Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. MARTHA M. MLATA) aliuliza:- Je, ni kwa nini Sherehe za Muungano zimekuwa zikifanyika na kupewa nafasi kubwa Kitaifa tu?

Supplementary Question 1

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali moja la nyongeza. Kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, kwa kuwa Muungano umetuletea faida nyingi sana katika nchi yetu na ndiyo maana viongozi wetu, waasisi na sisi wenyewe tumekuwa tukiuenzi na kuulinda kwa nguvu zote na kwa kuwa sasa huko vijijini vijana wetu wengi wamekuwa hawana uwelewa sana wa kutosha kuhusiana na huu Muungano. Je, ni ni kwa nini sasa Serikali isiweke utaratibu wakati wa sherehe hizi elimu itolewe kwa ajili ya vijana wetu na wananchi walioko vijijini kuliko kufanya sherehe kitaifa zaidi?

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati kwa niaba yake ambapo swali la msingi lilikuwa la Mheshimiwa Martha Moses Mlata. Kwanza kabisa nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Mlata kwa swali hili ambalo litatoa ufahamu mkubwa sana.

Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kutoa rai, siku ya tarehe 26 nafahamu itakuwa siku ya Ijumaa mwezi wa Nne kwamba Taasisi zote za Elimu zitumie fursa hii ya kutoa elimu kuhakikisha kwamba wanakuwa na makongamano na mijadala mbalimbali juu ya historia ya Muungano wetu. Ahsante.