Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:- Madeni ya Halmashauri hususan mikopo ya vijana na wanawake ya miaka ya nyuma kabla ya mwaka 2016 yamekuwa hayalipiki kutokana na Halmashauri nyingi kutokuwa na mapato ya kutosha kuendesha Halmashauri hizo hasa miradi ya maendeleo. Je, ni kwa nini madeni hayo yasifutwe ili kuondoa hoja za ukaguzi kwenye Halmashauri hizo?

Supplementary Question 1

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nina swali moja la nyongeza. Pamoja na kwamba Serikali imejibu vizuri, nawapongeza sana; na uamuzi unaokuja wa kufuta madeni ni mzuri sana, nawapongeza sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati hizi fedha zinakopesha huko nyuma, kuna baadhi ya Halmashauri zilipeleka fedha kidogo; pamoja na kwamba hazikupeleka zote, lakini fedha hizi wale waliokopeshwa au vikundi vilikopeshwa vimekuwa vikisuasua sana katika kulipa hizi fedha. Mfano Halmashuri ya Wilaya ya Njombe kabla, tulikuwa Halmshauri moja upande wa Wanging’ombe na Makambako. Baada ya kugawanya hizi Halmashuri, zile fedha zilizokopeshwa kwenye vikundi vya Halmashauri nyingine, kwa mfano, Wanging’ombe na Makambako, imekuwa ni vigumu sana kurejesha na wamekuwa wakisuasua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini kauli ya Serikali kwa vile vikundi ambavyo vilikopeshwa na sasa wanasuasua kurejesha au hawarejeshi kabisa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nashukuru kwa pongezi ambazo ametoa na kwa hatua ambazo Serikali inachukua kufuta madeni na malimbikizo haya. Naomba nitoe maelekezo kwamba hizi fedha hazikuwa sadaka, wala zawadi. Hii ilikuwa ni mikopo; na dawa ya kukopa ni kulipa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwaelekeze Wakurugenzi wote nchini walipo na wale Maafisa Ustawi wa Jamii na Mikoa, Wilaya na Kata, vile vikundi ambavyo vilipewa fedha hii ya Serikali kwa ajili ya kujiendeleza na kuboresha maisha yao, ni muhimu warejeshe fedha hizi na waweke time frame baada ya muda fulani fedha irejeshwe. Kwa sababu makusudi ya Serikali ilikuwa, kikundi kimoja kikikopeshwa kikaboresha maisha yake, wakirejesha na wengine zaidi wanaendelea kukopeshwa ili waweze kuyaboresha maisha yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Amina Nassoro Makilagi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:- Madeni ya Halmashauri hususan mikopo ya vijana na wanawake ya miaka ya nyuma kabla ya mwaka 2016 yamekuwa hayalipiki kutokana na Halmashauri nyingi kutokuwa na mapato ya kutosha kuendesha Halmashauri hizo hasa miradi ya maendeleo. Je, ni kwa nini madeni hayo yasifutwe ili kuondoa hoja za ukaguzi kwenye Halmashauri hizo?

Supplementary Question 2

MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2018 katika bajeti tulipisha sheria kwamba kila Halmashauri ni lazima kutenga 10% ya wanawake na vijana watu wenye ulemavu. Hivi sana ninavyozungumza zipo Halmashauri hapa nchini, ikiwemo Wilaya Butiama hawatoi mikopo kama ambavyo sheria tulivyoipitisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujua, nini kauli ya Serikali katika kuhakikisha Wakurugenzi wanatekeleza maagizio ya Bunge kutenga 10% ya wanawake, vijana na walemavu ili kusaidia katika vikundi na kuleta tija kwa wanawake, vijana na walemavu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni kweli kwamba sheria imeshatungwa na kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi ni kwamba huko nyuma hatukuwa na sheria, sasa sheria ipo in place inafanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwapongeze Wajumbe wa Kamati ya Wizara ya TAMISEMI, walikumbusha Wajumbe, walitoa maelekezo kwenye mikoa na Halmashuri zote nchini na wakatoa masharti kwamba kipindi kijacho, kama kuna Halmashauri ambayo haijapeleka fedha hizo kwa mujibu wa sheria, hao watapata taabu sana katika Kamati ile wakati wanaleta bajeti yao mwaka ujao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maelekezo ni kwamba kama umekusanya shilingi 100/=, baada ya kuondoa yale makato ya kisheria kabla ya kupeleka zile fedha kwenye makundi muhimu yaliyotajwa, ni lazima 10% ya fedha hiyo ipekwe kwenye vikundi na igawanywe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama Halmashauri ya Butiama haijapeleka fedha, najua walipokuja kwenye Kamati ya Bunge walikuwa wameweka asilimia ndogo karibu 15% au 25% ambayo wakikuwa wamepeleka, lakini tumepata manung’uniko ya hapa na pale; Mheshimiwa Mbunge najua ni mwenyeji mkaazi wa Mkoa wa Mara, naomba nitoe maelekezo tupate taarifa mahsusi kwa Halmashauri ya Butiama kama kweli hawajapata fedha hizi. Mkurugenzi, ikifika kesho saa 7.00 tupate taarifa kama amepeleka fedha kiasi gani; vikundi gani vimepelekewa? Ili tuweze kumaliza jambo hili. Ahsante.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:- Madeni ya Halmashauri hususan mikopo ya vijana na wanawake ya miaka ya nyuma kabla ya mwaka 2016 yamekuwa hayalipiki kutokana na Halmashauri nyingi kutokuwa na mapato ya kutosha kuendesha Halmashauri hizo hasa miradi ya maendeleo. Je, ni kwa nini madeni hayo yasifutwe ili kuondoa hoja za ukaguzi kwenye Halmashauri hizo?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Fedha nyingi hizi zimepotea kwa sababu ya maamuzi ya kisiasa ya kutoa hii mikopo, lakini mwarobaini tumeupata, ni hii sheria tuliyotunga hapa. Ila sasa ni lini Serikali italeta kanuni (najua zimeshaanza kuandaliwa) ambazo zitasimamia ugawaji wa hizi pesa ili kukomesha kabisa ugawaji holela wa hizi fedha na kuwabana hawa Wakurugenzi waweze kuzitoa vizuri?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Bahati nzuri Mheshimiwa Selasini ni Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya TAMISEMI na Utawala na mojawapo maelekezo ambayo yalitoka kwa Waziri wa Nchi, Mheshimiwa Selemani Jafo ilikuwa kanuni hizi zitolewe mapema iwezekanavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe taarifa kwamba kanuni hizi zimeshatolewa, ilitangazwa kwenye gazeti la Serikali, zinasubiri utekelezaji. Kwa hiyo, kimsingi jambo hili limeisha; na mambo yote ambayo Kamati ilielekeza na maoni ya Waheshimiwa Wabunge yamezingatiwa; namna ya kugawanywa, namna ya kusimamiwa na hatua za kinidhamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hata kama kuna vikundi vitakopeshwa fedha, wasipozingatia sheria na kanuni watawajibishwa. Hili ni jambo la kikundi husika ili fedha hii iweze kwenda vizuri kama ambavyo Bunge na Serikali ilikusudia kuboresha maisha ya Watanzania hawa.