Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Wananchi wa Kata za Kinyerezi, Bonyokwa, Segerea Liwiti, Kipawa, Kimanga, Kisukulu na Tabata wamekuwa wakitumia fedha na muda mwingi kwenda kutafuta bidhaa na huduma katika masoko ya Buguruni na Kariakoo kutokana na kukosa huduma hizo katika maeneo yao:- (a) Je, kwa nini Serikali isijenge soko kubwa katika eneo mbadala lililo katikati na linaloweza kufikiwa na wananchi hao kwa wakati? (b) Je, kwa nini Soko la Kinyerezi lililozinduliwa na Mwenge mwaka 2017 lisifunguliwe ili kutoa huduma kwa wananchi wanaozunguka soko hilo na maeneo ya karibu?

Supplementary Question 1

MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ambayo ameyajibu Mheshimiwa Naibu Waziri; kwa kuwa Serikali imeanzisha miradi ya kimkakati katika mikoa mingine na ukizingatia katika Jimbo la Segerea kuna wananchi wengi sana ambao wanakaribia 1,300,000; je, Serikali ina mpango gani kujenga masoko ambayo yatakuwa yanawasaidia wananchi ili wasiweze kwenda mbali kama hivyo alivyosema Kisutu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, nimemsikia Mheshimiwa Waziri anaongelea kuhusiana na Soko la Kinyerezi. Kutokana na kwamba nilifanya ziara mwezi uliopita, hilo soko mpaka sasa hivi kwanza linavuja, halafu pia halijamaliziwa vizuri. Kwa hiyo, haliwezi kuzinduliwa mwaka 2019 kama anavyosema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, kuna Kata nyingi ambazo hazina masoko kama Kata ya Kisukulu, Kata ya Kipawa na Kata nyingine: Je, Serikali ina mpango gani kuhusiana na hizo Kata nyingine kuhakikisha kwamba zinapata masoko?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuelewa, nakushukuru. Swali la kwanza ningeomba niseme tu kwamba utaratibu unaotumika kuibua miradi ya kimkakati ni Halmashauri husika, inakaa na wataalam wake, wanaandika andiko, wanaliwasilisha Ofisi ya TAMISEMI pamoja na Wizara ya Fedha; wataalam wa Wizara ya Fedha wanaenda kufanya tathimini ya andiko lenyewe, gharama zake na mrejesho kwa maana ya faida itakayopatikana na baada ya hapo wataruhusiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hii ya kuwa na masoko ya Kinyerezi na maeneo mengine, itategemea Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili nilitaka tu niseme kwamba inawezekana ni kweli Mheshimiwa Mbunge anasema, sasa nimwelekeze Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala aende akafanye utaratibu wa kukarabati na kurekebisha soko hilo ili liendane na ambavyo nimejibu katika swali langu la msingi, kwamba Kinyerezi ilizinduliwa mwaka 2017 na Mbio za Mwenge wa Uhuru lakini Mei mwaka huu linatakiwa lianze kufanya kazi. Mkurugenzi aweke pesa pale ili liweze kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja anayoizungumza Mheshimiwa Mbunge hapa, soko la Kisutu ni kweli lipo kwenye mkakati, limesharuhusiwa na Serikali na fedha imeshatolewa. Naomba nimhakikishie, kwa kadri anavyojua kwamba lazima lisimamiwe; na Mheshimiwa Mbunge nimridhishe kwamba yeye katika Manispaa ya Ilala ana ujenzi wa machinjio ya kisasa kabisa ya Vingunguti ambayo ipo pia kwenye mpango mkakati katika eneo hilo. Ahsante.

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Wananchi wa Kata za Kinyerezi, Bonyokwa, Segerea Liwiti, Kipawa, Kimanga, Kisukulu na Tabata wamekuwa wakitumia fedha na muda mwingi kwenda kutafuta bidhaa na huduma katika masoko ya Buguruni na Kariakoo kutokana na kukosa huduma hizo katika maeneo yao:- (a) Je, kwa nini Serikali isijenge soko kubwa katika eneo mbadala lililo katikati na linaloweza kufikiwa na wananchi hao kwa wakati? (b) Je, kwa nini Soko la Kinyerezi lililozinduliwa na Mwenge mwaka 2017 lisifunguliwe ili kutoa huduma kwa wananchi wanaozunguka soko hilo na maeneo ya karibu?

