Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO (K.n.y. MHE. KHADIJA NASSIR ALI) aliuliza:- Kwa kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea na zoezi la kununua ndege:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kuhakikisha kuwa ndege hizo zinakwenda kila mkoa wenye kiwanja cha ndege pamoja na nchi jirani ili kusaidia kushusha gharama za usafiri?

Supplementary Question 1

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mimi nina swali moja tu la nyongeza. Pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa na Shirika letu la Ndege la Taifa, kumekuwepo na malalamiko makubwa ya wananchi hususan kuhusu bei za tiketi. Ni kwa nini Serikali isione kuna umuhimu wa kupunguza gharama hizi za tiketi ili wananchi wengi waweze kumudu usafiri huu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kufanya hivyo, itapelekea shirika kuongeza routes badala ya kuwa na route moja kwa siku wanaweza kuwa na route mbili mpaka tatu. Mfano Dodoma – Dar es Salaam kuna route moja...

MWENYEKITI: Ahsante sana, umeeleweka.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Halima Bulembo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, bei za safari za ndege za ATCL huwa zinapangwa kutokana na hali ya soko. Ni ukweli usiopingika kwamba ATCL wako kwenye ushindani na sisi Serikali tunaendelea kuwa-encourage na watu wengine waendelee kutumia usafiri wa anga kupeleka ndege zao maeneo mbalimbali. Sasa hivi wanashindana na watu kama Precision na mashirika mengine, kwa hiyo, hayo mashirika mengine kutokana na ushindani huo ndiyo bei inajipanga yenyewe, huwa inapangwa kutokana na market force.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO (K.n.y. MHE. KHADIJA NASSIR ALI) aliuliza:- Kwa kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea na zoezi la kununua ndege:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kuhakikisha kuwa ndege hizo zinakwenda kila mkoa wenye kiwanja cha ndege pamoja na nchi jirani ili kusaidia kushusha gharama za usafiri?

Supplementary Question 2

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa safari za ndani za ATCL hakuna mkoa wowote unaoishinda Pemba kwa biashara ya ndege. Mheshimiwa Waziri ulituita mbele ya wadau ukatuahidi kwamba ikifika Novemba/Desemba, 2018 ATCL itaanza safari za Pemba. Hadi leo mwezi Aprili, 2019 haijaanza safari kuelekea Pemba, nini kauli yako Mheshimiwa Naibu Waziri?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hussein, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli mwaka jana tuliongea na baadhi ya Waheshimiwa kutoka Pemba kuhusu uwezekano wa ATCL kupeleka ndege yao Pemba. Mpaka sasa hivi hatupingi kwamba kuna abiria wa kutosha Pemba lakini ndege zenyewe siyo nyingi kiasi hicho. Naomba Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wengine wote waendelee kuvuta subira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni Mheshimiwa Rais ametupatia ndege mbili za Serikali, tunaendelea kuzipaka rangi ili zianze kutumika kwa ajili ya abiria. Kwa hiyo, naamini hata Pemba tutawapelekea ndege moja na sehemu nyingine mbalimbali tutaendelea kupanua wigo wa kusafirisha watu kwa usafiri wa anga.

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO (K.n.y. MHE. KHADIJA NASSIR ALI) aliuliza:- Kwa kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea na zoezi la kununua ndege:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kuhakikisha kuwa ndege hizo zinakwenda kila mkoa wenye kiwanja cha ndege pamoja na nchi jirani ili kusaidia kushusha gharama za usafiri?

Supplementary Question 3

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Wananchi wa Kahama wamekuwa wakiulizia usafiri wa ndege kwa Mkoa wa Shinyanga. Kwa sababu Uwanja wa Ndege wa Shinyanga bado unafanyiwa matengenezo, ni lini ATCL itaanza kutua Kahama?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Ezekiel Maige, Mbunge wa Kahama, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili nalo ni eneo lingine ambalo Serikali inakiri kwamba kuna abiria wa kutosha hata ATCL inafahamu hivyo lakini bado kuna changamoto kidogo ya uwanja, tunaendelea kurekebisha runway iweze kukidhi mahitaji ambapo ndege zetu za ATCL zitaweza kushuka. Tayari tumeshamu-assign TANROADS kwa ajili ya kufanya BOQ ya kurekebisha uwanja huo. Ukisharekebishwa vizuri tutaanza kutua kwa sababu pale abiria na soko la kutosha lipo.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO (K.n.y. MHE. KHADIJA NASSIR ALI) aliuliza:- Kwa kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea na zoezi la kununua ndege:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kuhakikisha kuwa ndege hizo zinakwenda kila mkoa wenye kiwanja cha ndege pamoja na nchi jirani ili kusaidia kushusha gharama za usafiri?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Nataka nimuulize Mheshimiwa Waziri kwamba wake wa Wabunge ama waume wa Wabunge wana haki mbalimbali za kupata huduma kama vile kupita njia za VIP lakini cha ajabu ni kwamba wake zetu wanapata shida sana upande wa VIP. Je, wana haki ama hawana haki ya kupata huduma upande wa VIP, kama vile kwenye feri na viwanja vya ndege?

