo hupanga bajeti zake za kila mwaka.
Sasa nawaomba sana Waheshimiwa Wabunge, sehemu ya kuanzia katika kukamilisha huduma mbalimbali katika Sekta ya Afya, iwe ya elimu, mipango yote inaanzia kwenye Halmashauri. Kama watakuwa waliweka kwenye bajeti zao, basi wanaweza wakapata hizo ambulance na vifaa ambavyo pengine vina upungufu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, sisi kwa sasa hatuna mpango mahsusi wa kununua magari ya ambulance kwa nchi nzima kwa sababu, upungufu ni mkubwa, isipokuwa tunaangalia kutokana na bajeti zao za Halmashauri na sisi Serikali kwa fedha iliyopitishwa tutakuwa tumewatengea na kuwapatia fedha hizo kwa kadiri walivyoomba katika bajeti zao.