Supplementary Question 2

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mji wa Karatu ni Mji wa Kitalii na hauna soko la uhakika. Hivi sasa wananchi wa Karatu kwa kutumia mapato yao ya ndani wameanza kujenga soko lenye hadhi ya Mji huo: Je, Serikali iko tayari sasa kuunga mkono jitihada za wananchi hao ili soko hilo likamilike?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika Mkoa wa Manyara tayari tuna mradi wa kimkakati katika Wilaya ya Hanang’. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, fedha zipo, Serikali ipo tayari kutoa ushirikiano. Cha muhimu, Halmashauri husika ikae na kutoa andiko, likija hapa kwenye tathmini hili jambo litafanyika. Sisi tunakusudia kuweka masoko, stendi na majengo mbalimbali ya kimkakati ili baada ya kuwekeza katika maeneo hayo, Halmashauri zetu zipate mapato ya kutosha ili kuweze kuendeleza na kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi wetu.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Wananchi wa Kata za Kinyerezi, Bonyokwa, Segerea Liwiti, Kipawa, Kimanga, Kisukulu na Tabata wamekuwa wakitumia fedha na muda mwingi kwenda kutafuta bidhaa na huduma katika masoko ya Buguruni na Kariakoo kutokana na kukosa huduma hizo katika maeneo yao:- (a) Je, kwa nini Serikali isijenge soko kubwa katika eneo mbadala lililo katikati na linaloweza kufikiwa na wananchi hao kwa wakati? (b) Je, kwa nini Soko la Kinyerezi lililozinduliwa na Mwenge mwaka 2017 lisifunguliwe ili kutoa huduma kwa wananchi wanaozunguka soko hilo na maeneo ya karibu?

Supplementary Question 3

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kata yangu ya Mahenge Mjini ambapo ndiyo Mji wenyewe ulipo, kuna shida kubwa ya soko. Wananchi walijitolea wakajenga soko, Serikali ikatia hela zake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2018 Mwenge ulikuja ukafungua hilo soko, lakini mpaka leo hii soko hilo halijaanza kutumika. Kwa hiyo, Mwenge umedanganywa, Mbunge kadangaywa, wananchi wamedanganywa. Je, lini Serikali itasimamia ufunguaji wa soko hilo ili wananchi wapate kulitumia?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuhsukuru. Hili jambo tumelipokea, tutalifanyia kazi tuone tatizo liko sehemu gani ili liweze kufanya kazi.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Wananchi wa Kata za Kinyerezi, Bonyokwa, Segerea Liwiti, Kipawa, Kimanga, Kisukulu na Tabata wamekuwa wakitumia fedha na muda mwingi kwenda kutafuta bidhaa na huduma katika masoko ya Buguruni na Kariakoo kutokana na kukosa huduma hizo katika maeneo yao:- (a) Je, kwa nini Serikali isijenge soko kubwa katika eneo mbadala lililo katikati na linaloweza kufikiwa na wananchi hao kwa wakati? (b) Je, kwa nini Soko la Kinyerezi lililozinduliwa na Mwenge mwaka 2017 lisifunguliwe ili kutoa huduma kwa wananchi wanaozunguka soko hilo na maeneo ya karibu?

Supplementary Question 4

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa imekuwa ni ahadi ya muda mrefu ya Serikali kujenga Soko la Mto wa Mbu Wilayani Monduli Mkoani Arusha, lakini mpaka sasa hakuna chochote kinachoendelea na wananchi wa Mto wa Mbu wamekuwa wakipata taabu: Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Soko la Mto wa Mbu Mkoani Arusha?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni kweli hili suala hata Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mheshimiwa Julius Kalanga ameniuliza jana. Kama nilivyosema, namwomba Mheshimiwa Mbunge wakae na Halmashauri yao, fedha zipo kama ulivyosema. Ni kuandika andiko na sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI tupo tayari kusaidia utaalaam na namna ya kuboresha pamoja na Hazina ili andiko likamilike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua kuna wapiga kura wengi sana pale Mto wa Mbu, tungependa wapate soko zuri, wapate kipato, pia wachangie kodi katika maendeleo ya Watanzania wenzetu. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane hili jambo liweze kufanyiwa kazi.