MWENYEKITI: Kwenye viwanja vya ndege?

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano viwanja vya ndege pamoja na feri.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la ndugu yangu wa Nyang’wale, Mbunge mahiri sana, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli ulio wazi kwamba wake au waume au wenza wa Wabunge wanayo haki yote ya kutumia VIP na sijawahi kuona hilo tatizo ninapotembelea viwanja mbalimbali vya ndege. Kwa hiyo, Mheshimiwa kama lilikutokea tunaomba radhi lakini siyo kitu cha kawaida, wenza wa Wabunge huwa wanapata huduma zote stahiki za VIP.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO (K.n.y. MHE. KHADIJA NASSIR ALI) aliuliza:- Kwa kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea na zoezi la kununua ndege:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kuhakikisha kuwa ndege hizo zinakwenda kila mkoa wenye kiwanja cha ndege pamoja na nchi jirani ili kusaidia kushusha gharama za usafiri?

Supplementary Question 5

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa ndege zetu za Air Tanzania zimekuwa zikishindwa kutua katika Uwanja wa Ndege wa Arusha kwa kuwa kiwanja hiki ni kidogo na tunaelewa kabisa Arusha ni kitovu cha utalii na nimekuwa nikiongea kila mara na…

MWENYEKITI: Uliza swali.

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Serikali imekuwa ikiniahidi lakini haitimizi, mpaka sasa hivi nimechoka kufuatilia. Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kupanua Kiwanja cha Ndege cha Arusha?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Catherine Magige, Mbunge Viti Maalum, Mkoa wa Arusha, kama ifutavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri ukweli kwamba Mheshimiwa Catherine Magige amekuwa akifuatilia sana suala la upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Arusha na nimpongeze kwa sababu kwa kupitia juhudi zake nimtaarifu rasmi kwamba TANROADS sasa hivi wanaandaa BOQ kwa ajili ya upanuzi wa uwanja huo kwa mita 200 zaidi lakini pia wanashirikiana na TAA katika kuhakikisha kwamba uwanja huo unaendelea kupanuliwa pamoja na kuwekewa apron nyingine mpya. Hivi karibuni mkandarasi ataingia site kwa ajili ya upanuzi wa uwanja huo ili ndege kubwa ziweze kuanza kuruka.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO (K.n.y. MHE. KHADIJA NASSIR ALI) aliuliza:- Kwa kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea na zoezi la kununua ndege:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kuhakikisha kuwa ndege hizo zinakwenda kila mkoa wenye kiwanja cha ndege pamoja na nchi jirani ili kusaidia kushusha gharama za usafiri?

Supplementary Question 6

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika marekebisho ya Uwanja wa Ndege wa Musoma, nakumbuka Mheshimiwa Rais amefika pale mara mbili na mara zote ameahidi uwanja huo ujengwe kwa kiwango cha lami na uthamini umefanyika, sasa ni zaidi ya miezi sita. Nataka kupata kauli ya Serikali baada ya kuwa kuna sintofahamu, je, mpango wa kujenga uwanja huo upo au haupo?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Manyinyi, Mbunge wa Musoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Uwanja wa Ndege wa Musoma uko kwenye mipango ya kupanuliwa na kuwekewa runway kwa kiwango cha lami na TAA. Hivi karibuni nilifanya ziara Mjini Musoma tukakuta kuna changamoto ya fidia ambapo kulikuwa kuna mvutano wa hapa na pale lakini kuna timu ya wataalam imetumwa pale kwa ajili ya kwenda kuhakikisha ile changamoto ya fidia ya shilingi bilioni tatu na milioni mia saba inatatuliwa ili tuweze kulipa fidia na upanuzi uweze kuendelea.