Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. BALOZI. DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:- Mto Kagera ni chanzo muhimu kinachoweza kusaidia upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wanaopakana nao:- Je, kwanini Serikali isifanye utaratibu wa kuvuta maji hayo ili yawasaidie wakazi wa maeneo hayo?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri na ninashukuru pia kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na Waziri wake na Katibu Mkuu wake. Ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Waziri anafahamu kwamba alituma wataalam kule Kata ya Kanigo, Kata ya Kashenye, Kata ya Ishozi na Kata ya Ishunju kwa ajili ya maandalizi ya awali ya kutumia maji ya Ziwa Victoria. Je, yuko tayari kuharakisha jitihada hizo ili maji hayo yaanze kutumika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali dogo la pili. Kwa kuwa Wilaya ya Misenyi tumebarikiwa kuwa na mito mingi; tunao Mto Kagera pamoja na Mto Nkenge na mingine: Je, mradi kama huu ambao uko mbioni kuanza kama Mheshimiwa alivyojibu katika maeneo ya Kyaka na Bunazi, atakuwa tayari kubuni mradi kama huo katika maeneo yaliyo karibu na Mto Nkenge?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nitumie nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya. Nilifika katika Jimbo lake, nimeona kazi kubwa zinazofanyika katika eneo lile. Kubwa ambalo ninalotaka nimhakikishie, sisi kama Wizara ya Maji ambayo siyo Wizara ya ukame, tumeona haja kwamba haina budi na kwamba haiwezekani tuone kabisa vijiji ama Miji ambayo iko karibu na mito mikubwa ama maziwa wakose maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tuna vyanzo vya uhakika, ndiyo maana tumewatuma wataalam wetu waweze kwenda katika eneo lile ili tuweze kubuni mradi na wananchi wake waweze kupata majisafi na salama na yenye kuwatosheleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala zima la ku- design katika Mto Nkenge; uwepo wa chanzo unatupa nafasi kama Wizara ya Maji katika kuhakikisha tunabuni miradi mikubwa ili tuweze kuwapatia wananchi wake maji. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, sisi kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo kuanzisha mradi katika Mto Nkenge ili wananchi wake waweze kupata majisafi, salama na yenye kuwatosheleza.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. BALOZI. DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:- Mto Kagera ni chanzo muhimu kinachoweza kusaidia upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wanaopakana nao:- Je, kwanini Serikali isifanye utaratibu wa kuvuta maji hayo ili yawasaidie wakazi wa maeneo hayo?

Supplementary Question 2

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa upo mradi wa maji ambao tunautegemea sana katika Wilaya ya Ngara, mradi ambao tayari umeshapata kibali cha Serikali; na mwaka huu unaoishia kwenye bajeti zilikuwa zimetengwa shilingi milioni 200 kwa ajili ya kuanza usanifu wa mradi huu.

Ni lini Mhandisi Mshauri atakuwepo site tayari kwa ajili ya kuanza usanifu wa mradi huu?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, binafsi nilipata nafasi ya katika Jimbo lake la Ngara na tumeona chanzo cha Mto Ruvubu ni chanzo cha uhakika na kina maji mengi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama viongozi wa Wizara ndiyo maana tukamtuma mtaalam wetu. Kwa hiyo, kubwa tutafanya kila linalowezekana kuhakikisha Mhandisi Mshauri anapatikana kwa haraka ili kazi iweze kuanza mara moja na wananchi wake waweze kupata mradi huo.