Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- (a) Je, ni kwa nini Serikali imeshindwa kukamilisha mradi wa visima 23 ambavyo vingesaidia kama suluhisho la muda mfupi la tatizo la maji safi na salama katika Mji wa Tarime hususan kwenye maeneo ya Kata za pembezoni kama Nyandoto (Masurula), Nkende, Ketare, Kenyamanyori, Nyamisangura na Turwa? (b) Mheshimiwa Rais alipofanya ziara Jimbo la Tarime Mjini Julai, 2018 aliwaeleza wananchi kuwa Serikali imetenga takriban shilingi bilioni 14 kwa ajili ya maji kutoka Ziwa Victoria ambayo itaondoa kabisa tatizo la maji katika Mji wa Tarime. Je, ni hatua gani imefikiwa kwenye ahadi hiyo hasa ikizingatiwa kuwa mradi huo upo kwenye mchakato kwa miaka mingi sasa?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa majibu yanayotia matumaini kama yatatekelezeka, kwa sababu mradi wa Ziwa Victoria kuanzia wakati wa Mheshimiwa Eng. Kamwelwe alisema mnafanya upembuzi yakinifu na mradi ungeenda kuanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mji wa Tarime ndiyo Makao Makuu ya Wilaya Tarime na umekuwa na matatizo ya maji kwa muda mrefu na kusababisha wananchi wasifanye shughuli zao za maendeleo; na kwa kuwa vyanzo vikuu katika Mji wa Tarime ni Bwawa la Nyanduruma na lile la Tagota ambalo halitoi majisafi na salama na Wizara tuliowaomba hata angalau wajenge treatment plant wakasema wanategema mradi mkubwa wa Ziwa Victoria:

Ni lini sasa mtahakikisha kwamba ule mradi ambao tumeuanzisha Gamasara ambao tumesha-rise certificate, Mkandarasi amesimama kuanzia Novemba tumeleta Wizarani mpaka leo hajalipwa, ni lini yule Mkandarasi atalipwa ili angalau ajenge lile tenki la lita 100,000 kuweza kusaidia wananchi wa Gamasara na Kata ya Nyandoto na Kata za pembezoni kwa kipindi hiki tukisubiria huu mradi wa Ziwa Victoria ambao mmesema unakwenda kuanza mwaka 2019/2020?

La pili, hawa DDCA wameshakamilisha na walileta certificate na hata Mheshimiwa Eng. Kamwelwe mimi mwenyewe nilimpa document, lakini mpaka leo inavyosemekana, hawajalipwa fedha na ndiyo maana hata hawajaanza kufanya huo utafiti wa maji ya chini ya ardhi kama mlivyo-report hapa. Napenda sasa nihakikishiwe leo kwamba hawa DDCA watalipwa fedha ili wananchi wa Tarime hasa zile Kata za pembezoni waweze kuchimba visima na wapate majisafi na salama. Ahsante sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimtoe hofu dada yangu Mheshimiwa Esther Matiko, Serikali ya Awamu ya Tano ikiahidi inatekeleza na ikichelewa kutekeleza, basi kunakuwa na sababu maalum ya kueleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa ninalotaka kusema, pamoja na mradi mkubwa huo wa Ziwa Victoria katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji Tarime, lakini tuna mradi pale Gamasara wa asilimia 25, lakini tunatambua kabisa utekelezaji wa miradi ya maji inategemeana na fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri, tulikuwa na madeni ya Wakandarasi zaidi ya shilingi bilioni 88, lakini tunamshukuru Mheshimiwa Rais amewaagiza watu Wizara ya Fedha kutupa zaidi ya shilingi bilioni 44 kwa ajili ya kuwalipa Wakandarasi na tumeshazipata na tumeshazigawa. Tuna shilingi bilioni 44 nyingine tutakazopewa mwezi huu wa Nne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuhakikishie, katika maeneo yote ambayo Wakandarasi wanadai, tutawalipa ili miradi iendelee kutekelezeka na ahadi ya kumtua mwana mama ndoo kichwani iweze kitimilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala zima la DDCA, sisi pale tumeona haja ya uchimbaji wa visima. Sasa katika mgao huo wa shilingi bilioni 44, watu ambao wamelipwa ni watu wa DDCA. Tunawaagiza waende Tarime haraka katika kuhakikisha hii kazi inafanyika ili ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kumtua mwana mama ndoo kichwani inatimilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu ni kwamba endeleeni kutuunga mkono bajeti yetu katika mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- (a) Je, ni kwa nini Serikali imeshindwa kukamilisha mradi wa visima 23 ambavyo vingesaidia kama suluhisho la muda mfupi la tatizo la maji safi na salama katika Mji wa Tarime hususan kwenye maeneo ya Kata za pembezoni kama Nyandoto (Masurula), Nkende, Ketare, Kenyamanyori, Nyamisangura na Turwa? (b) Mheshimiwa Rais alipofanya ziara Jimbo la Tarime Mjini Julai, 2018 aliwaeleza wananchi kuwa Serikali imetenga takriban shilingi bilioni 14 kwa ajili ya maji kutoka Ziwa Victoria ambayo itaondoa kabisa tatizo la maji katika Mji wa Tarime. Je, ni hatua gani imefikiwa kwenye ahadi hiyo hasa ikizingatiwa kuwa mradi huo upo kwenye mchakato kwa miaka mingi sasa?

