Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Susan Anselm Jerome Lyimo
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SUSAN A. J. LYIMO (K.n.y. MHE. CATHERINE N. RUGE) aliuza:- Kumekuwa na idadi ndogo ya wasichana wanaodahiliwa katika vyuo vya elimu ya juu katika fani ya sayansi ikizingatiwa kuwa sasa tunaelekea katika uchumi wa viwanda:- Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha inaongeza idadi ya wasichana katika masomo ya sayansi kuanzia ngazi ya chini mpaka vyuo vikuu?
Supplementary Question 1
MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri na mikakati yote ya Serikali bado idadi (ratio) ya wasichana kwa wavulana katika vyuo vyety vya elimu ya juu ni ndogo sana katika masomo ya sayansi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kwamba baadhi ya vyuo, kwa mfano Chuo Kikuu cha Dar es Salaam siku za nyuma kilikuwa na programu ambayo ilikuwa inawasaidia wasichana ambao wamepata point chache wanakuja kwenye hiyo programU walau miezi miwili ili waweze sasa kujiunga na vyuo lakini programU hiyo sasa haipo na bado tunahitaji sana wasichana kuendelea na masomo. Swali la kwanza, je, ni lini programu kama hizo zitarudishwa ili kusaidia wasichana kwa kuwa tunatambua mazingira magumu wanayowapata wasichana huku chini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, pamoja na kwamba wanajenga mabweni au hosteli katika vyuo na shule zetu lakini bado tuna tatizo kubwa sana la uhaba wa mabweni ambayo yangewasaidia wasichana hawa kuweza kujiunga na vyuo vya elimu ya juu kuweza kuweka uwiano wa kijinsia siyo tu katika vyuo lakini hata katika masuala mazima ya siasa maana tunapata wanawake wachache kwa sababu hiyo. Ni lini mtatekeleza hilo?
Name
William Tate Olenasha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngorongoro
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Susan Lyimo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Chuo Kikuu cha Dar es Salaam siku za nyuma kilikuwa na mpango ambao ulifanikiwa sana wa kuwasaidia wanafunzi wengi wa kike kuweza kujiunga na masomo ya sayansi. Mpango ule muda wake ulishaisha lakini kwa sasa tayari kuna majadiliano ya kurudisha au kuanzisha programu inauhusiana na suala hilo na katika hali ambayo itawahusisha watoto wa kike wengi zaidi katika vyuo vingine, kwa hiyo, majadiliano yapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sisi kama Serikali tunachofanya ni kuboresha elimu kwa ujumla wake pamoja na kutoa hamasa na kuomba wananchi na wadau wote washirikiane katika kuondoa mila na fikra potofu ambazo zinafanya watoto wa kike waogope kwenda kuchukua masomo ya sayansi. Nashukuru kwamba leo tumetembelewa na wanafunzi wa kike wa sekondari. Naomba nitumie nafasi hii kuwaeleza kwamba sayansi na hisabati ni ya kila mtu na siyo kwa ajili ya wanaume tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali lake la pili kuhusiana na ujenzi wa mabweni na hosteli, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara yangu mwezi Januari ilipeleka katika shule na vyuo tofauti 560 shilingi bilioni 56 ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kujenga miundombinu katika shule na vyuo vyetu na kati ya fedha hizo, nyingi zimeenda vilevile katika kujenga hosteli na mabweni. Yeye mwenyewe anajua baadhi ya vyuo kwa mfano Chuo cha Ardhi na Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere tunajenga hosteli kwa ajili ya wanafunzi lakini maarufu kwa utetezi wake wa Hall 2 na Hall 5 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa sasa vimetengewa shilingi bilioni nne. Kwa kweli katika vyuo vyetu tunajitahidi kujenga mabweni na hosteli za wanafunzi.
Name
Edward Franz Mwalongo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Njombe Mjini
Primary Question
MHE. SUSAN A. J. LYIMO (K.n.y. MHE. CATHERINE N. RUGE) aliuza:- Kumekuwa na idadi ndogo ya wasichana wanaodahiliwa katika vyuo vya elimu ya juu katika fani ya sayansi ikizingatiwa kuwa sasa tunaelekea katika uchumi wa viwanda:- Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha inaongeza idadi ya wasichana katika masomo ya sayansi kuanzia ngazi ya chini mpaka vyuo vikuu?
Supplementary Question 2
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Ili watoto wa kike waweze kufanikiwa katika masomo ya sayansi wanahitaji uwepo wa walimu. Tuna tatizo kubwa sana kama nchi ya walimu wa sayansi na hasa hasa physics. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakisha shule zetu zinapata walimu wa kutosha wa physics?
Name
William Tate Olenasha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngorongoro
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwalongo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama alivyosema kwamba ili watoto wa kike waweze kufanikiwa kuchukua masomo ya sayansi ni lazima kuwa na walimu na ndiyo maana Serikali imekuja na mikakati thabiti ya kuhakikisha kwamba walimu wanapatikana. Wote tunakumbuka kwamba Serikali ilipeleka wanafunzi wale waliokuwa UDOM kwenda kusoma masomo ya sayansi na tunategemea wataanza kuingia sokoni kwa ajira za hivi karibu. Pia katika vyuo 35 ambavyo tunavyo, Serikali imeamua sasa kutenga vyuo vichache kati ya hivyo vinakuwa ni vyuo vinavyofundisha sayansi. Kwa hiyo, tunaendelea kuongeza fursa na udahili katika vyuo vya elimu vinavyotoa walimu wa sayansi.
Name
Yussuf Salim Hussein
Sex
Male
Party
CUF
Constituent
Chambani
Primary Question
MHE. SUSAN A. J. LYIMO (K.n.y. MHE. CATHERINE N. RUGE) aliuza:- Kumekuwa na idadi ndogo ya wasichana wanaodahiliwa katika vyuo vya elimu ya juu katika fani ya sayansi ikizingatiwa kuwa sasa tunaelekea katika uchumi wa viwanda:- Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha inaongeza idadi ya wasichana katika masomo ya sayansi kuanzia ngazi ya chini mpaka vyuo vikuu?
Supplementary Question 3
MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Napenda nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri wa Elimu, kumekuwa na malalamiko mengi ya wanawake kwamba hawapati nafasi za kutosha katika shule kuanzia sekondari, vyuo na vyuo vikuu. Sasa ni mkakati wa Serikali kwamba wanawake wakifikia hapo waanze kubinywa au wanawake wenyewe wamezoea kudekezwa tu?
MWENYEKITI: Hebu tusaidiane kidogo, unauliza vizuri lakini hilo neno kudekezwa linyooshe tu.
MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri aseme kuna mkakati kwamba wanawake wanabinywa au sasa wao wenyewe wanataka wasaidiwe tu kwenda vyuoni?
Name
William Tate Olenasha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngorongoro
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti nilichokuwa nazungumzia katika maswali yangu yaliyopita ndiyo inajionyesha dhahiri hapa kwamba ni suala la mila, desturi na fikra potofu dhidi ya uwezo wa watoto wa kike kuweza kuendelea na kufanya vizuri kama watoto wa kiume.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Waheshimiwa Wabunge kila mmoja katika nafasi yake ajielekeze kwenye ukweli kwamba mtoto wa kike ana uwezo sawa na mtoto wa kiume, kwa hiyo, tuwasaidie waweze kusonga mbele.