Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY atauliza:- Serikali ina nia njema ya kuuweka Mji Mkongwe wa Mbulu kwenye mpango kabambe wa maboresho ya Miji na Majiji, Mikoa na Wilaya na kwenye Awamu ya Pili ya mpango huo kwa ajili ya miundombinu ya masoko, barabara, vituo vya mabasi na taa za barabarani:- (a) Kwa kuwa Mji wa Mbulu ni mkongwe toka kuanzishwa kwake, je, ni lini sasa nia hiyo njema itatekelezwa? (b) Je, mpango huo wa maboresho ya Mji utasaidiaje miundombinu ya barabara za mitaa ya Mji wa Mbulu ambazo ni zaidi ya kilomita 40 za changarawe kwa kuwa ni kilomita 1.8 za lami kwa sasa?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, mpango unaotekelezwa sasa wa kilomita 0.4 ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na kwa kuwa ahadi hii ya Mheshimiwa Rais ni kilomita 5 katika Mji wa Mbulu, nini majibu ya Serikali kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 kwa kuwa Rais atakuwa anataka ahadi hiyo iwe imetekelezwa na mimi nimeshatimiza wajibu wangu wa kuikumbusha Serikali mara kadhaa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, ni kweli Mji wa Mbulu ni mji mpya ulioanzishwa lakini ni Halmashauri au Wilaya kongwe katika ya Wilaya kongwe Tanzania. Kwa hivi sasa Mji wa Mbulu una kilomita 1.8 katika mitaa yake kwa kiwango cha lami. Kwa kuwa hali ya barabara na madaraja katika kata kumi ukiacha kata zingine nane za vijijini ni mbaya; na kwa kuwa TARURA wanapewa fedha kidogo sana hivyo kushindwa kutekeleza mahitaji yaliyoibuka, nini kauli ya Serikali kuwezesha miundombinu ya barabara katika Miji wa Mbulu pamoja na ahadi hiyo ya Rais?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimjibu Mheshimiwa Mbunge Zakharia, Mbunge wa Mbulu Mji maswali mawili ya nyongeza kwa pamoja, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza anauliza kuhusiana na ahadi ya Mheshimiwa Rais, naomba nimhakikishie kwamba hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais, kipenzi cha Watanzania, namhakikishia kabla ya 2020 ahadi hii itakuwa imekamilishwa ili Mheshimiwa Rais atakapoenda kuomba kura kwa awamu nyingine kwa niaba ya Chama cha Mapinduzi, asipate vikwazo kwa wananchi wa Mji wa Mbulu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, anapenda kujua tuna mpango gani, nitoe maelekezo kwa TARURA Mkoa na Wilaya yake ya Mbulu kama hali ya mji huu ni mbaya kiasi hicho wafanye mchakato walete maandishi hapa tujue namna ya kufanya ili tuweze kuboresha wakati tukisubiri kutafuta fedha nyingi zaidi za kuboresha Mji wa Mbulu. Ahsante.

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY atauliza:- Serikali ina nia njema ya kuuweka Mji Mkongwe wa Mbulu kwenye mpango kabambe wa maboresho ya Miji na Majiji, Mikoa na Wilaya na kwenye Awamu ya Pili ya mpango huo kwa ajili ya miundombinu ya masoko, barabara, vituo vya mabasi na taa za barabarani:- (a) Kwa kuwa Mji wa Mbulu ni mkongwe toka kuanzishwa kwake, je, ni lini sasa nia hiyo njema itatekelezwa? (b) Je, mpango huo wa maboresho ya Mji utasaidiaje miundombinu ya barabara za mitaa ya Mji wa Mbulu ambazo ni zaidi ya kilomita 40 za changarawe kwa kuwa ni kilomita 1.8 za lami kwa sasa?

Supplementary Question 2

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Katika majibu yake Mheshimiwa Naibu Waziri ameeleza kwamba mipango ya kuendeleza barabara za miji ni pamoja na Mpango wa DMDP. Katika Manispaa ya Ubungo mpango wa DMDP, unatekelezwa kwa upande wa Jimbo la Ubungo peke yake lakini upande wa Jimbo la Kibamba kwenye Kata sita za Kwembe, Msigani, Mbezi, Saranga, Goba mpango huu hautekelezwi kabisa.

Je, Serikali ina mpango gani wa kupanua utekelezaji wa mpango wa DMDP ili kuzigusa kata sita za Jimbo la Kibamba kwenye masuala ya miundombinu ya barabara?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mnyika, Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Mkoa wa Dar es Salaam ikiwepo maeneo ambayo ametaja ya Ukonga na maeneo mengine, tunatekeleza awamu ya kwanza ya mpango ya DMDP. Naomba niwahakikishie kwamba itakapokuja awamu ya pili Wabunge watashirikishwa waweze kuainisha maeneo yao ili tupanue wigo zaidi wa kuendeleza Mji wetu wa Dar es Salaam.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY atauliza:- Serikali ina nia njema ya kuuweka Mji Mkongwe wa Mbulu kwenye mpango kabambe wa maboresho ya Miji na Majiji, Mikoa na Wilaya na kwenye Awamu ya Pili ya mpango huo kwa ajili ya miundombinu ya masoko, barabara, vituo vya mabasi na taa za barabarani:- (a) Kwa kuwa Mji wa Mbulu ni mkongwe toka kuanzishwa kwake, je, ni lini sasa nia hiyo njema itatekelezwa? (b) Je, mpango huo wa maboresho ya Mji utasaidiaje miundombinu ya barabara za mitaa ya Mji wa Mbulu ambazo ni zaidi ya kilomita 40 za changarawe kwa kuwa ni kilomita 1.8 za lami kwa sasa?

Supplementary Question 3

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Mji wa Mafinga ulikuwa Mamlaka ya Mji Mdogo kwa miaka tisa na Julai 2015 ikawa Halmashauri kamili ya mji. Je, Serikali inaweza kuwahakikishia wana-Mafinga kwamba kwa kuwa Halmashauri ya Mji kamili na wao wameingia katika Mpango Kabambe wa Maboresho ya Miji? Kwa sababu sasa hivi Mafinga ni Halmashauri ya Mji kamili. Tunataka tu kuhakikishiwa na sisi tunaingia katika awamu ya pili? Kwa sababu ndiyo ukombozi wa barabara zetu?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cosato Chumi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge alikuwa na Mheshimiwa Rais amekubaliwa mambo yake yote manne leo amelala usingizi mnono kabisa. Katika suala hili, kama nilivyojibu swali la Mheshimiwa Zakharia, Mbunge wa Mbulu Mji, tutakapoanza kufanya mchakato miji mipya yote na huo mji wako utaingizwa katika awamu hiyo.