Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itachukua hatua za kimkakati kuhakikisha kwamba migogoro kati ya wafugaji na wananchi wanaoishi pembezoni mwa mbuga za wanyama inakwisha kabisa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa napenda niishukuru na niipongeze Serikali yangu kwa namna ambavyo imekuwa ikiwajali wananchi hasa wanaoishi vijijini na pia kuangalia namna gani ya kutatua matatizo ya wananchi. Pamoja na pongezi hizo za kupongeza Serikali yangu, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza; ni kwa kiwango gani Taarifa ya Wizara hizi ambazo zilikaa kama Kamati ambazo zimeweza kuja na ushauri namna gani ya kutatua matatizo ambayo hasa katika vijiji mfano katika Jimbo langu la Kavuu, vijiji vyangu ambavyo ni vijiji vya Ikopa, Itura, Luchima, Sentaunyenye, Iziwasungu, Kabunde na kwingineko?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; kwa kuwa tuna migogoro mikubwa katika kijiji cha Luchima na mpaka wa TANAPA kwa ajili ya mto wa Kavuu na nilikwishaleta maombi mwaka jana na TANAPA walikwishaanza kujenga kisima kwa ajili ya kupunguza mgogoro uliopo kati ya wananchi wa Kijiji cha Luchima pamoja na mpaka wao. Je, ni lini sasa hawa ndugu zangu wa TANAPA wataweza kumalizia kile kisima ili wananchi wangu wa kijiji cha Luchima waweze kuwa huru katika kufanya shughuli zao za kilimo na uvu vi bila kuingiliwa na askari wa TANAPA.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu amekuwa akifuatilia kwa karibu sana suala la migogoro baina ya maeneo ya uhifadhi na vijiji ambavyo amevitaja. Naomba nichukue nafasi hii kuwajulisha Wabunge wote ni kwamba taarifa hii ambayo Wizara yetu pamoja na Wizara zingine imeshiriki, itakapokuwa tayari kutumika sasa baada ya maelekezo ya Mheshimiwa Rais tutashirikisha Wabunge na viongozi katika Serikali za vijiji vyote na Halmashauri kuangalaia mipaka mipya ambayo tutaiweka ambayo itaondoa migogoro hii ambayo imekuwepo kwa muda mrefu. Kwa hiyo, nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu TANAPA kukamilisha mradi wa kisima cha maji, nawaelekeza TANAPA kwa sababu mradi huo walikwishaanza kukamilisha kisima hicho haraka katika mwaka huu wa fedha.