Supplementary Question 2

MHE. JOHN. W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Swali hili limekuja wakati mzuri kwa sababu ni swali linalohusu Tarime na ilikuwa Wilaya moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Mheshimiwa Rais amekuja Tarime Mwezi Julai, alisimama kwenye Mji wa Nyamongo kwenye Kijiji cha Kewanja na akaahidi kwamba Mwezi wa Tatu mwaka huu, watu wa Nyamongo ambao ni zaidi ya 35,000 wakazi wa pale na wakazi wa Sirari watakuwa wamepata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri anasemaje kuhusu hilo likiendana sana hasa na swali hili ambalo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Mwezi Julai?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimjibu tu kwa ufupi Mheshimiwa Mbunge. Ahadi ni deni; na Mheshimiwa Rais anapoahidi sisi hatuna kikwazo cha kushindwa kutekeleza. Kwa hiyo, tumejipanga katika kuhakikisha tunalitekeleza hilo jambo ili wananchi waweze kupata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- (a) Je, ni kwa nini Serikali imeshindwa kukamilisha mradi wa visima 23 ambavyo vingesaidia kama suluhisho la muda mfupi la tatizo la maji safi na salama katika Mji wa Tarime hususan kwenye maeneo ya Kata za pembezoni kama Nyandoto (Masurula), Nkende, Ketare, Kenyamanyori, Nyamisangura na Turwa? (b) Mheshimiwa Rais alipofanya ziara Jimbo la Tarime Mjini Julai, 2018 aliwaeleza wananchi kuwa Serikali imetenga takriban shilingi bilioni 14 kwa ajili ya maji kutoka Ziwa Victoria ambayo itaondoa kabisa tatizo la maji katika Mji wa Tarime. Je, ni hatua gani imefikiwa kwenye ahadi hiyo hasa ikizingatiwa kuwa mradi huo upo kwenye mchakato kwa miaka mingi sasa?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Wabunge tunachimba visima kwenye maeneo yetu. Kisima cha mita 100 kina-cost takribani shilingi milioni saba, lakini ukienda Halmashauri kisima cha mita 100, gharama zinazolipwa ni zaidi ya shilingi milioni 35 kwa kisima kimoja. Visima hivi 23 ambavyo vinataka kuchimbwa Tarime vitagharimu siyo chini ya shilingi milioni 900 kwa bei za Wakandarasi na bei za hao wanaokwenda huko kwenye Halmashauri zao.

Je, Serikali sasa lini ita-revisit bei hizi na kutoa bei elekezi kuhakikisha pesa za Serikali zinaokolewa na ubadhirifu ili wananchi wapate maji kwa bei nafuu ambapo yanaweza kupatikana kwa shilingi milioni saba tu kwa kisima cha mita 100?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nampongeza sana Mheshimiwa Zungu kwa swali lake zuri sana lakini kubwa tukiri kwamba kulikuwa kuna ubadhirifu mkubwa sana hasa katika miradi ya maji. Sisi tumeona hilo na ndiyo maana tukaanzisha Wakala wa Maji Vijijini na tuwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge kwa kutupitishai Muswada wetu na sisi tumejipanga katika kuhakikisha tunasimamia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya msingi katika kuhakikisha kwamba tunakuwa na gharama nafuu, sisi tunataka tuuongezee uwezo kwa Wakala wa Maji wa Uchimbaji Visima (DDCA) katika kuhakikisha tunawapa vifaa vya kutosha ili uchimbaji wake uwe nafuu uweze kuendana na watu binafsi. Ahsante sana.